Habari za Punde

Nafasi za masomo nchini Mauritius ngazi ya shahada ya kwanza

WIZARA YA ELIMU NA MAFUNZO YA AMALI INATANGAZA NAFASI ZA MASOMO ZILIZOTOLEWA NA SERIKALI YA MAURITIUS, NGAZI YA SHAHADA YA KWANZA KWA MWAKA WA MASOMO 2017-18

1          Sifa za muombaji

Asiyezidi miaka 25
Awe amemaliza kidato cha sita na amefaulu daraja la kwanza au la pili au amehitimu ngazi ya Diploma.

2 Utaratibu wa malipo

Waombaji watakao bahatika kupata nafasi hizo watapatiwa malipo yafuatayo;

i.                Posho la kila mwezi Rs 8,300 kwa USD 266
ii.            Ada ya masomo Rs 100,000 kwa USD 3205 kwa             mwaka
iii.           Tiketi kwa kipindi chote cha masomo hadi kumaliza.


3          Njia za kufanya maombi Waombaji wote wanatakiwa waombe barua ya kujiunga na chuo (Admission Letter) kupitia mitandao ya vyuo vya Mauritius kama vifuatavyo;

CHUO ANUANI

University of Mauritius www.uom.ac.mu
University of Technology, Mauritius www.utm.ac.mu
Universities des Mascareignes www.udm.ac.mu
Fashion & Design Institute www.fdi.ac.mu
Mauritius Institute of Education www.mie.ac.mu
Mahatma Gandhi Institute www.mgirti.ac.mu
Rabindranath Tagore Institute www.mgirti.ac.mu

Fomu ya maombi na maelekezo yake inapatikana katika mtandao ufuatao; http://ministry-education.govmu.org/English/Scholarships/ Pages/default.aspx

4.         Utaratibu wa kuwasilisha maombi Waombaji wa nafasi hizo watatakiwa kuwasilisha viambatisho vifuatavyo katika maombi yao;

1 Cheti cha kuzaliwa
2 Vivuli vya Vyeti vya kumalizia masomo vya “O” na “A” Level
3 Fomu ya Afya (Medical Report)
4 Kivuli cha pasi ya kusafiria
5 Nyaraka zote zinahusiana na masomo anayotaka kusomea


Kwa maelezo zaidi Kuhusiana na nafasi hizo fika; Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali – Kitengo cha Uratibu wa Elimu ya Juu chumba No.57.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.