Habari za Punde

ZASCCU Yapata Uongozi Mpya Mwenyekiti, Makamo Mwenyeki na Wajumbe 10.

Na Abdi Shamnah
Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, imesema inasimamia na kuendeleza mageuzi ya Vyama vya ushirika kwa kufuata taratibu, kanuni na sera, ili kuwa na vyama vyenye nguvu na vyenye kuleta tija kwa wanachama.
Hatua hiyo inakwenda sambamba na dhana ya umilikishaji wa vyama, ikiwa ni mwelekeo wa kuviunganisha vyama vyote vidogo vidogo a vya kati, ili hatimae kuwa na SACCOS kubwa ya Wilaya.
Hayo yameleezwa kwa nyakati tofauti na Mkurugenzi wa Idara za vyama vya ushirika Daud Simba, katika ufunguzi wa  mikutano mikuu ya ZASCCU kwa Mkoa ya Kusini na Kaskazini Unguja iliyofanyika Tunguu na Kinduni.
Pamoja na mambo mengine mikutano hiyo iliwachaguwa Weneyeviti, Makamo Wenyeviti na wajumbe 10 (kila Mkoa) kwa lengo la  kuunda Bodi ya ZASCCU Taifa, ambapo itaishirkisha Mikoa mitano ya Unguja na Pemba.
Akizungumza na wanachama, Simba alisema kuna umuhimu wa viongozi watakaochaguliwa kushirikiana na SACCOS zilizopo na kufanya akzi ya kuzinganisha ili kuwa na SACCOS moja yenye nguvu, ili kufikia dhana ya kuweka akiba ya kutosha.
Alisema viongozi wana jukumu la kuhamasisha uwekaji wa mitaji, na kufanya uwakilishi na utetezi ili kuvijengea uwezo vyama hivyo.
Aidha aliwataka wanachama hao kutokuwa na imani au huruma dhidi ya wale wote wanaojinufaisha kupitia migongo ya wanachama na kutaka hatua za kisheria zichukuliwe mara moja ili kujenga heshima ya vyama hivyo.
Mapema Mkuu wa Mkoa wa Kusini Unguja Dk.Muslih Hijja, aliwataka wanachama hao kujiamini kwa kila wanachokifanya baada ya kufanya utafiti na kubaini faida na hasara itakayopatikana.
Alisema ili huduma za ufanisi ziweze kupatikana kupitia vyama hivyo, ni wajibu wao kuzingatia suala la  uaminifu, pamoja na kushirikiana katika utendaji wa kazi.
Aidha aliwataka kuwa wabunifu ili kuibuwa mbinu mpya pamoja na kujenga utamaduni wa kujaribu, ili waweze kuongeza tija.
Nae Katiobuy Tawala Mkoa wa Kaskazini Unguja,Mohammed Omar, kwa niaba ya Mkuu wa mkoa huo kuzingatia umuhimu w akuwepo chombo hicho kwa lengo la kujenga nguvu ya pamoja na kusukuma mbele malengo ya kuanzishwa kwa vyam vya akiba na kukopa.
Akizungumzia uchaguzi huo, Omar aliwataka wanachama hao kuchaguwa mgombea kulinga na uwezo alionao ili kufikia malengo ya kuwa na Bodi ya ZASCCU.
Alisema serikali inashajiisha kuwepo kwa vyama imara ili kwenda smabamba na mpango wa serikali wa kukuza uchumi na kupunguza umasikini sambamba na kuibuwa ajira.
Katika chaguzi hizo Ali Makame Juma kutoka North ‘B’ SACCOS, alichaguliwa kuwa Mwenyekiti wa ZASCCU Mkoa wa Kaskzini Unguja, wakati Abdulahalimu Ameir akichaguliwa Makamo mwenyekiti.

Aidha Juma Zungu Ameir alichaguliwa Mwenyekiti ZASCCU Kusini Unguja na Ameir Hashim akiwa Makamo Mwenyekti. 

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.