6/recent/ticker-posts

Taaluma ya Mwezi wa Ramadhani bado ipo – Waziri.

Na Mwandishi Wetu. 
Waziri wa Katiba na Sheria Zanzibar amesema kuwav hakuna sababu yoyote nzito ya kutunga sheria juu ya wananchi wanaovyunja sheria katika mwezi mtukufu wa Ramadhani.

Waziri wa Habari Utamaduni Utalii na Michezo Zanzibar Said Ali Mbarouk, alisema hayo jana barazani kwa niaba ya Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Abubakar Khamis Bakar, katika kikao hicho cha baraza la Wawakilishi wakati akijibu suali la msingi liloulizwa na Mwakilishi wa jimbo la Muyuni Mhe, Jaku Hashim Ayoub,alipotaka kujua ni kwa nini Serekali haiyoni haja ya kutunga sheria ya kulinda utamaduni mzuri wa kuheshimu mwezi mtukufu wa Ramadhani kwa wale wanaovuja sheria kwa makusudi.

Sambamba na hilo lakini mwakilishi huyo alitaka kujua Serekali inatoa kauli gani unapofika mwezi mtukufu wa Ramadhani kuhusu vitendo hivyo vinavyokwenda kinyume na utamaduni.

Waziri Mbarouk alisema ni wajibu kwa Waislam kuelimishana mara kwa mara ili kujua zaidi wajibu wao katika mwezi wa Ramadhani na miezi mengine.

Serekali ya Mapinduzi Zanzibar tokea enzi zilizopita hadi leo kila unapowadia mwezi Mtukufu wa Ramadhani imekuwa ikitoa kauli juu ya Wananchi na Waislam kuheshimu mwezi huo.


Alisema kauli ya kwanza hutolewa na Mhe Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt. Ali Mohamed Shein, mwezi wa Shaaban na kauli nyegine hutolewa na Waziri wa Katiba na Sheria Zanzibar  ambapo na Mufti wa Zanzibar na Masheikh nao huelimisha jamii kuhusu utukufu wa mwezi huo na vipi waislam wanatakiwa kuuheshimu.

Waziri Mbarouk alifahamisha kuwa katika kauli hizo hulazimika hoteli zote zifungwe wakati wa mchana watu wavae nguo zenye stara, pia kutokula ovyo mchana wasilewe, wasaidiane na kuoneana huruma na kuheshimiana na kutokana na maagizo hayo kwa kiwango kikubwa yanatekelezwa .


Aidha aliwataka Waislam kuripoti matukio ya aina hiyo ambyo yatavunja heshima ya mwezi Mtukufu wa Ramadhani.        

Post a Comment

0 Comments