Mkurugenzi wa Pennyroyal(Gibraltar) Zanzibar Ltd na Zanzibar Amber Resort Bw. Saleh Mohammed Said akizungumza na waandishi wa habari kuhusu ujio wa ugeni muhimu wa aliyekuwa waziri wa Fedha na Naibu Waziri Mkuu Mauritius Dkt. Ramakrishna Sithanen anaetarajiwa kuwasilin tarehe 06 Juni
Jumanne
tarehe 6 Juni, aliyekuwa waziri wa Fedha na Naibu Waziri Mkuu Mauritius Dkt.
Ramakrishna Sithanen anategemewa kuwasili Zanzibar kwa mualiko wa Mkurugenzi wa Pennyroyal
(Gibraltar) Zanzibar Ltd na Zanzibar Amber Resort Bw. Saleh Said.
Dkt.
Ramakrishna Sithanen anatarajia kukutana na wajumbe 40 wa Zanzibar Association
of Tourism (ZATI),
Zanzibar National Chamber of Commerce, Industry and Agriculture (ZNCCIA),
Zanzibar Association of Tour Operators (ZATO) katika hoteli ya Serena tarehe 7 Juni, na
watazungumza maswala mbalimbali ikiwemo jinsi ya kubadilisha na kuboresha utalii
Zanzibar. Pia atakutana na viongozi wa serekali ya Zanzibar. Ajenda
kuu ya Mkutano huo ni “Kuondoa Umasikini Zanzibar Kupitia Uwekezaji wa Kigeni.”
Pennyroyal
Gibraltar Ltd ilichukua uamuzi wa kumwalika Zanzibar Dkt. Ramakrishna Sithanen,
kwa sababu ya ujuzi na weledi wake kwa kuwa kiungo kikuu cha mabadiliko ya
Mauritius. Ni mategemeo ya Saleh kwamba, Zanzibar itafuata nyao za Mauritius
katika kupunguza umasikini na kukuza uchumi kupitia Utalii.
"Naamini
tukifanya kazi pamoja na Dkt. Sithanen na kupata ujuzi wake, kampuni yetu na
Zanzibar kwa ujumla tutafanikisha kulete mabadiliko ya kimaendeleo kwa sababu
ana uzoefu mkubwa, na amewezesha Mauritius kupata mafanikio. Ninayo furaha
kwamba amekubali kuja kutuelimisha na kutupa ujuzi wake, na wadau wa utalii na
maendeleo wanasubiri kwa hamu kupata kusikia kutoka kwa mtaalamu huyu
aliyebobea katika maswala ya uwekezaji na Utalii." Alisema Mkurugenzi wa
Pennyroyal Gibraltar Zanzibar Ltd Saleh Said.
Dkt. Ramakrishna
Sithanen ana uzoefu wa miaka 37 katika sekta binafsi kama mwana uchumi na
ameshawahi kushikilia nafasi za juu kama Mkurugenzi kwenye Shirika la Ndege
Mauritius, Mkurugenzi wa Mikakati kwenye Benk ya maendeleo ya Africa (African
Development Bank) na alikua Mshauri wa Kimataifa katika Afrika na nchi za
Bahari ya Hindi.
Mwaka 1991 alipata
nafasi ya kua Waziri wa Fedha Mauritius mpaka 1995, kipindi hicho alifanikiwa
kubadilisha sera za kiuchumi nchini Mauritius na kupanua uchumi wa nchi.
Alichaguliwa kama Naibu Waziri Mkuu mwaka 2005 na kuleta mabadikilo yakijasiri
katika mataasisi mbalimbali nakufanikiwa kukuza uchumi nchini humo.
Zaidi ya hapo mwaka 2009 alipata heshima ya juu kutoka kwa Raisi wa
Mauritius inayo julikana kama Grand Commander of the Order of the Star and Key.
Dkt. Sithanen anasifika kwa kazi nzuri aliyofanya na mafanikiyo ya kukuza
uchumi wa Mauritius, kwa sasa ni Mwenyekiti na Mtokea 2013kurungezi wa
International Financial Services, ambayo ni moja wapo ya makampuni makubwa
yanayo simamia fedha Mauritius. Vilevile ni Mwenyekiti wa Bodi ya maendeleo ya
Rwanda na alikuwa Mshauri wa Serikali ya Rwanda kwa mambo ya kodi, ushindani na
Fedha baina ya mwaka 2013 na 2015.
"Ni
mategemeo yetu kuwa, safari hii ya Dkt.
Ramakrishna Sithanen hapa italeta mafanikio makubwa sana kiuchumi hasa hasa
kenye sekta ya utalii Zanzibar, na sisi tutapata kujua vigezo vilivyo wezesha
Mauritius kufanikiwa. Dkt. Sithanen anauelewa mzuri wa changamoto zinazo kabili
uchumi wa Afrika na visiwa vidogo kama Zanzibar, ni matumaini yangu kwamba
serikali ya Zanzibar itapata muamko wa mabadiliko" Alisema Saleh Said
No comments:
Post a Comment