Habari za Punde

Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar Dkt.Idrissa Muslim Hija Amewataka Wahitimu wa Kidatu cha Sita Wasome Kwa Mashirikiano.Wahakikishe Wanakuwa na Marafiki Wema Ili Kupata Mafanikio.


Katibu Mkuu Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar Mhe. Dkt. Idrissa Muslim Hija, akizungumza na kutowa nasaha zake kwa Wanafunzi Waliofanya vizuri Mitihani yao ya Kidatu cha Sita kwa mwaka 2017/2018 kwa kupata Daraja la Kwanza, wakati wa hafla ya kukabidhiwa zawadi na Uongozi wa PBZ kwa kufanya vizuri mitihani yao na kujiandaa na Elimu ya Juu.

KATIBU Mkuu wa Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali 
Zanzibar Idrissa Muslim Hija amewataka wahitimu wa kidatu cha sita wasome kwa mashirikiano,waondokana na ubinafsi  na wahakikishe wanakuwa na marafiki wema ili kupata mafanikio waliyoyakusudia.
Aliyasema hayo katika sherehe ya  kukabidhiwa zawadi za fedha na Benki ya Watu wa Zanzibar Ltd kwa wanafunzi wa kidatu cha sita waliofaulu daraja la kwanza kwa Skuli za Sekondari za Unguja na Pemba,katika viwanja vya Kariakoo mjini hapa.
Alisema  masomo ya ngazi ya juu daraja la kwanza ni magumu hivyo inahitajika juhudi na mikakati iliobora ili waweze kufaulu vyema.
Aliwataka wanafunzi hao kujenga ari,hamasa na bidii zaidi katika masomo yao ili kuijengea heshima nchi yao ya Zanzibar hasa ikizingatiwa dharau si jambo jema.
“Ubinafsi epukeni nao kwani siku zote hauleti neema nawaombeni mnapokwenda shirikianeni,saidianeni muweze kufanikiwa “,alisisitiza.
Aidha aliwashauri wanapomaliza masomo wahakikishe wanarejea nyumbani kwao kwani taifa linawahitaji kwa ajili ya uimarishaji wa maendeleo na uchumi. 

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.