Habari za Punde

Jengo la mahakama Mkoani Pemba lipo katika hali mbaya



Na Haji Nassor, Pemba
UONGOZI wa mahakama ya wilaya ya Mkoani Pemba, umeiomba serikali kuangalia uwezekano wa kulihami haraka jengo la mahakama hiyo, kutokana na kuvuja baadhi ya maeneo na kuwapa usumbufu wafanyakazi wakati mvua inaponyesha.

Kauli hiyo imetolewa na Kaimu, hakimu wa mahakama ya wilaya hiyo Nassor Suleiman, alipokuwa akiwasilisha taarifa ya utekelezaji, kwa Naibu waziri wa wizara nchi afisi ya rais, Katiba, sheria utumishi wa umma na utawala bora, alipofika hapo na jumbe wake, ikiwa ni sehemu za ziara yake ya siku mbili kisiwani Pemba.

Alisema kuvuja kwa jengo hilo, wakati wakiwa kazini huwapa mashaka ya kuhama hama na kusababisha kusita kwa kazi, kutokana na kukimbia maji kwa baadhi ya mapaa ya mahakama hiyo.

Hakimu huyo alisema, ingawa lipo paa walipata msaada wa kuezekewa na Baraza la mji Mkoani, wakati wakifanya matengenezo ofisi yao, lakini kwa yaliobakia yapo baadhi yanavunja na juhudi zinahitaji kuokolewa.

“Muheshimiwa Naibu waziri tumeshaona juhudi za serikali za kulifanyia matengenezo makubwa jengo letu la mahakama kuu Chakechake, lakini na hili la wilaya ya Mkoani, hali iko mbaya maana yapo mapaa yanavuja’’,alifafanua.

Aidha alisema changamoto nyengine inayowakumbuka wafanyakazai hao wa Idara ya mahakama Mkoani, ni ukosefu wa usafiri kutokana na kuwa na vespa moja pekee.

Akielezea changamoto nyengine inayowakabili, mfanyakazi wa mahakama hiyo Riziki Mohamed Makame, alisema wanapata ugumu wa kusambaa baruza za wito ‘smears’ kwa wahusika.

“Mahakama inapotoa barua za wito, inatubidi tutumie nauli zetu, na kumuomba mtuhumiwa au mlalamikaki ni kosa, sasa kama tukiwa na usafiri wetu, kazi itafanyika vyema.

Nae mfanyakazi Muhidin Mohamed Muhidin, amelalamika kutoingizwa kwenye orodha ya posho la shilingi 50,000 ingawa wenzao wa Unguja wameshaanza kupata.

Akilitolea ufafanuzi hilo, Afisa Utumishi wa wizara hiyo Chumu Khamis Omar, alisema lililojitokeza hadi wafanyakazi wa Pemba, kuchelewa kuingizwa kwenye posho hilo, ni kuchelewa kupewa taarifa kutoka makao makuu Unguja.

“Ni kweli wafanyakazi sasa kuna posho la mazingira magumo, kutoka shilingi 20,000 hadi shilingi 50,000, lakini kwa sisi wafanyakazi wa Pemba, tulichelewa maana taarifa zilichelewa kutufikia’’,alifafanua.

Mapema Naibu waziri wa nchi afisi ya rais Katiba, sheria Utumishi wa umma na utawala Bora Zanzibar, Khamis Juma Maalim, aliwapongeza wafanyakazi hao licha ya changamoto zinawazowakabili.

Kwa upande wake Naibu Mrajisi wa Mahakamu kuu Zanzibra Ali Ameir, alisema kutokana na changamoto zinazowakabili wafanayakazi hao, na kufanikiwa kufanya kazi, ile dhana ya hapa kazi imewadia.

Ujumbe huo wa Idara ya mahakama ikiambatana na Naibu waziri wa wizara hiyo, wamekamilisha ziara ya siku mbili kisiwani Pemba, ambapo walitembelea jengo la mahakama kuu Chakechake lililofanyiwa ukarabati, mahakama za Konde, Wete, Kengeja na Mkoani.

Wakati huo huo Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi dk: Ali Mohamed Shein, anatarajiwa kuwa mgeni rasmi wa ufunguzi wa jengo la mahakama kuu Chakechake lililofanyiwa matengenezo makubwa.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.