Habari za Punde

Maadhimisho ya Siku za Haki za Binaadamu Duniani Kisiwani Pemba.

Afisa mfawidhi  Kutoka tume ya haki za binaadamu na utawala bora Pemba Bw Suleiman Salim Ahmad akitoa majibu ya maswali mbalimbali yaliyoulizwa katika maadhimisho ya siku ya haki za binaabadamu yaliyofanyika huko chakechake mkoa wa kusini Pemba chini ya kituo cha Huduma za sheria afisi ya Pemba
Mratibu wa kituo cha huduma za sheria afisi ya Pemba Bi Fatma Khamis Hemed akitolea ufafanuzi michango na maswala mbalimbali yaliyoulizwa na washiriki katika maadhimisho ya siku ya haki za binaadamu yaliyoandaliwa na kituo hicho

Meneja wa Zanzibar Saving and Credit  co-operative Union ( ZASCCU) Omar Abdalla Ali akiuliza swali katika maadhimisho ya siku ya haki za binaadamu yaliyofanyika leo huko chakechake Pemba na yaliyoandaliwa na ZLSC afisi ya Pemba ambapo alitaka ufafanuzi  kwanini kituo kimejikita zaidi kwa akinamama wakati haki ni kwa wote. 
Mshiriki wa maadhimisho ya siku ya haki za binaadamu yaliyoandaliwa na kituo cha huduma za sheria leo huko chakechake Muhammed Ali Muhammed akitaka ufafanuzi juu ya kesi zinazopelekwa  mahakamani ambapo Jaji mkaazi hayupo, jee zinachukuliwa hatua gani
Ibrahim  N. Kombo kutoka JUMAZA akitaka kujua ni kwanini  mahkama inawanyima dhamana washtakiwa na pia kesi kuchukua muda mrefu  bila ya kufikia tamati, ni katika maadhimisho ya siku ya haki za binaadamu huko chakechake pemba,  maadhimisho ambayo yameandaliwa na kituo cha humuda za sheria afisi ya Pemba
Mshiriki   katika maadhimisho ya siku ya haki za binaadamu yaliyofanyika leo huko chakechake Pemba yaliyoandaliwa na ZLSC afisi  ya Pemba bw: Yussuf Abdalla kutoka jumuiya ya maimamu  Zanzibar akiuliza juu ya ucheleweshaji wa upatikanaji wa vyeti vya kuzaliwa kwa watoto unasababishwa na nini.(Picha Salmin Juma - Pemba)

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.