6/recent/ticker-posts

Ushauri nasaha ndio suluhisho la kumbadilisha tabia mtoto

Na Bakar Mussa, Pemba 
Walimu wa Ushauri Nasaha Kisiwani Pemba, wameshauriwa kuwa karibu sana na Wazazi wa Wanafunzi hasa wale wenye tabia zisizo za kawaida ili kuweza kupata mafanikio ya haraka ya kuwabadilisha tabia zao.
Akizungumza na Walimu wa Ushauri Nasaha kwa Skuli 53 za Kisiwani humo huko katika Skuli ya Sekondari Madungu,Afisa wa kitengo cha Stadi za Maisha kutoka Wizara ya Elimu Pemba, Khamis Haji Hamad , alisema kuwa Bakora sio suluhisho linaloweza kumbadilisha tabia mtoto wa aina hiyo na badala yake Ushauri Nasaha unaweza kumuweka pazuri zaidi.
Afisa huyo alifahamisha kuwa Walimu hao wanamchango mkubwa wa Malezi iwapo watakuwa bega kwa bega na Wazazi  jambo ambalo linaweza kumuepusha Mtoto wa aina hiyo kuwa mzigo kwa wenzake na Wazazi wake .

Halima Ali Ahmada, Mratibu wa Ushauri Nasaha WEMA Pemba, aliwataka Walimu hao kutowa Mafunzo hayo kwa Wanafunzi wao kwani lengo la kuwepo kwao ni kuwapa Ushauri mbali mbali Wazazi na Walimu ili kuepuka na kujiingiza katika matendo maovu na hatarishi.
Alisema kuwa ni vyema Walimu hao kuwa karibu sana na Wazazi wa Watoto bila ya woga ili kuwepo mashirikiano ya pamoja ya malezi yenye maadili mema ambayo hayatakuwa na Vishawishi.
Kassim Hamad Khamis, Mwalimu Mkuu wa Skuli ya Mkia wa Ng’ombe Pemba, alieleza kuwa mafunzo yatawasaidia sana kwa vile wamekuwa wakikaa pamoja na Watoto wenye tabia na Mazingira tafauti ambazo zinaweza kurekebishika kwa kuwapa Ushauri Nasaha.
“ Mbinu tunazopatiwa za Ushauri Nasaha zinaweza kutusaidia vya kutosha kwa kujenga Taifa lenye Vijana wenye Maadili mema”,alisema.
Alifahamisha kuwa Ushauri Nasaha ni muhimu zaidi kumfukuza mtoto kuliko Bakora kwa Vile zinamfanya mtoto kuwa Mkaidi zaidi.
Nae, Mwalimu wa Ushauri Nasaha wa Skuli ya Msingi Vitongoji ,Mkunga Hamad Sadala, alisema kuwa Wanafunzi sasa hivi wamekuwa wakijiingiza katika mambo mbali mbali ya Anasa kama vile Mapenzi ya ya Umri mdogo,  madawa ya kulenya nk, hivyo mafunzo hayo wanayopatiwa mara kwa mara yatawasaidia kuwatowa Wanafunzi katika Dimbwi hilo hatarishi hasa wale wanaoingia katika rika la Utuuzima(Balekhe).
“Mafunzo haya ya mara kwa mara tunayopatiwa yanatusaidia sana ili kukabiliana na Watoto wenye wenye Changamoto na Vishawishi mbali mbali vya Kimaisha,” alisema Mkunga.
Hivyo alisema kuwa Suala la Mapenzi kwa Wanafunzi ni tatizo  kubwa na kama sio mafunzo hayo ya Ushauri Nasaha wanayopatiwa Taifa lingekuwa hali mbaya zaidi.

Post a Comment

0 Comments