Habari za Punde

Zanzibar Heroes yawasili kisiwani Pemba

 MELI ya Mv Mapinduzi II ikiwasili katika bandari ya Mkoani, ikiwa imebeba wachezaji wa Timu ya Taifa ya Zanzibar Heroes na Kikundi cha Tarab cha Taifa.(PICHA NA ABDI SULEIMAN, PEMBA.)
 VIONGOZI mbali mbali wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar wakiongozwa na Naibu Waziri wa Harabi Utalii,Utamaduni na Michezo Zanzibar Mhe:Chumu Kombo Khamis, wakuu wa wilaya, Maafisa wadhamini na wananchi mbali mbali wa Pemba, wakiwasubiri kuwapokea wachezaji wa timu ya Zanzibar Heroes.(PICHA NA ABDI SULEIMAN, PEMBA.)
 MSHAURI wa Rais mambo ya Utamaduni Zanzibar Chimbeni Kheir, akiteremka katika meli ya Mv Mapinduzi II, iliyowasili katika bandari ya mkoani na mashujaa wa timu ya Zanzibar Heroes.(PICHA NA ABDI SULEIMAN, PEMBA.)
 NAIBU waziri wa Habari, Utalii, Utamaduni na Michezo Zanzibar, Mhe:Chumu Kombo Khamis, akisalimiana na Mshauri wa Rais mambo ya Utamaduni Zanzibar Chimbeni Kheir, mara baada ya kuwasili na msafara wa wachezaji wa timu ya Zanzibar Heroes Katika bandari ya Mkoani.(PICHA NA ABDI SULEIMAN, PEMBA.)
 WACHEZAJI wa Timu ya Zanzibar Heroes wakiongozwa na Kocha makuu wa timu hiyo, Hemed Morocco wakiteremka katika maeli ya Mv Mapinduzi II katika bandari ya Mkoani, kwa lengo la kucheza mchezo wa kirafiki na Timu ya Pemba Kombaini.(PICHA NA ABDI SULEIMAN, PEMBA.)
 WACHEZAJI wa Timu ya Taifa ya Zanzibar (Zanzibar Heroes) wakisalimiana na viongozi mbali mbali wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, baada ya kuwasili katika bandari ya mkoani kwa ajili ya mchezo wa kirafiki dhidi ya Pemba Kombaini.(PICHA NA ABDI SULEIMAN, PEMBA.)
 WADAU na Mashabiki mbali mbali wa soka wakiwapokea na kuwashangiria mashujaa wa Timu ya Taifa ya Zanzibar (Zanzibar Heroes) baada ya kuwasili katika bandari ya Mkoani.(PICHA NA ABDI SULEIMAN, PEMBA.)
BRASSBAND ya vijana chipukizi Kisiwani Pemba, wakiongoza maandamano ya wachezaji na Viongozi wa Timu ya Taifa ya Zanzibar (Zanzibar Heroes) walipowasili katika bandari ya Mkoani Kisiwani Pemba.(PICHA NA ABDI SULEIMAN, PEMBA.)

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.