6/recent/ticker-posts

Polisi yatinga nusu fainali Mapinduzi Cup baada ya kuwaondoa mabingwa watetezi KCC kwa penelti

Mabingwa watetezi wa kombe la Mapinduzi, KCC ya Uganda imeyaaga mashindano hayo baada ya kutolewa kwa penalti 5 kwa 4 na makamo bingwa wa ligi ya zanzibar timu ya Polisi Zanzibar.

Mchezo huo wa robo fainali ya pili uliochezwa majira ya saa 9 alasiri na kuhudhuriwa na kamishna wa Polisi Zanzibar, Hamdani Makame, vijana wa polisi ambao walionekana kucheza mchezo huo kwa kujilinda zaidi katika muda mwingi wa mchezo huo na kuwafanya KCC kuutawala mchezo huo.

Mbali na kamishna huyo pia mchezo huo ulishuhudiwa na Rais wa shirikisho la soka la Tanzania aliyeambatana na kocha mkuu wa Taifa Stars, Polisi ililazimika kuwa makini muda wote kutokana na washambuliaji Willium Wadri na Saka Mpima kulisakama lango la Polisi na kokosa nafasi nyingi za kufunga.

Hali hiyo iliendelea hadi kukamilika kwa mchezo huo na ndipo mikwaju ya penalti ikachukua nafasi yake ambapo timu ya Polisi walioanza kupiga penalti hizo na kupata 3 kati ya 5 sawa na KCC ndipo zilipoongezwa penalti moja moja na Polisi kukwamisha wavuni 2 na KCC 1.


Waliofunga kwa upande wa mabingwa hao walioutwaa mwaka jana baada ya kuifunga simba 2 – 0 ni Tom Masiko, Ronnie Kiseka, Mpiima Saka na Kasule Owen wakati Ntege Ivan na Wadri Willium penalti zao ziliishia mikononi mwa golikipa wa polisi Nassir Suleiman kabla ya Namwanya Simon penalti yake kugonga nguzo na kutoka nje.

Kwa upande wa Polisi ni waliofunga ni Daniel Justine, Mohamed Seif, Abdalla Mwalim, Mohamed Salim na Ali Khalid huku penalti za Juma Ali na Suleimani Makungu zikiota mbawa na kutoka nje.


Kwa matokeo hayo Polisi itacheza na Simba katika mchezo wa nusu fainali utakaochezwa siku ya jumamosi katika uwanja wa Amaan.

Post a Comment

0 Comments