Habari za Punde

Sweden Yaipatia Tanzania Msaada wa Kibajeti wa Shs.Bilioni 436.

Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mipango, Bw. Doto James (wa pili kulia) na Mkuu wa Kitengo cha Ushirikiano na Maendeleo wa Ubalozi wa Sweden nchini Tanzania Bw. Ulf Kallsting (wa pili kushoto) wakisaini Makubaliano ya Msaada wa jumla ya Sh. bilioni 435.79 kwa ajili ya Msaada wa kibajeti na  kusaidia mpango wa elimu, katika ukumbi wa Wizara ya Fedha na Mipango Jijini Dar es Salaam.
Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mipango, Bw. Doto James (kulia)na Mkuu wa Kitengo cha  Ushirikiano na Maendeleo wa Ubalozi wa Sweden nchini Tanzania Bw. Ulf Kallsting (kushoto) wakisaini Makubaliano ya Msaada wa jumla ya Sh. bilioni 435.79 kwa ajili ya Msaada wa kibajeti na  kusaidia mpango wa elimu, katika ukumbi wa Wizara ya Fedha na Mipango Jijini Dar es Salaam.
Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mipango, Bw. Doto James (kulia) na Mkuu wa Kitengo cha Ushirikiano na Maendeleo wa Ubalozi wa Sweden nchini Tanzania Bw. Ulf Kallsting (kushoto) wakibadilishana Mkataba wa  Msaada wa wa jumla ya Sh. bilioni 435.79 kwa ajili ya Msaada wa kibajeti na  kusaidia mpango wa elimu, katika ukumbi wa Wizara ya Fedha na Mipango Jijini Dar es Salaam.
Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mipango, Bw. Doto James (kulia) na Mkuu wa Kitengo cha  Ushirikiano na Maendeleo wa Ubalozi wa Sweden nchini Tanzania Bw. Ulf Kallsting (kushoto) wakiwa wameinua juu Mkataba wa  Msaada wa wa jumla ya Sh. bilioni 435.79 kwa ajili ya Msaada wa kibajeti na  kusaidia mpango wa elimu, katika ukumbi wa Wizara ya Fedha na Mipango Jijini Dar es Salaam.
Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mipango, Bw. Doto James akizungumza na waandishi wa habari kuhusu msaada wa jumla ya Sh. bilioni 435.79 kutoka Sweden kwa ajili ya Msaada wa kibajeti na kusaidia mpango wa elimu, ambapo amesema msaada huo unatoa fursa kwa  Serikali kupeleka fedha zilizotakiwa kutekeleza majukumu hayo maeneo mengine ya Maendeleo ya Wananchi, hafla iliyofanyika Jijini Dar es Salaam
Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mipango, Bi Amina Khamis Shaaban (Kushoto), Kamishna Msaidizi wa Fedha za Nje wa Wizara hiyo Bi. Mamelta Mutagwaba na wengine wakishuhudia utiaji saini wa Mkataba wa  Msaada wa wa jumla ya Sh. bilioni 435.79 kwa ajili ya Msaada wa kibajeti na  kusaidia mpango wa elimu, katika ukumbi wa Wizara ya Fedha na Mipango Jijini Dar es Salaam.
Maafisa waandamizi kutoka Ubalozi wa Sweden Nchini Tanzania wakishuhudia utiaji saini wa Mkataba wa  Msaada wa wa jumla ya Sh. bilioni 435.79 kwa ajili ya Msaada wa kibajeti na  kusaidia mpango wa elimu, katika ukumbi wa Wizara ya Fedha na Mipango Jijini Dar es Salaam.
Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mipango, Bw. Doto James (wa pili kushoto), Mkuu wa Kitengo cha Ushirikiano na Maendeleo wa Ubalozi wa Sweden nchini Tanzania Bw. Ulf Kallsting (wapili kulia) pamoja na Maafisa waandamizi kutoka Wizara ya Fedha na Mipango na Ubalozi wa Sweden wakiwa katika Picha ya pamoja baada ya kusainiwa  Mkataba wa  Msaada wa wa jumla ya Sh. bilioni 435.79 kwa ajili ya Msaada wa kibajeti na  kusaidia mpango wa elimu, katika ukumbi wa Wizara ya Fedha na Mipango Jijini Dar es Salaam.


(Picha na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini-Wizara ya Fedha na Mipango)


Sweden imeipatia Tanzania Msaada wa jumla ya Fedha ya Sweden SEK. Bilioni 1.64 ambayo ni sawa na takribani Sh. bilioni 435.79 kwa ajili ya Msaada wa kibajeti na  kusaidia mpango wa elimu. 

