Mbunge wa Dimani (CCM). Hafidh Ali Tahir amefariki dunia katika Hospitali ya General huko Dodoma. Kwa mujibu wa Wabunge wenzake wanasema juzi Mbunge huyo ambaye ni Kocha Msaidizi alikwenda mazoezini akiwa amevaa suti huku wenzake wakimtania kutokana na vazi hilo lakini mwenyewe alijibu hajisikii vizuri lakini baada ya mazoezi aliendelea na vikao vya kamati tendaji kama kawaida hadi saa nane usiku alipojisikia vibaya na kwenda hospitali mwenyewe kwa gari yake na baada ya saa moja alifariki dunia majirani ya saa tisa usiku. Mwenyeenzi Mungu amsamehe makosa yake na amlaze mahali pema
MICHANGO ISIZUIE MTOTO KUPATA ELIMU
-
Na Angela Msimbira, NZEGA
NAIBU Waziri, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, Mhe.
Zainab Katimba amesisitiza kuwa uchangiaji katika sekta ya...
6 hours ago
No comments:
Post a Comment