Habari za Punde

Hutuba ya Mwenyekiti wa Bodi ya BOA Balozi Mwanaidi Maajar Wakati wa Ufunguzi wa Tawi la Bank Of Africa Mlandege Zanzibar.

HOTUBA YA MWENYEKITI WA BODI YA WAKURUGENZI WA BANK OF AFRICA - TANZANIA BALOZI MWANAIDI SINARE MAAJAR WAKATI WA UZINDUZI WA TAWI JIPYA LA BANK OF AFRICA ZANZIBAR, TAREHE 3 MACHI 2016

Mheshimiwa Mgeni rasmi, Waziri wa fedha wa Serikali ya 

Mapinduzi ya Zanzibar, Ndugu Omar Yussuf Mzee,

Mkurugenzi mtendaji wa BANK OF AFRICA - TANZANIA, 

Ndugu Ammish Owusu- Amoah,

Wakurugenzi wa Bodi,

Wapendwa wateja,

Wafanyakazi wa BANK OF AFRICA - TANZANIA,

Ndugu Waandishi wa Habari,

Mabibi na Mabwana,

Ninayo furaha kubwa kuwakaribisha nyote katika tukio hili 

muhimu la kihistoria kwa BANK OF AFRICA - TANZANIA. 

Namshukuru Mwenyezi Mungu mwingi wa Rehema kwa 

kutuwezesha sote kuwa hapa leo, na pia shukrani zangu za dhati 

kabisa ziende kwa mgeni wetu rasmi, Mheshimiwa Omar Yussuf 

Mzee - Waziri wa Fedha wa serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar 

kwa kuchukua muda adhimu nje ya ratiba yake yenye 
mambo mengi muhimu ya kitaifa na kuweza kujumuika nasi katika kuadhimisha uzinduzi huu wa Tawi letu jipa la BANK 
OF AFRICA hapa Zanzibar.

Napenda pia kuwakaribisha wakurugenzi wetu wa bodi ya BANK 

OF AFRICA, wateja wetu wapendwa na sote tuliojumuika hapa 

jioni hii ya leo kushuhudia BANK OF AFRICA – TANZANIA 

ikipiga hatua nyingine katika kukuza mtandao wa benki yetu 

Tanzania. 


Mabibi na Mabwana

BANK OF AFRICA - TANZANIA ni benki ya kibiashara 

ilioanzishwa Juni 2007 hii ni baada ya kuinunua Eurafrican Bank 

iliokuwepo Tanzania tangu Septemba 1995 ikiwa na matawi 

matatu. BANK OF AFRICA ipo katika nchi 18 za Africa na yenye 

makao makuu yake Dakar, Senegal. Kwa hapa nchini Tanzania 

BANK OF AFRICA ina makao makuu yake jijini Dar es Salaam  

tayari ikiwa na matawi 22 pamoja  na kituo kimoja cha biashara 

pale Dar es Salaam kwajili ya kuhudumia wateja wakubwa. 

Katika miaka 9, BANK OF AFRICA - TANZANIA imeonyesha 

maendeleo mazuri na hata kujichukulia nafasi nzuri miongoni mwa 

benki muhimu katika sekta ya kibenki nchini Tanzania. Benki 

imeleta mchango endelevu kwa watanzania. Hili linaonyeshwa na 

uwezo wa benki kupeleka matawi yake katika maeneo mbalimbali 

ya Tanzania ikiwemo:  Dar es Salaam, Arusha, Dodoma, Moshi, 

Mwanza, Mbeya, Tunduma, Morogoro, Kahama, Mtibwa na 

Mtwara. Katika miaka hii tisa pia benki imeweza kutengeneza 

faida zaidi ya billioni 7 za kitanzania.

Katika kutambua mahitaji ya wateja BANK OF AFRICA inakuja 

na huduma stahiki ambazo zitaweza kumfikia kila mzanzibari kwa 

urahisi zaidi hii ni katika kutimiza ari ya benki isemayo “focused 

on development in the heart of Africa” yaani: kulenga maendeleo 

katika moyo wa Africa. Bodi ya wakurugenzi pamoja na uongozi 

wa BANK OF AFRICA umeendelea bila kuchoka kuweka nguvu 

katika maendeleo ya kila mtanzania hii ikionyeshwa na uamuzi wa 

benki kufungua tawi hili la 22 la BANK OF AFRICA ZANZIBAR.

Mabibi na Mabwana

Takwimu zinaonyesha Zanzibar imeendelea kujenga uchumi imara 

na endelevu, ufanisi katika mfumo wa fedha ni moja ya mahitaji ya 

muhimu na ya msingi katika ukuaji wa uchumi na maendeleo kwa 

ujumla. Tukiwa na hili akilini BANK OF AFRICA iliona 

umuhimu wa kuwekeza hapa Zanzibar ili kuendeleza ukuaji wa uchumi. BANK OF AFRICA – TANZANIA imetengeneza huduma katika muundo bora ambao ni rahisi kutumia na utakao mfaa kila moja watu kwa mahitaji yake hii ni katika kurahishisha utunzaji wa fedha, utoaji wa mikopo na hata uwekezaji.    

Zanzibar inafahamika kwa uwezo wake mkubwa katika kilimo 

hasa cha karafuu, uvuvi, biashara na utalii. Thamani ya mauzo ya bidhaa na huduma Ilikuwa milioni 229 Dola za kimarekani ikilinganishwa na milioni 203 Dola za kimarekani katika mwaka unaoishia Januari 2014. Thamani ya bidhaa zinazouzwa nje imeongezeka kwa asilimia 23, kwa kiasi kikubwa ukuaji huu wa uchumi umechangiwa hasa na biashara ya viungo, Karafuu ikiendelea kutawala soko la nje na kufikia asilimia 51.8 kuishia Januari mwaka 2015.

Katika kufungua tawi hili jipya hapa Zanzibar BANK OF 

AFRICA- TANZANIA imekuja na huduma zilizotengenezwa rasmi kufikia na kutimiza mahitaji ya wateja wetu. BANK OF AFRICA - TANZANIA pia tupo katika mchakato wa kuangalia jinsi ya kutoa huduma ya “Islamic Banking” ili kuhudumia na kufikia mahitaji ya wateja wetu.

Mabibi na Mabwana

BANK OF AFRICA - TANZANIA tupo hapa ili kuleta mageuzi 

katika sekta ya kibenki tukiweka nguvu zetu zote katika ukuaji wa 

uchumi wa Zanzibar na ukuaji wa sekta ya kifedha. Tupo tayari 

kufanya kazi nzuri na wananchi wa Zanzibar na ninaimani kwamba uwepo wetu utaleta maendeleo ya kiuchumi kwa wananchi wa Zanzibar.  

Napenda pia kuipongeza menejimenti na wafanyakazi wa BANK 

OF AFRICA - TANZANIA, kwa kujitoa kwao na kufanya kazi 

kwa bidii katika kufanikisha hili tunaloshuhudia leo. Bila Juhudi 

zao tukio hili lisinge kuwa na mafanikio haya makubwa 

tunayoyashuhudia.

Kwa maneno haya machache, kwa mara nyingine tena, nichukue 

nafasi hii kumshukuru Waziri wa Fedha wa serikali ya mapinduzi 

ya Zanzibar kwa kukubali kujumuika nasi leo na pia napenda 

kuwakaribisha nyote katika uzinduzi rasmi wa tawi letu jipya hapa 

Zanzibar.

 Asante.


No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.