Habari za Punde

STATE HOUSE ZANZIBAR
OFFICE OF THE PRESS SECRETARY
PRESS RELEASE
    Zanzibar                                                                                                   10 Machi, 2016
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein amemjulia hali Makamu wa Kwanza wa Rais Maalim Seif Sharif Hamad.
Maalim Seif ambaye alikuwa amelazwa katika hospitali ya Hindu Mandal kwa siku kadhaa kwa ajili ya matibabu hivi sasa anapumzika katika hoteli ya Serena jijini Dar es salaam baada kuruhusiwa kutoka hospitalini.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi alifika hoteli ya Serena jana jioni na kumpa pole Maalim Seif na kumuomba Mwenyezi Mungu amponye haraka ili aweze kuendelea na shughuli zake kama kawaida.  
Kwa upande wake Makamu wa Kwanza wa Rais alimshukuru Dk. Shein kwa kufika kumjulia hali na kumuombea apone haraka.
Kuhusu hali yake Maalim Seif alimueleza kuwa hivi sasa anaendelea vizuri na kwamba ameshauriwa na madaktari wake apumzike kwa wiki nane.

Postal Address: 2422 Tel.+255 776 613 015, Fax: 024 2231822 




---

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.