Makubaliano ya msaada huo yamesainiwa Jijini Dar es Salaam kati ya Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mipango, Bw. Doto James na Mkuu wa Kitengo cha  Ushirikiano na Maendeleo wa Ubalozi wa Sweden nchini Tanzania Bw. Ulf Kallsting.

Bw. James alisema kuwa imesainiwa Mikataba mitatu ya msaada huo ambayo ni; mkataba kwa ajili kusaidia Bajeti ya Serikali wa kiasi cha SEK milioni 600 ambazo ni sawa na Sh. bilioni 159.59 kwa kipindi cha kuanzia mwaka 2017/18 hadi 2019/2020, ambapo kwa mwaka wa fedha 2017/2018 watatoa takribani Sh. bilioni 53.20.

Alisema fedha hizo zitaelekezwa katika kuboresha uhalisia wa Bajeti ili kuweza kutimiza majukumu ya kisera, kuimarisha ukusanyaji wa mapato ya ndani ya kikodi na yasiyo ya kodi na pia kusaidia Serikali kutoa huduma nzuri kwa wananchi kupitia taratibu za manunuzi. 

Mkataba mwingine ni kwa ajili ya kusaidia Mpango wa Elimu kwa Matokeo (EPforR) wa kiasi cha Fedha ya Sweden SEK milioni 885 ambayo ni sawa na Sh. bilioni 235.40 kuanzia mwaka 2017/18 hadi 2020/2021.

“Lengo la msaada huu ni kusaidia Mpango wa Elimu kwa Matokeo ambapo tunapimwa namna ambavyo tumeweza kutimiza wajibu wetu tuliojiwekea katika bajeti. Baada ya ya Serikali kutimiza wajibu wake wa kupeleka fedha katika Sekta ya Elimu kwa wakati, wameamua kutupatia fedha hizo ambazo Serikali tunazipangia kazi kulingana na vipaumbele”, alieleza Bw. James.

Alieleza kuwa Mpango wa Elimu kwa Matokeo ulianza mwaka 2015/ 2016 na katika kipindi hicho yamepatikana maendeleo makubwa katika ujenzi wa miundombinu ya madarasa, vyoo, mabweni. Utekelezaji wake umefanywa katika shule 361 kwenye Halmashauri 129 nchini.

“Katika Mpango huo Vyuo 17 vya Walimu vimekarabatiwa ikiwa ni pamoja na kununua Kompyuta 260, Magodoro 6,730 na viti 1,976. Mpango huu unafanikiwa kutokana na dhamira ya Serikali ya Awamu ya Tano ya kuweka mkazo katika Sekta ya Elimu hivyo kupeleka fedha kwa wakati jambo linalosababisha washirika wa maendeleo wazidi kutuamini” alifafanua Bw. James.

Mkataba wa tatu ni Marekebisho ya Mkataba wa  Mpango wa Kusoma, Kuhesabu na Kuandika ambao una kiasi cha Dola za Marekani 94.8 zilizotolewa na Taasisi ya Kimataifa ya Global Partnership for Education (GEP) na kukabidhiwa kwa nchi ya Sweden ili iweze kuusimamia.

Akifafanua kuhusu Mkataba huo Bw. Doto James alisema kuwa Serikali ili saini Mkataba  huo na Sweden Mei, 2015 na muda wa utoaji wa fedha hizo ulikwisha Agosti, 2016 na kubakia kiasi cha Dola milioni 18.3 ambazo zitapatikana baada ya kusainiwa kwa mkataba huo.

Kwa upande wake Mkuu wa Kitengo cha Ushirikiano na Maendeleo katika Ubalozi wa Sweden nchini Tanzania Bw. Ulf Kallsting amesema kuwa nchi yake imedhamiria kuhakikisha inajenga uwezo na ujuzi  kwa watanzania kuanzia elimu ya Awali kwa kuwa  nchi yake inathamini sana elimu.

Bw. Kallsting alisema kuwa Tanzania imekuwa na uhusiano mzuri na Sweden na  inatekeleza kwa ufanisi miradi mbalimbali hivyo  nchi yake itaendelea kuisaidia Tanzania katika maeneo mbalimbali ya Maendeleo ili kufanikisha mipango yake.

Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mipango, Bw. Doto James ameishukuru Sweden kwa niaba ya Serikali kwa kuendelea kuisaidia Tanzania katika kutekeleza bajeti yake.

Imetolewa na;
Benny Mwaipaja
Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
Wizara ya Fedha na Mipango

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.