MKUU wa wilaya ya Mkoani Hemed
Suleiman Abdulla, amewataka viongozi mbali mbali, kuwaacha wanasheria
kutekeleza wajibu wao, badala ya kuwaingilia kwenye majukumu yao, kwani kufanya
hivyo ni kudhoofisha utendaji wao wa kazi.
Alisema
wanasheria wamekuwa wakitekeleza wajibu wao kama walivyo watendaji wengine,
amboa hawapendi kuingiliwa utendaji wao, hivyo ni vyema na wao wakaachiwa
kufanya majukumu yao waliopangiwa kwa mujibu wa sheria.
Mkuu huyo wa
wilaya, ametoa tamko hilo, Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar ZLSC tawi la
Pemba, alipokuwa akifungua mafunzo ya siku mbili, juu ya haki za binadamu kwa
makadhi, marakani na wazee wa mahakama na kusema wanasheria wanafanya kazi zao
vyema.
Alisema wamekuwa
wakitoa msaada mkubwa wa kisheria kwa wananchi, kabla ya kutaka kufungua
mashauri yao mahakamani, hivyo iwapo watakuwa wanaingiliwa kwenye kazi zao,
hawawezi kufikia malengo yao.
Alisema kama
viongozi watatumia vibaya nafasi zao, na sasa kuamua kuwaingilia wanasheria
wakati wanapotekeleza majukumu yao, ufanisi wa kazi kwao hauotokuwepo.
“Hivi tunayo
oifisi ya Mkurugenzi wa Mashitaka, Kituo cha Huduma za sheria na hata vyombo
kama mahakama na Polisi, wamekuwa wakiwasaidia wananchi kisheria, lakini kama
tukiwaingili sisi viongozi ufanisi hautokuwepo”,alifafanua.
Katika hatua
nyengine Mkuu huyo wa wilaya ya Mkoani, amewataka wazee wa mahakama, makadhi na
makarani kisiwani Pemba, kuendelea kufanya wajibu wao kwa kufuata sheria na
kaununi zilivyo, hata kama kufanya hivyo, hakutowaridhisha watu wengine.
Mapema
Mratibu wa Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar Fatma Khamis Hemed, amesema
makadhi, makarani na wazee wa ,mahakama ni nguzo muhimu kwenye kuendesha kesi
mbali mbali.
Hivyo
alieleza ndio maana, Kituo kimeamua kuwapa mafunzo ya haki za binadamu kwa vile
haki hizo ni wajibu wa kila mmoja kuzitunza za mwenzake ili na za kwake
zitunzwe.
Akiwasilisha
mada uwajibikaki na utendaji wa haki Mwanasheria Dhamana wa Afisi ya Mkurugenzi
wa Mashitaka Pemba, Ali Rajab Ali alisema kwenye kutekeleza majukumu ya umma,
hakupaswi kwa mktoa uamuzi kuegemea upande mmoja.
“Nguzo za
kutekeleza wajibu na haki, unaonekena kwenye maeneo matano, ikiwa ni pamoja na kuwepo
kwa majukumu, kufuatwa kwa mujibu wa sheria na kutoa huduma kwa kiwango
kinachotakiwa”,alifafanua.
Wakichangia
mada kadhaa washiriki wa mafunzo wameziomba mamlaka husika, kuhakikisha kwa
wazee wa mahakama kuwa ofisi maalum ya kukaa kabla ya kuanza kwa uendeshaji wa
kesi badala ya utaratibu wa sasa wa kuchanganyika na wanaosubiri huduma.
Mzee wa
mahakama Chakechake Abdalla Nassor Mauli, alisema haipendezi kuona wanapofika
mahakamani kuchanganyika na mashahidi, watuhumiwa na watu wengine wanaotaka
huduma Makamani.
Aidha Kadhi
ya mahakama ya rufaa Daud Khamis Juma, alisema elimu ya utendaji kazi, inapaswa
kuwepo kila baada ya muda, maana ukumbushaji hauna muda malum.
Akighairisha
mafunzo hayo, Afisa Mipango wa Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar ZLSC tawi la
Pemba, Khalfan Amour Mohamed, alisema makadhi na makarani wanayonafasi kubwa ya
kupatikana kwa haki mahakamani.
Katika
mafunzo ya siku mbili mada kadhaa zilijadiliwa, ikiwa ni pamoja na changamoto
na mtizamo wa jamii kwa mahakama za kadhi na wazee wa mabaraza, haki za
binadamu, maadili ya makadhi na wazee wa mahakama pamoja na huduma kwa wateja.
No comments:
Post a Comment