Waziri wa Habari, Utalii na Mambo ya Kale, Mhe.Mahmoud Thabit Kombo akizungumza na
waandishi wa habari wa vyombo mbalimbali kuhusiana na maonesho ya utalii
(Tourism show) yatakayofunguliwa katika
Hoteli ya Verde iliopo Mtoni Unguja , mkutano huo ulifanyika katika Hoteli ya
Park Hyatt iliopo Shangani mjini Unguja
Katibu Mtendaji wa Kamisheni ya Utalii Zanzibar, Dk. Abdula Mohammed Juma akizungumza
na waandhishi wa habari wa vyombo mbalimbali kuhusiana na ufunguzi wa maonesho
ya utalii Zanzibar (Tourism show) yatakayofanyika katika Hoteli ya Verde Mtoni
Mwandishi wa Habari wa Gazeti la Tanzania daima, Talib Ussi akiuliza suala katika
mkutano kuhusiana na ufunguzi wa maonesho
ya utalii Zanzibar, uliofanyika katika Hoteli ya Park Hyatt iliopo Shangani
Tabia Makame mwandishi wa habari wa Redio ya Bahari Fm akiuliza suala katika mkutano kuhusiana na ufunguzi wa maonesho ya Utalii
Zanzibar, uliofanyika katika Hoteli ya Park Hyatt iliopo Shangani
Waziri wa Habari, Utalii na Mambo ya Kale Zanzibar Mhe. Mahmoud Thabit Kombo akifafanua jambo wakati wa mkutano na waandishi wa habari wa vyombo mbalimbali vilioko Zanzibar kuhusiana na kukamilika kwa maandalizi ya Tamasha la Kitalii Zanzibar linalotarajiwa kufanyika katika Hoteli ya Verde Mtoni Zanzibar,mkutano huo ulifanyika katika Hoteli ya
Park Hyatt iliopo Shangani mjini Unguja
Mwenyekiti wa Bodi ya Kamisheni ya Utalii Zanzibar, Sabah Saleh Ali akitoa ufafanuzi katika mkutano wa
waandishi wa habari kuhusiana na ufunguzi wa maonesho ya Utalii Zanzibar
(Tourism show), mkutano huo ulifanyika katika Hoteli ya Park Hyatt iliopo
Shangani mjini Unguja
Meneja wa Hoteli ya Kitalii ya Park Hyatt,Mr.Nicolas Cedro akichangia
katika mkutano wa waandishi wa habari ulijadili ufunguzi wa maonesho ya Utalii
Zanzibar, yanayotarajiwa kufanyika tarehe 17/10/2018.
Waandishi wa habari wa Vyombo mbalimbali vya habari vilioko Zanzibar wakifuatilia Mkutano huo na Waziri wa Habari Utalii na Mambo ya Kale Zanzibar Mhe. Mahmoud Thaibt Kombo uliofanyika katika ukumbi wa Hoteli ya Kitalii ya Park Hyatt Shangani Zanzibar.
Waandishi wa Habari wa Vyombo mbalimbali vilioko Zanzibar wakifuatilia mkutano huo uliofanyika katika hoteli ya Park Hyatt Shangani Zanzibar.(Picha na Haroub Hussein)
No comments:
Post a Comment