Habari za Punde

Mtazamo wa Jamii ya Kizanzibari juu ya Utalii




                Mtazamo wa Jamii ya Kizanzibari juu ya Utalii

Semina ya “Dhana ya Utalii kwa wote”. Iliyoandaliwa na Kamisheni ya Utalii Zanzibar, Hoteli ya Bwawani
  18 Juni, 2012
Mtayarishaji na muwasilishaji Mada:  Dkt. Issa H. Ziddy, Chuo Kikuu  (SUZA


      Kusafiri kutoka sehemu moja hadi nyengine kwa lengo la kujifurahisha, kujifunza na kupata maarifa ya mambo mapya: المعجم العربي الأساسي
        Kusafiri katika nchi kwa ajili ya matembezi, kusoma, kutafiti na kugundua mambo:    http://islamqa.info/ar/ref/87846

   Malengo ya Utalii

      Kujifurahisha: Kujiliwaza kwa kutembelea mandhari za kipekee na za kuvutia
      Kijamii: kutembelea wapenzi, ndugu na jamaa
      Kielimu: mafunzo, na kubadilishana uzowefu
      Kiutamaduni: maonesho, michezo, sanaa, matamasha, sherehe za kijadi, kimila, kuzuru majengo na sehemu za historia.
      Kidini: kuzuru miji mitakatifu, majumba, sehemu tafauti za ibada.

Historia ya Utalii Zanzibar

Utalii enzi hizo 

      Zanzibar imevutia watalii wengi mno hata kabla ya kuzaliwa Nabii Issa. (W. H. Ingrams, Zanzibar its History and its people + جهينة الأخبار في تاريخ زنجبار )
      Sababu kuu: Eneo ilipo, hewa mwanana, mandhari na fukwe nzuri, tamaduni anuwai (Idrisi, Ibnu Khalduun, Abu Zayd Hassan, AlBiruni, Ibn Batuta, Abulfeda, Captain James Lancanster  1592, Mr. Burton nk)

Watalii walitoka Afrika, Arabuni, Asia, Bara Hindi, Ulaya na Marekani (A guide to Zanzibar

Historia
      kuanguka kwa bei ya zao la karafuu katika soko la dunia kwenye miaka ya 1970 na 80, kuliporomosha ukuaji uchumi Zanzibar
      utalii ukahuishwa na kuwa njia mbadala ya kukuza uchumi wa Zanzibar.
Maeneo ya Marikiti Darajani mwaka 1917
      Idadi ya watalii iliongezeka sambamba na kuongezeka idadi ya mahoteli, nyumba za kulala wageni, vivutio vya utalii na ajira

Maoni ya baadhi ya Wazanzibari
      Mvutano baina ya mahitaji ya utalii na mporomoko wa maadili na dini
      Serikali inajali zaidi mazingira yatayokuza utalii, wakati jamii zinatoa aula  kwenye maadili na dini
      Matokeo yake ni suitafahamu baina ya pande mbili hizo na kutoshiriki katika shughuli za kitalii au hata kuupiga vita.

Mtazamo wa Uislamu kuhusu Utalii
      Je utalii unaruhusiwa katika dini ya Kiislamu?
      Kama jawabu ni ndio; Je ni utalii wa aina gani unaoruhusiwa?
      Je kuna mipaka na vigezo vyovyote vya utalii katika Uislamu?
      Je kuna nchi za Kiislamu zinazokuza uchumi wake kwa shughuli za utalii?

