Habari za Punde

Miaka 53 ya Mapinduzi Zanzibar utalii wasonga mbele


Chumba cha chini ya bahari Pemba, chatimiza malengo la Mapinduzi

Na Haji  Nassor, Pemba

‘’JAMANI hicho chumba kinkaa vipi….!!!!….. lakini kiko kweli au ni wazungu tu wanchomoka’’



‘’Tuseme kiko kweli, haya wapita vipi………mambo makubwa…ivyo chumba kikae chini ya bahari kisha puunzi wavuta vipi……?

‘’Mie sio kama si amini vooo….!!!!……lakini wapita vipi hata usirowe….. maana sote hapa twajua kuwa chini ya bahari kuna maji.

Kauli hizi zilisambaa mithili ya mafuta ya taa, kwenye uwekaji wa jiwe la nanga la Chumba cha chini ya bahari, kwenye hoteli ya Manta resort ilipo takriban kilomita 50 kutoka mji wa Chake chake.

Manta resort ni hoteli ya kitalii iliopo kijiji cha Mkangaale Wilaya ya Micheweni Mkoa wa Kaskazini Pemba, lakini hili la chumba cha chini ya bahari, wenyeji na walioshuhudia awali hawakuamini, je wewe unae soma makala hii vipi? nifuate.

Masuali mengi na mazito, wananchi kadhaa waliiohudhuria hapo, walikua wakiuliza na hakukua na hata mmoja aliekuwa akitoa jawabu, likiwadhaniwa kua ni la kweli.

Suali kubwa ambalo lilitawala kwenye sakafu za vyumba vya akili vya watu, lilikuwa je unavutaje pumzi kwenye chumba hicho……!!!!…?

Wapo waliodiriki kusema, kuwa tokea milango ya biashara huria, iliotokana na Mapinduzi matukufu ya mwaka 1964, sasa kila kitu kinawezekana na kila jambo la maendeleo litwasilisi Zanzibar.

Kwa siku ya uzinduzi wa chumba hicho, wakati wa kufika kwa mgeni rasmi matarajiwa wa kuweka jiwe la nanga la chumba hicho (under water room) ambae ni Makamu wa Pili wa rais Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi alifika.

Awali kulitanguliwa na hutuba yake, kwenye shamra shamra za kusherehekea miaka 49 ya Mapinduzi ya Zanzibar kwa wakti huo, laki wengi wao hawakuwa na hamu ya hutuba, bali ni kutaka kujua chumba hicho cha kitalii kikoje.

Masuali haya yakaanza kujibiwa na wakati huo aliekuwa Waziri wa Habari Utamaduni Utalii na Michezo Said Ali Mbaruok, baada ya kudokoa kidogo, juu ya kuwepo kwa chumba hicho ambacho kutoka kwenye fukwe ni kama mita 300, sawa na viwanja vitatu vya mpira wa miguu.

‘’Ngudu wananchi, wakati huu tukisherehekea miaka 49 ya Mapinduzi ya Zanzibar, sasa sekta ya utalii inacho cha kujivunia na kutembea kifua mbele’’,alianza hivyo.

‘’Maana muda mfupi ujao tutawamalizia kiu yenu ya kutaka kujua juu ya chumba hicho cha chini ya bahari na hili ni ishara ya kupevuka na kutanuka kwa sekta ya utalii’’,alieleza Waziri huku akitabasamu.

‘’Mapinduziii…!!!!…..daimaaa…jamani leo tunafuraha..tena Mapinduziii…. daimaa akaitikiwa huku wananchi wakiwa makini kweli na kuvutiwa na chumba cha chini ya bahari ambacho mtu anaweza kulala.

Wakati huu tukisherehekea miaka 53 ya Mapinduzi ya Zanzibar, kwa wananchi wa Zanzibar na hasa walioko Pemba, ni jambo la kujivunia kwa Serikali kupitia Wizara ya Habari, hasa sekta ya utalii maana mradi huo ni mwanzo kwa baraza la Afrika.

Miaka hii 53 ya Mapinduzi Zanzibar chumba hicho, kimeshatimiza miaka mitatu, kikiendelea kuwepo chini ya bahari.

