Habari za Punde

Kituo cha Huduma za Sheria Kisiwani Pemba Chatoa Elimu ya Sheria Kwa Jamii .

WASANII kutoka Kampuni ya Jufe Production wakioongozwa na Mwinyi mpeku, wakionyesha igizo la namna ya watu wanavyoyamaliza kesi za ubakaji nje ya vyombo vya sheria, kabla ya kuanza kwa mkutano wa wazi wa kuelezwa wananchi umuhimu wa kushiriki na kushirikishwa wakati wa utungaji wa katiba na sheria, mkutano huo ulifanyika shehia ya Tumbe Mashariki, wilaya ya Micheweni Pemba
MRATIBU wa Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar ZLSC tawi la Pemba, Fatma Khamis Hemed, akijibu maswali ya wananchi wa shehia ya Tumbe mashariki wilaya ya Micheweni, kweye mkutano wa wazi wa kuelezewa umuhimu wa wananchi kushiriki na kushirikishwa, wakati wa utungaji wa Katiba na sheria
NAIBU sheha wa shehia ya Tumbe Mashariki wilaya ya Micheweni, Seif Omar Hamad, akimtambulisha Msaidizi wa sheria Jimbo la Tumbe kwa wananchi wa shehia hiyo, waliohudhurai mkutano wa wazi wa kuelezwa umuhimu wa ushirikishwaji na ushiriki, wakati wa utungaji wa sheria na katiba, mkutano huo ulitayarishwa na Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar ZLSC tawi la Pemba


WASANII kutoka Kampuni ya Jufe Film Producation ya mjini Wete, wakipamba jukwaa kwa kucheza musiki wa kizazi kipya, kabla ya kuanza kwa mkutano wa wazi wa kuelezwa umuhimu wa ushirikishwaji na ushiriki wakati wa utungaji wa sheria na katiba, kwa wananchi wa shehia ya Tumbe Mashariki wilaya ya Micheweni Pemba, mkutano huo ulitayarishwa na Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar ZLSC tawi la Pemba

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.