Hukmu ya Utalii katika Uislamu
      Utalii unaofuata misingi na miongozo inayokubaliwa na Uislamu ni halali (مندوبة) (Dkt. Hussein Hussein Shihata – Azhar University)
      Aya ya 9 ya Sura ya Ar-ruum na Aya ya 13 ya Sura ya Al-hujraat
      madua’at” , “Tabliigh” na wafanya biashara, Mahujaji ni mfano
  
Faida za Utalii unaokubalika katika Uislamu

      Ni nyenzo inayosaidia malezi ya kiroho na kiimani. (Al’imraan: 191)
      Ni nyenzo ya kujuana na kutambuana. (Al-hujraat: 13)
      Ni nyenzo ya utekelezaji wa baadhi ya ibada
      Husaidia “Tabliigh”. - hupata kipato, Taaluma
      Utalii wa biashara ndio ulioeneza Uislamu ZNZ
      Husaidia kukuza nafsi na kupumzisha mwili    

Mipaka ya Utalii katika Uislamu

      Uwe unalinda akili, nafsi, familia/jamii, mali, mazingira na ibada – Wasio waislamu hawakatazwi kutalii ktk jamii za Kiislamu
      Uwe ktk nyanja za uhalali ktk kauli, amali na tabia (Fatwa nambari (332 / 26) na (224 / 26)  ya "اللجنة الدائمة" )
      Uwe unahifadhi maadili, mila, utamaduni, mwenendo na vipaumbele vya halali vya jamii
      Uwe unachangia uchumi na maendeleo ktk jamii
      Usipelekee kufanya dhambi na israfu
 kuondosha dhana kuwa hapana tija ya utalii bila ya kuwapo ulevi, uasharati, kamari nk

Nchi za Waislamu na Utalii ...

      OIC inahamasisha uatalii na inalitambuwa Shirika la Utalii Duniani (WTO)
      Benki ya Kiislamu ya (IDB) inafadhili Utalii
      Licha ya kutangaza kufuata sera za Kiislamu, Malaysia imekuwa ni nchi ya 14 duniani kwa kupokea watalii wengi wa kimataifa mwaka 2005 kwa mujibu wa ripoti ya WTO. Katika Commonwealth ni nchi ya tatu
      Faida za watalii wanaotoka nchi za Kiislamu
      Malaysia na Maldives zimevutia watalii wa dunia kwa kauli mbiu ya Tourist Friendly na Muslim Friendly
      Uturuki na Malaysia zimeshinda msimu wa Utalii wa mwaka 2001-2002
      Tukio la kigaidi la Septemba 11, 2011 limepelekea kuwapo kwa (Religious/Islamic Tourism)
      Umuhimu wa kujitambulisha waziwazi katika dunia kuhusu sera za utalii zinozofuatwa
      Saudia inakuza uchumi wake kwa utalii pia 

Tathmini ya Utalii wa Zanzibar

      Je malengo yake yanaendana na haja ya jamii?
      Je kuna uwiano baina ya uchumi na maadili ya wanajamii?
      Je waanajamii wazanzibari wanashirikishwa?
      Je muamala wa utalii unaendana na maadili ya jamii?
      Je Utalii wa ZNZ ni kwa ajili ya uchumi na pesa tu au pia kutunza maadili na utamaduni?

Maoni ya mwisho

Dk Ziddy Akiwafundisha Watalii kuvaa mavazi ya kiasili ya Mzanzibari
      Juhudi zifanywe ili kuondosha dhana kwamba  kazi za Utalii ni za kihuni.
      Kutilia mkazo utalii unaoonesha silka na hali halisi ya ZNZ na sio kuharibu historia
      Kutilia mkazo vivutio vya utalii vinavyochunga maadili ya jamii ya Zanzibar kama nguo, lugha, uvuvi, kilimo, taaluma vyuo vya kielimu nk
      Kuwa na watembezaji watalii wanaoijua Zanzibar na historia na wenye maadili mema

Maoni…

Dk Zidy akiwa na Watalii waliovaa vizuri mavazi yetu ya kiasili
      kuandaa vipeperushi vingi vinavyoonesha maadili ya Mzanzibari na kuwaomba wageni kwa lugha ya kidiplomasia waheshimu maadili hayo
      Kutangaza utalii katika nchi za Kiislamu na kuzifanya huduma ziwe rafiki  kwa watalii wa nchi hizo na nyenginezo.
      Kuwaandalia watu wa ndani sehemu na kuwashajihisha kutalii.

Ahsanteni kwa Kunisikiliza.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.