Habari za Punde

Islanders hawashikiki uwanja wa Gombani



NA HAJI NASSOR, PEMBA

WENYEJI wa uwanja wa Gombani timu ya Younger Islanders inayokipiga ligi ya Zanzibar kanda ya Pemba, jana ilidhihirisha kuwa wanapokuwa ndani ya nyasi bandia, hutembeza kipigo, baada ya jana tena kuichapa Chuo basra kwa mabao 3-0.

Katika mchezo wa awali waliocheza kwenye uwanja huo,Oktoba 19, iliiyeyusha Shaba kwa bao 1-0, ingawa walipotoka nje ya dimba hilo Okotba 13, walipachikwa bao 1-0 na FSC.

Kwa jana ndani ya dimba hilo la Gombani, walianza mchezo vyema, huku wapenzi na washabiki wao wakianza kunadia bao, kunako dakika ya 23, baada ya mpira ulioamba ambaa kwenye kibendera cha kona, na kumfikia Ali Khamis, aliefunga bao.

Chuo basra wajikaza sana baada ya kuingia kwa bao hilo, na kujaribu mashuti ya mbali, kila walipokuwa wakipata nafasi, lakini yote yalikuwa chakula mbele ya mlinda mlango wa wenyeji wao.

Dakika tano kabla ya mapunziko (40), Abubakar Habibu aliipatia Islnders bao la pili, baada ya uzembe wa mwaka, uliofanywa na walinzi wa Basra, na kisha mfungaji kuutumia mwanya huo, na kwenda mapunziko wakiwa mbele kwa mabo 2-0.

Kipindi cha lala salama, Basra walianza kwa mwendo kasi, huku wakifanya mabadiliko ya wachezaji, ili wajinasue na kipigo hicho, lakini walijikuta wakikatishwa tamaa na Mohamed Khamis kunako dakika ya 80, kwa kuwapachika bao la tatu.

Katika uwanja wa FFU Finya, timu isiotabirika ya Okapi iliotokea kwenye nane bora msimu uliopita, waliwakaanga Hard Rock kwa mzinga 1-0.

Kwa matokeo hayo sasa, Islanders, Mwenge na FSC ndizo timu zinazokabana koo, kwenye kiti cha uongozi wa ligi kuu ya Zanzibar kituo cha Pemba, kwa point sita kila timu, huku timu za Okapi na News star zikiwa na point nne nne, ingawa hadi sasa timu ambayo haijavuna pointi, ni Wawi star ambayo ishashuka dimbani mara mbili.


Leo kutakuwa na mchezo mmoja tu wa ligi kuu ya Zanzibar kituo cha Pemba, kwa Shaba yenye polint tatu, itaumana na New star yenyewe ikiwa na point nne, ambapo kesho ni zamu ya Opec yenye point moja, watakaovutana na Kizimbani yenye point tatu,  kwenye uwanja wa FFU Finya.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.