Na.Abdi Shamnah Zanzibar.
Wadau wanaotumia fukwe za bahari nchini wametakiwa kuweka vifaa maalum kwa ajili ya
kuhifadhia taka zinazozalishwa na binadamu, ili kuepuka uharibifu wa mazingira.
Hayo
yameelezwa na wananchi mbali mbali walioshiriki katika zoezi la usafi wa
mazingira katika fukwe za bahari ya Muyuni Kijini, skuli ya msingi Mbuyu Tende
pamoja na Kijini.
Zoezi
hilo lililowashirikisha walimu, wanafunzi, wafanyakazi wa Hoteli ya Mnemba
Island, mapapasi pamoja na wananchi ,
limeratibiwa na Kampuni ya Penny Royal kupitia mradi wa Best of Zanzibar, ikiwa
ni maadhimisho ya siku ya Afya Duniani.
Akizungumza
na washiriki wa zoezi hilo, Mkuu wa Wilaya Kaskazini ‘A’ Unguja, Hassan Ali
Kombo alisema kuna umuhimu mkubwa kwa wananchi wa ukanda wa Pwani kujenga
utamaduni endelevu wa kufanya usafi katika maeneo wanayoishi, ikiwemo fukwe ya
bahari.
Alisema
ni vyema kwa watumiaji wa fukwe za bahari, ikiwemo watembeza watalii kuweka
vifaa maalum ili kuhifadhia taka, kwa
kuzingatia kuwepo ongezeko kubwa la mabaki ya vifaa vitokanavyo na plastik,
kama vile chupa za maji, lotion na kadhalika.
Alisema
ili kuondokana na magonjwa mbali mbali ya miripuko pamoja na kuvutia wageni,
kuna ulazima kwa jamii kujibidisha katika suala la kufanya usafi katika maeneo
yao.
‘‘Halmashauri
iandae utaratibu wa kuweka vifaa katika maeneo ya fukwe na yale yenye
uzalishaji mkubwa wa taka, ili kuangalia uwezekano wa baadhi yake kuzifanyia ‘recyling’
baaade’’, alisema.
Mkuu
huyo wa Wilaya aliipongeza Kampuni ya Penny Royal kupitia mradi wa Best of Zanzibar
kwa hatua zake za kuunga mkono juhudi za Serikali ya Wilaya hiyo katika
kuimarisha usafi wa mazingira katika maeneo mbali mbali.
Mapema,
Mkurugenzi wa Mradi wa Best of Zanzibar Aminata Keita, alisema zoezi hilo
lililowashirikisha wanafunzi limelenga kuwajengea utamaduni wa kuendeleza usafi
katika maisha yao.
Alisema
skuli za Kijini na Mbuyutende zinapitiwa na mradi mkubwa wa ujenzi wa Hoteli ya
Kitalii, ambapo kw anykati tofauti zimekuwa zikihusishwa katika programu mbali
mbali ikiwemo elimu ya Afya.
Alisema
zoezi hilo limelengwa kuondokana na mrundikano wa takataka zinazozalishwa na
binadamu, ikiwemo mifuko ya plasiti na mabaki mengine ya vifaa vinavyotokana na
matumizi ya binadamu katika eneo la ukanda huo.
Nae,
Ofisa kutoka Mamlaka ya Mazingira Zanzibar Hashim Salum Hashim, alipongeza
juhudi na mwamko wa wananchi wa maeneo hayo kwa kujitokeza kwa wingi kushiriki
katika Kampeni hiyo ya jusafi wa mazingira.
‘‘
Tuna kila sababu ya kupongeza, mwamko wa jamii ni mkubwa, kiasi ambacho wageni
wanaonekana kufurahia sana, unaona wale kama ingelikuwa fukwe sio safi, katu
wasingeweza kulala pale kwenye mchanga,
juhudi iliyofanyika inafaa kupongezwa’’, alisema Salum.
Alitowa
wito kwa watembeza watalii na wadau wengine wanaoambatana na wageni kwa ajili
ya mapumziko kwenye fukwe hizo, kuandaa utaratibu wa kuweka vifaa, ili
kuhifadhi mabaki ya bidhaa wanazotumia.
Alisema
wageni ikiwemo watalii ni aina ya watu waliojengeka katika utamaduni wa kutii sheria,
hivyo ni dhahiri pale patakapokuwa na vifaa hivyo, hawatosita kuvitumia.
Mwanafunzi
Mariamu Hassan kutoka Skuli ya Mbuyu tende alisema ni muhimu kwa jamii kuwa na
utaratibu endelevu wa kufanya usafi katika maeneo wanayoishi, ili kuondokana na
matatizo mbali mbali ikiwemo ugonjwa wa mri[puko.
Alisema
zoezi hilo limefanikiwa vyema, hivyo na kusisitiza umuhmu wa kuendeleza
utamaduni wa kufanya usafi katika maeneo mbali mbali ikiwemo fukwe za bahari,
kwani ni eneo hilo moja la vivutio vya utalii.
Wastani
wa wananchi 200 walishiriki katika zoezi la usafi wa mazingira katika maeneo
hayo, ambapo kiasi cha tani saba za taka zilikusanywa.
No comments:
Post a Comment