“Drones” kutanda anga
Nikwa
ajili ya Matangazo Mubashara kutoka PBA
Kuanza
rasmi Alhamis 27 Julai saa 4:00 asubuhi kwa mkutano na wa wanahabari
Kati ni Yussuf Hamad mwenyekiti wa kampuni ya Rafiki Network akizungumza na manahodha wa Ngalawa pamoja na waendesha baiskeli watakaoshiriki katika tamasha la Kimichezo kisiwani Pemba “Pemba Weekend Bonanza” Kulia ni Salim Jabu Dawa Mratibu wa Matukio Kisiwani Pemba na Kushoto ni Umrat Khator Khamis ambae ni Afisa Masoko wa Kampuni ya Rafiki.
Ali
Othman Ali
Timu ya AZAM TV imewasili rasmi kisiwani Pemba kwa
ajili ya kurusha “live” Tamasha la Kimichezo Kisiwani Pemba lilioandaliwa na
Kampuni ya Rafiki Network.
Akizungumza kwa njia ya simu mara baada ya kuwasili Azam
Sea Link 2 bandari ya mkoani Raisi wa Kampuni Ya Rafiki Network Bw. Hamad Omar
Hamad amesema amefarijika kusikia AZAM wamewasili na vifaa vyakisasa zikiwemo
drones ambazo zita paa angani kuhakikisha kwamba matukio yote yanaonekana ndani
na nje ya nchi.
Nae Mwenyekiti wa Kampuni ya rafiki Network Bw.
Yussuf Shoka Hamad amewataka manahodha na waendesha baiskeli ambao watashiriki
katika Bonanza kujali sheria za michezo hiyo wakiamini kwamba Kampuni ya Rafiki
Network nia yake ni kuibua vipaji vyao na kuviendeleza kwa maslahi yao na Taifa
kwa ujumla.
“Tumeanzisha Tamasha hili la Pemba Weekend Bonanza
ili kuibua vipaji vitakavyotuwakilisha katika medani za kitaifa na kimataifa
Hivyo tunawaomba kujali sheria na kanuni za michezo mukijua kwamba mashindano
yote yanaoneshwa mubashara na Kituo cha TV cha AZAM” amesema bwana Hamad.
Tamasha la Pemba Weekend Bonanza Litaanza rasmi siku
ya Ijumaa 28 Jula 2017 saa nane jioni Kwa mchezo wa Ng’ombe utakaofanyika Skuli
ya Chwale ambapo siku ya Jumamosi tarehe 29 Julai itakua ni mashindano ya
baiskeli hatuo ya mchujo.
Bonanza litaendelea Siku ya kilele kwa shangwe na
shamra shamra za ngoma mbalimbali huko katika fukwe za vumawimbi ambako
mashindano ya kuogelea pamoja na mchuano mkale wa kihistoria wa resi za ngalawa
utafanyika
No comments:
Post a Comment