Chumba hicho kilicho kwenye bahari, ni chamba cha kwanza duniani, lakini ni cha pili, baada ya kile kilichoko nchini Sweden lakini kikiwa kwenye ziwa la maji baridi.

Hapa sasa ndio unapoona umuhimu wa kuyalinda na kuyaenzi Mapinduzi ya Zanzibar ya mwaka 1964, ambayo leo hii kila kona na chochoro ya visiwa vya Unguja na Pemba, neema yake imeshafika.

“Leo ndugu wananchi tumeshajikomboa leo, na kila mmoja wetu nitahakikisha atakaa na kuishi kwa mazingira bora, na sasa hakuna tena kutawaliwa’’,alisema kwenye moja ya hutuba yake rais wa kwanza wa Zanzibar marehemu Abeid Amani Karume.

Sasa hapa, ndio unapoona umuhimu na faida ya Mapinduzi ya Zanzibar ya mwaka 1964, ambayo yaliwakombowa wazanzibar na viongozi kuitangaaza Zanzibar kiutalii, na leo hii tukiadhimisha miaka 53, Kisiwa cha Pemba chang’ara kwa kukua utalii.

Chumba hicho kwa njia moja ama nyengine, kimeanza kufungua ukurasa mpya wa utalii wenye hadhi na wa daraja la kwanza, hasa kwa vile chumba hicho ndio pekee kwa bara la Afrika.

Yote kwa yote, chumba hicho (under water room), kila anefika kwenye fukwe ya hoteli ya Manta resort Makangale, anashindwa kuamini mia juu ya mia, kwamba chumba hicho kinaweza kulaliwa na watu bila ya kupoteza uhai.

Meneja wa hoteli hiyo Matthew Saus kutoka Sweden, ambae anasema kuwa ujenzi wa chumba hicho umegharimu kiasi cha dola laki tano za Marekani.

‘Mimi na mwenzangu tulifika Pemba miaka kumi iliopita, na tukaanza harakati hizo za kujenga chumba cha chini ya bahari, na taasisi kadhaa zilitukubalia, na leo hii tukiwa kwenye sherehe za Mapinduzi ndio tumefikia hapa’’,alieleza.

Chumba hicho pamoja na kuonekana cha maajabu makubwa, lakini wakati ukiwa umelala au unajipatia chakula, basi hapo samaki wa aina zote, watakupita karibu sana na kutaka kuwagusa huku ukizuiwa na viambaza maalum vya chumba hicho mitihili ya kioo kigumu cha plastiki.

Kwa hili la chumba cha chini haliishia tu kama sherehe lakini Mapinduzi ya Zanzibara ya mwaka 1964, sasa yametinga duniani hasa kwenye sekta ya utalii, na kuziacha nchi zote za bala la Afrika nyuma.

Chumba hicho, ambacho ni cha kwanza duniani kuwepo kwenye maji ya bahari na ni cha pili baada ya kile kilichoko nchini Sweden, kwenye Ziwa la maji baridi, ni ishara kwamba Zanzibar imeshatanuka kiutalii wa daraja la kwanza ndani ya miaka hii 53.

‘’Leo tukiadhimisha miaka 53 ya Mapinduzi ya Zanzibar, ni nani engetarajia kuwa tungefika hapa kwenye sekta ya utalii, hii yote ni faida ya Mapinduzi yale yaliotukomboa chini ya Jemedari wa taifa hili marehemu Abeid Amani Karume’’, alisema Balozi wakati huo. 

Kwa hakika chumba hichi ambacho kinatumia umeme wa sola (jua), ili kuwapa mwangaza wa kutosha wapendwa watakao kua chini ya maji ya bahari, leo hii tunayo kila sababu ya kutembea kifua mbele, kwa kujivunia Mapinduzi ya Zanzibar ya mwaka 1964.

Wakati tukiadhimisha miaka 49 ya Mapinduzi ya Zanzibar, Balozi Seif Ali Iddi, alieonekana na furaha kubwa na alidakiza kuwa, muda mrefu Zanzibar ilikuwa ikiwakumbatia wawekezaji wasio na uwezo (uchwara), na ambao huekeza kwa muda mfupi na kisha kutimua (kurudi kwao).

