Na Bakar Mussa, Pemba
Shirika la Biashara la Taifa ( ZSTC)
Zanzibar, limekabidhi msaada wa Bidhaa mbali mbali kwa Mkuu wa Mkoa wa
Kaskazini Pemba, Mheshimiwa , Dadi Faki Dadi, wenye thamani ya Tshs,
5,325,000/=, kwa ajili ya kuwasaidia Wananchi waliofikwa na maafa ya kuunguliwa
na Moto wa Shehia za Shumba Mjini na Maziwa Ng’ombe katika Wilaya ya Micheweni
.
Akikabidhi msaada huo kwa Mkuu wa MKoa wa
Kaskazini Pemba, MKurugenzi Mwendeshaji wa Shirika hilo, Mwanahija Almas Ali,aliwataka
Wananchi hao kuwa na subra katika kipindi hichi kwani yaliotokezea yote ni
maandiko kutoka kwa Mwenyeezi Mungu na kila Mmoja ameguswa na Mtihani huo ambao
unaweza kutokezea kwa mtu yoyote.
Akizungumza na Wananchi hao huko katika
Viwanja vya Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Micheweni Pemba, Mkurugenzi huyo alisema
kuwa Mtihani wowote unatokezea basi huwa umepangwa na Allah hivyo aliwasisitiza
kuwa na subra na wapokee msaada huo ambao umetolewa na ZSTC, na iko pamoja nao
na itaendelea kusaidiana nao kwa kadri ya Uwezo wao utaporuhusu.
“ Shirika letu linaguswa na Mtihani huu na
liko pamoja nanyi na halitosita kuwasaidia kwa kadri Uwezo wetu utaporuhusu”,
alisema, Mwanahija.
Mkurugenzi huyo , alieleza kufurahishwa
kwao na juhudi zilizo chukuliwa na Wananchi wa Shehia ya Maziwang’ombe katika
Wilaya hiyo ya kuamuwa kuwajengea Wananchi Nyumba za kuishi kwa haraka sana na
kuahidi kuchangia Tshs, 400,000/= kwa ajili ya kuongezea Matufali kwa ajili ya
kuendeleza Ujenzi huo ambapo Nyumba nne tayari zimeshajengwa kwa kutumia
Matufali ya kuchongwa kwa wale walaiofikwa na mtihani wa kuunguliwa na moto
Majumba yao.
Akipokea Msaada huo wa Bidhaa mbalimbali
ikiwemo Mchele, Unga wa Ngano, Sukari , Mafuta ya kula na Maharage, Mkuu wa
Mkoa wa Kaskazini Pemba, Mh, Dadi Faki Dadi,alilipongeza Shirika la ZSTC,
kwa kujali maisha ya Watu wengine hasa
wenye matatizo kama hayo na kwamba Msaada huo ameupokea kwa furaha kubwa na
utawafikia Wahanga wa tukio hilo kama ulivyokusudiwa.
Alisema kuwa Utamaduni wa kusaidiana kwa
Watu ambao wamekuwa wakikabiliwa na matatizo kama hayo ulikuwepo miaka mingi
iliopita na kwamba ni Vyema Wananchi kuendeleza Utamaduni huo , na kuyataka
Mashirika na Watu wengine wenye Uwezo kuiga mfano wa Shirika hilo la ZSTC.
Masheha wa Shehia hizo, Rahma Moh’d Shaame
wa Shehia ya Shumba ya Mjini, na Asha Yussuf Hassan, wa Shehia ya Maziwa
Ng’ombe, alieleza kuwa ni jambo la faraja kuona kuwa Serikali iliposikia
Wananchi wake wamefikwa na Mitihani kama hiyo haikukaa kimya na badala yake
wakafuata moja kwa moja kuja kuwafariji hiyo inwapa myo Wananchi hao kuona kuwa
Serikali na Viongozi wao inawajali.
Wakizungumza na Mwandishi wa habari hizi
huko katika Viwanja vya Ofisi ya mkuu wa Wilaya ya Micheweni Pemba, kwa pamoja
walieleza kwamba wamefurahishwa namna ya Viongozi wa Serikali na wale wa Vyama
vya Siasa na Mashirika na Watu binafsi kwa walivyoguswa na Mtihani huo
uliotokezea kwa Wananchi wao na kuonesha moyo wa kutowa misaada mbali mbali ya
kiutu kwa Wahanga hao.
“ Mtihani uliopita kwa Wananchi wa Shehia
zetu ni mkubwa lakini yote ni maandiko kutoka kwa Mwenyeezi Mungu , lakini kwa
vile Wananchi kutoka mbali mbali kuona wanaguswa na mtihani huu tuliopewa na
wakaamuwa kutusaidia tumefurahi ijapo tuna machungu, “alisema , Sheha wa Shehia
ya Maziwang’ombe , Asha Yussuf.
Haji Ali Kombo (70) Mkaazi wa Shehia ya
Maziwang’ombe ni mmoja wa Wahanga hao, ambae aliunguliwa na Nyumba yake,
alisema kuwa anaipongeza Serikali ya Mapinduzi kwa kuona kuwa lilotokezea na
Mtihani wa Allah, na kuwafika kwa haraka Wananchi kuwafariji na kuwasaidia
jambo ambalo limewatia moyo na kuona kuwa Viongozi wao wanawajali Wananchi wao.
Kombo Shineni Ali (25) mkaazi wa Maziwa
Ng’ombe, ni miongoni mwa Wahanga hao , ambae alimueleza Mwandishi wa habari
hizi kwamba ni wazi kwamba Serikali inawajali Wananchi wake hasa wanapokuwa na
Mitihani kama hiyo na kuwa karibu nao kwa hali na mali ili kukabiliana na
matatizo yao.
Alisema kuwa ” tunayashukuru Mashirika
mbali mbali ikiwemo ZSTC, na wale watu binafsi ambao wamekuwa wakitusaidia kwa
hali na mali na kwamba tunawaomba wasisite kufanya hivyo na mola atawalipa lao
fungu”.
Kombo Faki Kombo (70) mkaazi wa Shumba ya
Mjini ni miongoni mwa Wahanga hao, ambae alisema kuwa Wananchi wa Zanzibar
hawana budi kurejesha Utamaduni wa Kusaidiana hasa pale wanapofikwa na mitihani
kama hiyo iliotokezea ni jambo la kutia moyo kuwaona Wananchi mbali mbali
wamekuwa karibu sana na wale waliofikwa na mtihani huo.
Massoud Ali Khamis (48)mkaazi wa Shumba ya
Mjini, ni miongoni mwa Wahanga hao, ambae alilipongeza shirika la ZSTC ,kwa
kuonesha moyo wa kuguswa na Mtihani huo na kuamuwa kuwasaidia Binaadamu
wenzao waliofikwa na maafa kama hayo.
Misaada mbali mbali ya Kibinadamu imekuwa
ikitolewa na Serikali , Mashirika, Taasisi na Watu mbali mbali kwa ajili ya
Wahanga hao , ikiwemo Chakula , Nguo, Fedha Taslim, Vyombo vya matumizi nk
No comments:
Post a Comment