Habari za Punde

JESHI LA ZIMAMOTO NA UOKOAJI LAFUNGA MAFUNZO YA UZAMIAJI MAJINI KINA KIREFU.

Kamishna wa Operesheni wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji, (CF) Billy Mwakatage, akipokelewa na Maafisa wa Jeshi hilo pamoja na mwenyeji wake ambaye ni mmiliki wa Yatch Club Bw. Brian Fernandes, alipokwenda kufunga mafunzo ya uzamiaji majini kina kirefu daraja la pili kwa Askari wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji. Mafunzo hayo yalikuwa yakifanyika katika kisiwa cha Bongoyo kilichopo ndani ya bahari ya hindi, Jijini Dar es Salaam.
Mzamiaji wa kikosi maalum cha Uokoaji majini wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji, Sajini Gift Longwe, akionesha mbinu mbalimbali za uzamiaji majini kwenye kina kirefu walizojifunza toka kwa wakufunzi kutoka nchini Ujerumani,  kwa mgeni rasmi Kamishna wa Operesheni wa Jeshi hilo, (CF) Billy Mwakatage (hayupo pichani). Wakati wa hafla ya kufunga mafunzo ya uzamiaji majini kina kirefu daraja la pili kwa Askari wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji, mapema leo Jijini Dar es Salaam. 
Kamishna wa Operesheni wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji, (CF) Billy Mwakatage (katikati), akimkabidhi cheti mmoja ya wahitimu wa mafunzo ya uzamiaji majini kina kirefu, Sajini Gift Longwe (kushoto). Wakati wa hafla ya kufunga mafunzo ya uzamiaji majini kina kirefu daraja la pili kwa Askari wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji, mapema leo Jijini Dar es Salaam. 

Wazamiaji wa kikosi maalum cha Uokoaji majini wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji, Sajini Gift Longwe (kushoto) na Koplo Siwizan Kazimoto (kulia), wakionesha umahili wao wa uzamiaji majini kwenye kina kirefu mbele ya mgeni Kamishna wa Operesheni wa Jeshi hilo, (CF) Billy Mwakatage (hayupo pichani). Wakati wa hafla ya kufunga mafunzo ya uzamiaji majini kina kirefu daraja la pili kwa Askari wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji, mapema leo Jijini Dar es Salaam. (Picha na Jeshi la Zimamoto Na Uokoaji)

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.