Habari za Punde

Viongozi Utumishi wa umma watakiwa kufuata maadili ya utumishi

Na Salmin Juma, Pemba

Viongozi na wakuu wa utumishi wa umma nchini wametakiwa kuwa wakweli na wawazi na kufuata  maadili ya utumishi  ili kutekeleza wajibu  wao kwa jamii.

Mkuu wa Mkoa wa Kusini Pemba, Mwanajuma  Majid Abdalla ameyasema hayo katika ukumbi wa Makonyo Wawi alipokuwa akifungua mafunzo ya siku moja ya umuhimu wa maadili kwa wakuu wa Mikoa ,Wilaya na viongozi wengine wa umma Kisiwani Pemba .

Amesema kama viongozi wanapaswa hufahamu wajibu wao katika utendaji wa kazi wanazozifanya  ili waweze kuaminika mbele ya jamii.

Naye Mwenyekiti wa Tume ya  utumishi wa umma Zanzibar, Asaa Ali Rashid amesema  lengo la mafunzo hayo ni kutekeleza matakwa ya sheria ya utumishi wa umma ya namba nne ya mwaka 2015 na kukuza uelewa wa maadili kwa  viongozi hao 

Amesema suala la maadili ni la kila mtu katika jamii  hivyo viongozi ni lazima wawajibike ili kuondoa dosari miongoni mwa jamii.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.