Habari za Punde

Fastjet kunusuru Makundi maalum na kuendelea kurahisisha usafiri wa anga


Na Mahmoud Ahmad,Arusha
SHIRIKA la ndege la Fastjet nchini Tanzania limesema litaendelea kutoa huduma za usafirishaji kwa bei nafuu pamoja na kusaidia makundi maalum katika jamii ikiwa ni pamoja na watoto yatima na watoto wenye ulemavu wa ngozi ili waweze kupata elimu  hatimaye kukabliana na mazingira wanayoishi .

Meneja wa Fastjet  Afrika Mashariki Jimmy Kibati akizungumza na waandishi wa Habari Jijini Arusha janaa wakati akitoa ufafanuzi wa safari mpya za Entebe  Kilimanjaro  na Mwanza  kuwa  hatua hiyo ni kuendelea  kuboresha huduma ya usafiri wa anga ikiwa ni pamoja na kuzidi kupunguza bei kwa wateja wao ili wapate fursa ya kutumia usafiri huo.

Bw,Kibati alisema kuwa tayari   pamoja kuwa wanatoa huduma za usafiri ,wameweza kuwawezesha madaktari bingwa sita wa meno kwenda Mkoa wa Shinyanga kwenda kuhudumia  watoto wanaotoka katika mazingira magumu,wenye matatizo ya meno na kuwa suala la kuhudumia jamii linapewa kipaumbele na Shirika hilo .

Akitoa ufafanuzi wa huduma za Shirika hilo alisema kuwa wameanza kutoa safari tatu katika siku za Jumanne ,Alhamisi na Jumamosi  na kuwa safari hizo ni za Kilimanjaro na Entebe na zitaanza tarehe 31 March 2015

Alisema kuwa Safari ya Entebe na Kilimanjaro itafungua fursa kwa wafanyabiashara na kuwa gharama yake ni Tshs 95,000 

Pamoja na mambo mengine alisema kuwa Safari mpya kati ya Kilimanjaro na Mwanza inatarajia kuanza tarehe 30 Machi  2015 kwa nauli   Tshs   35,000 na kuwa safari hiyo itakuwa mara nne kwa wiki ikiwa ni siku ya Jumatatu ,Jumatano na Jumapili

Kimsingi alisema kuwa wateja wanaweza kupanga safari zao kupitia tovuti  ya Fastjet inayojulikana kwa www.fastjet.com 

Alitaka wateja wa Shirika hilo kufanya utaratibu wa usafiri mapema ili waweze kulipa nauli nafuu

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.