Habari za Punde

Madaktari wa China wawafanyia vipimo wanafunzi Pemba




NA HAJI NASSOR, PEMBA

TIMU mpya wa madaktari nane (8) kutoka China waliopo hospitali ya Mkoa ya Abdalla Mzee Mkoani Pemba, imesema mpango wa kuwafuata wanafunzi wadogo na kuwafanyia vipimo vya kiafya, utakuwa endelevu kila baada ya muda.

Kauli hiyo imetolewa na kiongozi mkuu wa madaktari hao Chen Er Dong, alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi hospitali hapo, mara baada ya kuamalizika kwa zoezi la vipimo walilolifanya kwa wanafunzi wa skuli ya msingi ya Makombeni wilaya ya Mkoani hivi karibuni.

Alisema timu hiyo ya madaktari inataka kuwa na kitu cha aina yake cha kuwafuata wanafunzi popote waliopo kisiwani Pemba, ili kuwafanyia vipimo vya masikio, pua na koo ‘ENT’ na kuwapa elimu ya kujikunga na magonjwa yatokanayo na viungo hivyo na kishaa kuwapa dawa.

Dk Chen alisema, kwa kuanzia wameanza na skuli hiyo ya Makombeni, ingawa kila baada ya muda wanatarajia kuwafikia wanafunzi wa skuli nyengine, ili kuwapa elimu na kisha kuwafanyia vipimo.

“Wanafunzi wanaonekana wananyemewa na michubuko au athari ya masikio, pua na koo maana wanaruhusu viungo hivyo kuingia vumbi’’,alisema.

Hata hivyo alisema kwenye zoezi hilo walilolifanya na madaktari wenzake, hawagundua mwanafunzi alieathirika sana ingawa wanaonekana kunyemelewa.

Katika hatua nyengine kiongozi huyo wa madaktari kutoka China, amewataka wazazi na walezi kujenga utamaduni wa kuwafikisha hospitali watoto wao, ili kufanyiwa uchuguzi hata kama hawajaanza kuugua.

Kwa upande wake msaidizi madaktari hao kutoka China dk He, alisema wananchi wa kisiwa cha Pemba, wasisite kuitumia hospitali Mkoa iliopo Mkoani, ambayo kwa sasa ina dawa na vifaa mbali mbali vya kisasa.

“Hopsitali ya Mkoani baada ya serikali ya watu wa China kwa kushirikiana na Serikali ya Zanzibar, wa meshaiimarisha kila hali, sasa ni wajibu wa wananchi kuitumia’’,alishauri dk He.

Mwalimu mkuu wa skuli hiyo ya Msingi ya Makombeni Othman Machano Mmanga, alisema ujio wa madaktari hao kwenye skuli hiyo, kumeibua mambo kadhaa ya kiafya hasa baada ya kuwapa elimu.

“Mimi napendekeza kama ingekuwa inawezekana kila mwaka waje mara tatu, maana ni jambo jema lenye kuhusiana na afya za wanafunzi ambao hawana utamaduni wa kuchunguuza afya zao’’,alifafanua.

Hata hivyo mwalimu Mkuu huyo, amewaomba madaktari hao kwenda na skuli nyengine kwa ajili ya zoezi la kuchunguuza afya za wanafunzi, hasa kwa vile jamii haina utamaduni wa kuchunguuza afya zao kama wakijihisi ni wazima.


Timu hiyo ya madaktari wapya kutoka China, waliwasili mwezi mmoja uliopita kisiwani Pemba, baada ya wenzao waliokuwepo kumaliza muda wao, kwenye hospitali hiyo ya ya mkoa ya Abdalla Mzee Mkoani Pemba. 

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.