‘’Zamani kabla ya kuwajua baadhi ya wawekezaji, tulikua kila anae kuja tunampa eneo, wengine wakisharejesha gharama zao tu hao…. wanarudi kwao na kutuachia majengo lakini kwa hasa nasema heko’’, alifafanua Makamu huyo wa pili.

Wakati leo hii tukiadhimisha miaka 53 ya Mapinduzi ya Zanzibar, Sekta ya utalii inafungua ukurasa mpya wa utalii Kisiwani Pemba na Zanzibar kwa ujumla, na hasa kwa vile mradi huo ni mwanzo ndani ya bara la Afrika.

‘’Hichi chumba, nasema kimeanza kufungua milango kwa watalii wakubwa na wa juu na matajiri wakubwa duniania, maana sasa akina Bilget wakija watapata sehemu ya kiutalii kwa mujibu wa hadhi na fedha zao’’,alieleza Mkuu wa Kamisheni ya utalii Pemba Suleiman Amour.

Japo kuwa gharama ya kukaa kwa usiku mmoja, kwa mujibu wa Meneja wa wa hoteli ni shilingi milion tatu laki mbili na sabiini (3,270,000), lakini kama sio gharama kubwa, naamini watalii wengi ambao wangetarajiwa kwenda ingekuwa ni hawa wa watalii wa ndani.

Chumba hicho, ambacho kwa juu ni mithili ya boya ambalo linaumbile la mlango wa nyumba ya kawaida unaweza kuingia humo kwa aina ya kushuka ngazi hadi chini, ambapo kumetajawa kuwa unapokua humo samaki unawaona kwa karibu.

Chumba hicho kilicholetwa hapo kutoka nje ya nchi kuta moja baada ya nyengine, unapokuwa ndani yake unauwezo wa kuona umbali wa mita100, huku samaki na bustani ya bahari ikiwa ndio bustani yako.

Kwa vile muwekezaji huyo, ana nia ya kuongeza idadi ya vyumba vya aina hiyo katika eneo hilo, iwapo hicho cha mwanzo ambacho ni cha majaribio kitafanikiwa vizuri.

Sasa tukiwa tunaadhimisha miaka 53 ya Mapinduzi ya mwaka 1964, kazi sasa ipo kwa Wizara ya Habari, kuzidi kukitangaaza Kisiwa cha Pemba na Zanzibar kwa ujumla, juu ya utalii kwa wote wa daraja la kwanza.

Lengo la Mapinduzi pia ilikuwa ni kukuza pato la wananchi, hasa baada ya kujitawala na  sasa kwa vile watalii wameshatukubali nasema hapa ndio pakuanzia kwani mjenga nchi ni mwananchi.

Mkuu wa Mkoa wa Kaskazini Pemba Omar Khamis, hakukosa la kusema  juu ya chumba hicho, kutokana na kujaa na furaha yeye akawasisitiza wananchi kuendelea kutoa ushirikiano na mwekezaji huyo.

Asha Ali Omar wa Makangale, anasema uwepo wa chumba hicho, sasa kunadhihirisha kufikiwa kwa malengo ya kweli ya Mapinduzi ya Zanzibar ya mwaka 1964.

“Leo tukiadhimisha miaka 53 ya Mapinduzi Zanzibar, mimi binafsi nnafuraha maana, utalii umetanua mbawa, na yale malengo ya jemedari wetu yamefikiwa’’,alifafanua.

Muhidini Makame Haji wa Mchanga mdogo, anasema hakuna mwananchi wala kiongozi wa Zanzibar, ambae hajanufaika na Mapinduzi ya Zanzibar ya mwaka 1964.

“Kila mmoja leo akisherehekea miaka 53 ya Mapinduzi Zanzibar, hakuna ambae hajala keki ya taifa, iwe kwenye utalii, afya, elimu au miundombinu ya barabara’’,alifafanua

Aliishauria serikali kila atakaeyabeza Mapinduzi ya Zanzibar kwa njia moja ama nyengine, ni vyema akashughulikiwa maana, atakuwa hapendi maendeleo.


Kwa hapa sasa ni dhahiri kuwa, Mapinduzi ya Zanzibar ya mwaka 1964, na leo hii tukiwa katika shamra shamra za maadhimisho ya miaka 53, ni ukweli kwamba Utalii wa hadhi ya juu umeshaweka nanga Kisiwani Pemba.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.