NA/ SALAMA NASSOR--- PEMBA.
OFISA Mdhamini Wizara ya nchi ofisi ya Rais,katiba,Sheria
utumishi wa Umma na Utawala bora Pemba, Masoud Ali Mohamed, amewataka wadau wa
Sheria nchini kuusimamia mswaada wa sheria juu ya utowaji wa huduma za sheria
ili iweze kuwafikia jamii.
Kauli
hiyo ameitowa wakati alipokuwa akifunguwa mafunzo ya siku moja yaliofanyika
katika ukumbi wa Nyaraka Chake Chake , ambapo alisema jamii haina uwelewa mkubwa juu ya
mswada huo hivyo aliwaomba wadau hao kushirikiana kwa pamoja kwa kutowa elimu
ili iweze kufikia malengo yalio kusudiwa.
Alieleza
taaluma hiyo iweniendelevu kwa ajili kuendeleza Taifa na sio vyema kuiwacha
njiani wakati wapo wengi wanaihitaji.
“Jamii
wakipatiwa elimu juu mswada huo ulionzishwa basi kutaondokana na malalamiko
pamoja na kukosa huduma zao wakati wanapokabiliwa na matatizo na wanakuwa
wanakosa uwezo wa kujikwamuwa kutokana na hali zao kuwa ni duni”,alisema.
Akitowa
maada katika mafunzo hayo, Saleh Said Mubaraka, alisema lengo la mafunzo hayo
ni kuwasaidia watu ambao hawana uwezo wa kulipia huduma za sheria hivyo
Serikali imeamuwa kuwanzisha wadau wa sheria ili waweze kufanya kazi.
Aliwataka
wadau kuusoma vizuri ili kutowa maelekezo katika mswaada huo kabla ya
haujapitishwa na baraza la Wawakilishi ili wananchi uwafikie wakati muwafaka.
Alifafanuwa
kwa kusema mswaada huo ni kuhakikisha kila mwananchi anapata haki zake za
msingi kwa mujibu wa sheria.
“Ikiwa
mswaada huu utapita wananchi watafaidika hususani kwa wale walengwa
waliokusudiwa ambao wasiojiweza na kutaondokana na malalamiko yaliokuwa
yanajitokeza wakati wanapotaka kupatiwa haki zao”,alisema.
Ofisa
huyo, aliwataka wanasheria kuwa makini katika kazi zao na wasiwe wanaangalia
upande mmoja kwani wao wanajukumu kubwa katika nchi kinyume na hivyo
kutapelekea malalamiko yasiokuwa ya lazima.
Kwa upande
wao washiriki katika mafunzo hayo, Ofisa Mipango kutoka kituo cha huduma za sheria, Safia
Saleh Sultan, alisema ameyapokea vyema mafunzo hayo kwani kwani Serikali
imefanya juhudi kubwa kwani haujabaguwa mtu.
Aliitaka
Wizara hiyo kutowa elimu kwenye vyombo vya habari kwani wakifanya hivyo
watafaidika wananchi walio wengi hususani wa vijijini.
Naye
Ofisa upelelezi Dawati la kijinsi na watoto, Hamad Faki Ali, alisema mswaada
huo utapelekea kuleta maendeleo kwa jamii na pia watapata kutetea haki zao.
Alisema
jamii haina elimu ya haki na kujuwa sheria na hupelekea kupata Changamoto
nyingi, lakini mswaada huo ukipita watajuwa haki zao kwani umechanganya mambo
mengi na haukuweka ubaguzi.
Hivyo
aliomba kuweko mashirikiano ya pamoja kwa wadau wote , ili kuhakikisha muswada
huo unaeleweka kwa Wananchi wote.
No comments:
Post a Comment