Spika wa Baraza la Wawakilishi Mhe. Zubeir Ali Maulid akizungumza na Msaidizi Balozi katika Ofisi ya Ubalozi wa Iran hapa nchini bwana, Mohammad Dehghani .
Spika wa Baraza la Wawakilishi Mhe. Zubeir Ali Maulid akisalimiana na Msaidizi Balozi katika Ofisi ya Ubalozi wa Iran hapa nchini bwana Mohammad Dehghani .
Spika wa Baraza la Wawakilishi Mhe. Zubeir Ali Maulid akisisitiza jambo wakati alipokuwa akizungumza na Msaidizi Balozi katika Ofisi ya Ubalozi wa Iran hapa nchini bwana Mohammad Dehghani .
Na Himid Choko
Zanzibar
na Jamhuri ya Watu wa Iran zinakusudia kutanua wigo wa mashirikiano katika masuala ya Kibunge ili kubadilishana
uzoefu na mbinu bora za kuendesha
vyombo hivyo duniani.
Aidha
mashirikiano hayo yanalenga kutafuta
mbinu muwafaka zaidi za kuwajengea uwezo wajumbe , pamoja na ushiriki mpana zaidi wa wananchi katika vyombo vyao vya uwakilishi
na utungaji wa sheria.
Makubaliana
hayo yamefikiwa leo hii wakati wa Mazungumzo ya pamoja kati ya Spika wa Baraza
la Wawakilishi Mhe. Zubeir Ali Maulid na
Msaidizi Balozi katika Ofisii ya Ubalozi wa Iran hapa nchini bwana Mohammad
Dehghani .
Mazungumzo
hayo yamefanyika katika Ofisi za Baraza la Wawakilishi Chukwani nnje Kidogo ya
Mji wa Zanzibar.
Viongozi
hao kwa pamoja wamesifu ushupavu mkubwa na kujiamini kwa viongozi wa Jamhuri ya watu wa Iran, suala ambalo linachangiwa na kuwa na bunge
imara la nchi hiyo.
Katika
mazungumzo hayo viongozi hao pia wamekubaliana kuendelea kuenziwa kwa
ushirikiano na uhusiano wa muda mrefu kati ya Zanzibar na Iran hasa katika
masuala ya utamaduni na biashra.
Katika
hatua nyengine msaidizi Balozi huyo wa Ubalozi wa Iran hapa nchini kwa niaba ya
Spika wa Bunge la Iran amemuwalika rasmi
Mheshimiwa Zubeir kutembelea rasmi bunge la nchi hiyo mwezi ujao.
No comments:
Post a Comment