Habari za Punde

Tosamaganga Alumini Association Watoa Msaada wa Vifaa Tiba vya Zaidi ya Shs. Milioni Moja Laki Sita Katika Hospitali ya TOSAMAGANGA

Baadhi ya wanafunzi waliowahi kusoma shule ya sekondari ya Tosamaganga iliyopo wilaya ya Iringa mkoani Iringa maarufu kwa jina la Tosamaganga Alumni Association wakiwa wanajadili kitu walipokuwa kwenye ziara ya kuitembelea shule waliyosoma
 Baadhi ya wanafunzi waliowahi kusoma shule ya sekondari ya Tosamaganga iliyopo wilaya ya Iringa mkoani Iringa maarufu kwa jina la Tosamaganga Alumni Association wakiwatembelea wagonjwa katika hospitali ya Tosamaganga mkoani Iringa
Baadhi ya wanafunzi waliowahi kusoma shule ya sekondari ya Tosamaganga iliyopo wilaya ya Iringa mkoani Iringa maarufu kwa jina la Tosamaganga Alumni Association wakiwa katika hospital ya Tosamaganga.

Na Fredy Mgunda,Iringa
Wanafunzi waliowahi kusoma shule ya sekondari ya Tosamaganga iliyopo wilaya ya Iringa mkoani Iringa maarufu kwa jina la Tosamaganga Alumni Association wametoa msaada wa mashuka sabini na tano na vifaa tiba vyenye thamani ya shilingi 1,672,500 katika hospitali ya Tosamaganga iliyopo katika katta ya kalenga mkoani Iringa kwa lengo la kuendelea kuboresha sekta ya afya ikizingatiwa kuwa wengi wao waliwahi kutibiwa hapo wakati wanasoma.

akizungumza wakati wa hafla ya kukadhi msaada huo mwenyekiti wa kamati ya Tosamaganga Alumni association ambaye pia ni mkurugenzi Mtendaji wa kampuni ya Umoja Switch inayotoa huduma ya mashine za kutolea fedha (ATM) katika benki mbalimbali nchini, Danford Mbilinyi alisema kuwa walijipanga kuja kutoa msaada huu kwa kuwa wangi wao walikuwa wanatibiwa katika hospital hiyo wakati wakiwa masomoni miaka mingi iliyopita.

“Leo hii tunaafya njema kwa ajili tulitibiwa vizuri kipindi tulivyokuwa tunaumwa na ilitusaidia kufanya vizuri masomo yetu na ndio maana leo hii tupo hapa bila kupata huduma iliyobora nafikiri wengi wetu tusinge kuwa hapa” alisema Mbilinyi

Mbilinyi alisema kuwa wamechangisha kidogo walichopata wameamua kununua vifaa hivyo ambavyo wanafikiri vitakuwa na msaada kwa wagonjwa waliopo hospitalini hapo.
“Hiki kidogo tu lakini tunajua kwa namna moja au nyingine vinaweza kuwasaidia wagonjwa na kuwapunguzia mzigo uongozi wa hospitali yetu pendwa ambayo imekuwa ikitutibu kwa muda mrefu sana kipindi tukiwa masomoni katika sekondari ya Tosamaganga” alisema Mbilinyi

Dr Steven Biginagwa ni daktari bingwa wa magonjwa ya watoto na mtafiti wa ugonjwa wa malaria alisema kuwa hospital hiyo iliokoa maisha yake kwa kupata huduma bora kwani alikuwa na ugonjwa wa utumbo kujifunga  lakini madaktari waliokoa maisha yangu hadi hii leo.

“Mimi nililazwa hapa mwezi wa kwaza na mwezi wa pili wa masomo nilipata matatizo ya huo ugonjwa lakini nashukuru mungu kuwawezesha wahudumu wote wa hii hospital kunitibu na kuokoa maisha yangu hadi leo nipo na afya yangu njema na mfanyakazi niliajiliwa hivyo bila kuwepo kwa hospital hii sijui leo hii ningekuwa wapi” alisema Dr Biginagwa

Dr Biginagwa alisema kuwa licha ya kumaliza masomo yake lakini mitihani mine ya mwisho alifanyia hodini akiwa amelazwa kutokana na ugonjwa aliokuwa nao na madaktari walimsaidia kupata huduma bora ndio maana alifanya vizuri mitihani kwenye mitihani na kufaulu vizuri.

“Kwa miaka yangu vyote miwili nimekuwa nikishinda sana hapa hospitalini lakini mungu alisaidia nikamaliza masomo yangu na nafikiri kutokana na hudumu nilikuwa napewa hapa ndio iliyonipelekea kwenda kusomea udaktari na ndio maana hadi leo hii mimi ni daktari bingwa wa magonjwa ya watoto” alisema Dr Biginagwa

Kwa upande wake mkurugenzi mtendaji wa TASAF Ladslausi Mwamanga aliwaomba wananchi popote walipo hapa nchi kukumbuka kutoa msaada waote katika hospital ili kuendelea kuboresha sekta ya afya kwa kuwa serikali bila wadau haiwezi kukamilisha kila kitu yenyewe.

“Unajua kuwa serikali inamambo mengi ambayo inayaofanya hivyo kukamilisha kila kitu kwa wakati ni vigumu sana hivyo sasa sisi wadau tuendelee kuisaidia serikali kwa kile tuchokipata kutoa msaada kwenye sekta hii ya afya ambayo inachangamoto nyingi sana” alisema Mwamanga

Naye diwani wa kata ya Kalenga Thobias Kangalawe aliwashukuru wanafunzi hao waliosoma shule ya Tosamaganga miaka iliyopita kwa niaba ya uongozi wa hospitali ya Tosamaganga,alisema kuwa ni nadra sana kuona watu wanakumbuka walikopatia mafanikio na kutoa msaada kama wenu.

Nyinyi watu wa kipekee kabisa toka nimekuwa kiongozi siajwahi kuona kundi kubwa lenye kujali wapi walikotoa na kuendelea kutafuta njia mbdala za kusiadia kutatua changamoto kama nyinyi hivyo hongeni na namuomba mungu awaongezee pale mlipo punguza” alisema kangalawe

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.