Na. Mwashamba
Juma
Spika wa
Baraza la Wawakilishi Mhe.Zubeir Ali Maulid alisema Zanzibar inaelekea kukaa
kwenye chati ya ramani ya kimataifa kutokana na kuimarika kwa sekta ya Utalii.
Mhe. Maulid
aliyasema hayo huko ukumbi wa Z- Ocean Kihinani, wakati akifungua warsha ya
siku moja kwa Wajumbe wa Baraza la Wawakilishi kuhusu mradi wa ujenzi wa kijiji
cha Utalii Matemwe (Penny Royal) huko mkoa wa Kaskazini Unguja.
Alisema
kukamilika kwa ujenzi huo kutaleta tiba ya changamoto ya ajira kwa wananchi wa
Zanzibar nakueleza kuwa huduma za utalii zinawagusa moja kwamoja Wazanzibari.
Alisema sekta
ya Utalii Zanzibar inatoa mchango mkubwa katika kupunguza makali ya maisha kwa
wananchi wa Zanzibar kutokana na kuchangia kiasi kikubwa kwenye pato la taifa.
Alisema
lengo la warsha hiyo ni kuwafahamisha Wajumbe wa Baraza la Wawakilishi kuhusu
maendeleo ya mradi huo kwani wao ni washauri wakuu katika masuala ya maendeleo
ya nchi. Aidha Aliishauri Wizara ya Habari Utalii, Utamaduni na Michezo kukaa
pamoja na Mamlaka ya Uwekezaji (ZIPA) pamoja na Idara ya Uhamiaji ili kusaidia
ufanikishaji wa mradi huo.
Akizungumzia
utekelezaji wa mradi wa ujenzi huo, Mwanasheria kutoka kampuni ya wanasheria ya
Immma jijini Dar es Salaam ambae pia anasimamia mradi huo wa Matemwe (Penny
Royal), Casper Msika alisema kampuni kupitia mradi wake wa “Amber Reasort”
unampango wa kujenga miundombinu ya mawasiliano, barabara na huduma za jamii
zikiwemo afya maji safi na elimu kwa wananchi wa Zanzibar na wakaazi wa kijiji
cha Matemwe.
Alisema mradi
pia unalengo la kuingia mikataba na maskuli na hospitali za kimataifa kwaajili
ya kuwekeza katika kijiji cha Matemwe na kuongeza kuwa lengo la uwekezaji huo
ni kutoa huduma bora za afya na elimu kwa Wanzibari ili kuwapunguzia gharama za
kuzifuata nje ya nchi yao.
Kuhusu
miundombinu ya barabara, umeme na maji safi alisema mradi unania ya kuzalisha
umeme wake mwenyewe kwani utahitaji megawati 50 za umeme utakaotokana na nishati
ya jua pamoja na taka taka zitakazozalishwa Zanzibar na wanakijiji cha Matemwe.
Aidha alisema
mradi tayari umefanya mazungumzo na ZECO, ZAWA pamoja na Mamlaka ya barabara ambapo
alieleza wana nia ya kujenga kilomita 22 zitakazozunguka eneo la Mashariki na
Magharibi mwa kijiji cha Matemwe kuanzia kijiji cha Kidoti na kueleza kuwa
tayari kilo mita 10 za ujenzi wa barabara hiyo umeanza.
Aliongeza
kuwa mradi pia unalengo la kujenga nyumba za maendeleo zenye nia ya kutunza
haiba ya Zanzibar ambazo zitapewa majina kutokana na uhalisia wa Zanzibar
pamoja na kujenga kiwanja cha ndege kikubwa kwenye kijiji hicho cha Matemwe.
Akizungumzia
maendeleo ya kilimo kwenye mradi huo, Casper alisema wanatajia kuchukua
asilimia kubwa ya wanakijiji kwaajili ya kilimo cha mbogamboga ambao alieleza
mradi utawapatia mafunzo, mbinu na vifaa vya kisasa vya kilimo kwaajili ya
kuekeza kwenye sekta hiyo.
Hata hivyo
alieleza mradi unatarajia kukukamilika baada ya miaka 15 nakuongeza kuwa
utatekelezwa kwa awamu sita tofauti sambamba na kueleza awamu ya kwanza
itakamilika baada ya miaka miwili kwa kutumia gharama za dola za kimarekani
milioni 75 sawa na bilioni sita kwa thamani ya fedha za Tanzania.
Akitoa
ufafanuzi wa mgogoro wa ardhi uliopo baina ya Wanakijiji cha Matemwe na
Mwekezaji wa mradi huo wa Matemwe (Penny Royal), Waziri wa Ardhi, Maji, Nishati
na Mazingira Mhe. Salama Aboud Talib alieleza serikali ilibaini mgogoro huo
baada ya mwekezaji kuanza kulipa fidia kwa wanachi kupitia wakala aliemteuwa
mwenyewe bila kuishirikisha serikali.
Hivyo alieleza Wizara yake imeteuwa
kamati maalum ya kuratibu malaalamiko ya wananchi chini ya uongozi wa Mkuu wa
wilaya ya Kaskazini kwaajili ya kusimamia haki za wananchi.
Akizungumzia
ukubwa wa eneo lililotolewa na serikali kwaajili ya mwekezaji huyo, Waziri
Aboud alisema serikali imempa hekta 411.8 sawa na ekari 1000 kwa sharti la
kuwalipa fidia, kujenga miundombinu ya barabara na maji safi kwa wanachi wa
eneo hilo mbali na mikataba mengine na serikali.
Hata hivyo
alisema serikali inategemea kupata mapato makubwa kutoka kwa mwekezaji huyo
sambamba na kuwaahidi wananchi wa eneo hilo kutoa ushirikiano mzuri ambapo
wakati huu serikali inasimamia na kutatuliwa malalamiko yao.
Mapema
akizungumza na Wawakilishi wa Baraza la Wawakilishi, Mmiliki wa kampuni hiyo ya
Matemwe (Penny Royal), Brian Thomas alisema mradi unalengo la kutoa fursa
nyingi za ajira kwa wakazi wa Zanzibar na wanakijiji cha Matemwe.
“Mradi
hautobadili maisha wa Wamatemwe pekee, bali ni kwa Wananchi wote wa visiwa vya
Zanzibar” alisema Thomson.
Aidha
alitumia fursa hiyo kumshukuru rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la
Mapinduzi, Dkt. Ali Mohamed Shein kwa nia yake njema ya kuwaletea maendelo
wananchi wa Zanzibar kususani kuondosha tatizo la ajira kwa vijana na kinamama
wa vijijini.
No comments:
Post a Comment