Habari za Punde

Serikali kuendelea kulinda haki zote za wafanyakazi


 
STATE HOUSE ZANZIBAR
OFFICE OF THE PRESS SECRETARY
PRESS RELEASE
  Zanzibar                                                                 1.05.2017
---
SERIKALI ya Mapinduzi ya Zanzibar itaendelea na utaratibu wake wa kuzilinda haki zote za wafanyakazi  na kuimarisha maslahi yao hatua kwa hatua ili waweze kumudu hali ya maisha pamoja na kuongeza ufanisi katika uzalishaji na utoaji wa huduma kwenye sektka mbali mbali.

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein amesema kuwa aliyasema hayo leo huko katika viwanja vya Mpira Mahonda, Mkoa wa Kaskazini Unguja katika kilele cha maadhimisho ya Siku ya Wafanyakazi Duniani, Mei Mosi ambayo kilele chake hufanyika kila tarehe 01. Mei ya kila mwaka duniani kote.

Katika hotuba yake aliyoitoa katika kilele cha maadhimisho hayo, Dk. Shein alisema kuwa kutokana na kujali kazi na kuufahamu umuhimu wa wafanyakazi pamoja na kuufahamu wajibu wake akiwa Rais wa Zanzibar amechukua hatua ya kupandisha mishahara na posho mbali mbali kadri hali ya uchumi na ukuaji wa mapato inavyoruhusu.

Sherehe hizo ambazo viongozi mbali mbali wa vyama vya siasa, Sekta binafsi na Serikali walihudhuria akiwemo Makamo wa Pili wa Rais wa Zanzibar, Balozi Seif Ali Idd, Dk. Shein aliongeza kuwa katika nyakati mbali mbali za uongozi wake katika kipindi cha kwanza cha uongozi wake alipandisha mishahara mara tatu, mwaka 2011, 2013 na mwaka 2015.

Aidha, alisema kuwa wakati wa Kampeni za Uchaguzi wa mwaka 2015, aliahidi tena kuwea Serikali atakayoiongoza katika kipindi cha pili mwaka 2015 na 2020 itaongeza kima cha chini cha mshahara kwa sekta ya Umma kwa aslimia 100 kutoka TZS. 150,000 hadi  TZS 300,000.

Kwa maelezo yake aliahidi kuwa mabadiliko hayo ya mshahara yataanza mwishoni mwa mwezi wa April, 2017 na kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa kumuwezesha pamoja na Serikali yake kwa kutekeleza ahadi hiyo ambapo kuanzia mwezi uliopita wafanyakazi wote wa Sekta ya Umma wameanza kufaidika na nyongeza hiyo ya mishahara.

Aliongeza kuwa ongezeko hilo limetekelezwa kwa wafanyakazi na maafisa wa ngazi mbali mbali kwa viwango tofauti vilivyowekwa na Taasisi zinazohusika kulingana na kwiango cha mshahara anachokipata mfanyakazi.

Sambamba na hayo, Dk. Shein pia, aliahidi kuwa Serikali itazishughulikia  changamoto chache kama zitakuwepo   kwa baadhi ya wafanyakazi zilizojitokeza kulingana na utaratibu uliowekwa na kuwahakikishia wafanyakazi kuwa zitapatiwa ufumbuzi wa haraka.

Pia, Dk. Shein aligusia kupunguzwa kwa kwiango cha kodi ya mapato katika mishahara kutoka asilimia 13 hadi 9 kuanzia mwaka wa fedha 2016/2017, hatua hizo zote zimechukuliwa kwa lengo la kuimarisha ustawi wa wafanyakazi na kuongeza ufanisi katika kazi.

Aisha, Dk. Shein alieleza kuwa kwa wafanyakazi wanaowadharau wananchi wanapokweknda kupata huduma, wanaowapuza, wanaowanyanayasa na wanaodai chochote ili wasaidie kutoa huduma katika kipindi hiki Serikali itaongeza kasi na itaanza kuwachukulia hatua Wakurugenzi wao, Maafisa Wadhamini wao na Makatibu Wakuu wao.

Na wale wote wenye tatbia ya kutoroka kazini, kuchelewa kazini, wasiojali Kanuni zilizopo za Utumishi wa Umma, wababaishaji na wanaojifanya hawajali na wababe, Serikali haitowavumilia tena na watawajibishwa wao na kama hapana budi pamoja na viongozi wao wote wataondoshwa kazini.

Alisisitiza kuwa uwezo wa kuongeza mishahara unatokana na ongezeko la mapato na ukuaji wa uchumi, mambo ambayo ni matokeo ya juhudi katika utendaji kwani mshahara ni ujira wa kazi na mapato yanatoongezeka kwa juhudi katika kazini.

Akizingumzia suala la mishahara hewa kutokana na ripoti aliyopelekewa hivi aribuni, Dk. Shein alisema kuwa hapana atakae samehewa kwa atakebanika kufanya kosa na hapana atakaeonewa au kudhulumiwa ambaye hajafanya kosa.

Pia, Dk. Shein alitoa wito kwa wafanyabiashara na watoaji huduma ambali mbali, kuacha mtindo wa kuongeza bei za bidhaa na huduma bila ya sababu za msingi kwani matokeo yake na wao wanaweza kuathirika na wasije wakawalaumu wananchi na Serikali yao.

Kwa upande wa wafanyakazi katika sekta binabsi, Dk. Shein aliwajuulisha kuwa taratibu za kisheria zinaendelea ili kutangaza na kulipwa kwa kima kipya cha mishahara katika sekta hiyo.

Bila ya kwuasahau wafanyakazi wa majumbani, Dk. Shein alitoa nasaha zake kwa waajiri wa wafanayakzi hao kujenga utamaduni wa kuwathamini, kuwatambua rasmi, kuwapatia stahikli zao, kuwawekea mazingira ya kazi yanayostahiki na wao wapate fursa ya kujadiliana na waajiri wao kama zilivyo kada nyengine.

Nae Waziri wa Kazi, Uwezeshaji, Wazee, Vijana, Wanawake na Watoto Maudline Cyrus Castico alieleza juhudi zinazoendelea katika kulitafutia ufumbuzi suala la kima kipya cha mishahara kwa sekta binafsi huku akitumia fursa hiyo kupongeza Rais Dk. Shein kwa juhudi zake za kuwaenzi wafanyakazi.

Mapema  Mwakilishi wa Shirika la Kazi Duniani (ILO), Albert Okelo akitoa salamu za Mkurugenzi Mkuu wa Shirika hilo Tanzania,  alitoa pongezi kwa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kwa kuwajali wafanyakazi na kuwasamini pamoja na juhudi za Serikali za kuanzisha Pensheni Jamii kwa wazee.

Katibu Mkuu Vyama Huru vya Wafanyakazi Zanzibar, Khamis Mwinyi Mohammed alitoa pongezi kwa Dk. Shein kwa kutekeleza ahadi yake ya kupandisha mishahara kwa kima cha chini sambamba na kupongeza Serikali chini ya uongozi wake kwa kudumisha amani na utulivu na kueleza baadhi ya mafanikio yaliopatikana katika uongozi wa Dk. Shein.

Mapema Dk. Shein alipokea maandamano ya wafanyakazi wa Sekta ya Umma pamoja na Sekta binafsi na kabla ya hotuba yake alitoa zawadi kwa wafanyakazi bora 16 kwa niaba ya wenzao 100 kutoka sekta ya Umma.

Rajab Mkasaba, Ikulu Zanzibar

Postal Address: 2422 Tel.:0777427449. Fax: 024 2231822 
 E-mail: rajabmkasaba@yahoo.co.uk

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.