Habari za Punde

Rais wa Zanzibar Dk. Ali Mohamed Shein Atembelea Kiwanda cha Kusindika Samaki. Sharjah.

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein, akipata maelezo ya uhifadhi wa samaki kwa ajili ya kusafirisha Nje ya Nchi wakati alipotembelea kiwanda hicho akiwa katika ziara yake katika Nchi za Umoja wa Nchi za Kiarabu UAE. 

Katika ziara yake mjini Sharja Dk. Shein alipata fursa ya kutembelea eneo la shughuli za uvuvi la ‘East Fishing Processing LLC”, lililoko Al Jurf  katika eneo la Ajman  na kupata maelezo juu ya namna ya eneo hilo lenye kiwanda kikubwa cha kisasa cha samaki jinsi kinavyosarifu  na kuhifadhi samaki pamoja na kuwaweka katika mfumo maalum wa kwa ajili ya kuuzwa.
Kwa mujibu wa Mkurugenzi Mkuu wa Kampuni hiyo inayolishirikisha kundi la Kampuni ya THOMSUN, K.V. Thomas alimueleza Rais Dk. Shein namna na kiwanda hicho kinavyosarifu samaki wa aina mbali mnali wakiwemo kamba kutoka nchi mbali mbali ikiwemo Tanzania.

Dk. Shein kwa upande wake alipendezewa na namna kiwandaa hicho kinavyofanya kazi na kutokana na juhudi zinazoendelea kuchukuliwa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar katika sekta ya uvuvi na viwanda vya samaki pamoja na azma ya kuanzisha Kampuni ya Uvuvi, Rais Dk. Shein alisisitiza haja ya kuwepo kwa mashirikiano ya pamoja ili Zanzibar ipate kupanua wigo katika sekta hiyo.

Kutokana na kiwanda hicho kutumia teknolojia ya kisasa katika kusarifu samaki wa aina mbali mbali pia, soko la ajira limeonekana kuchukua fursa yake kutokana na kuajiri vijana wengine hatua ambayo Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar imo katika kupambana na changamoto iliyopo katika suala zima la ajira.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.