Habari za Punde

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dk.Ali Mohamed Shein, Azungumza na Rais wa Seychelles Mhe. Danny Faure Jijini Nairobi Kenya.


Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Ali.Mohamed Shein, akizungumza na Rais wa Seychelles Mhe. Danny Faure, walipokutana kwa mazungumzo yaliofanyika katika ukumbi wa Hoteli ya Inter Continental Jijini Nairobi Nchini Kenya.

Na.Mwandishi Maaluum Nairobi.
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein, alikutana na kufanya mazungumzo na Rais wa  Seychelles Danny Faure katika ukumbi wa Hoteli  ya Intercontinental   Mjini Nairobi,na  kueleza kwamba  Zanzibar na Seychelles zina mazingira ya kijiografia na  shughuli za kiuchumi zilizofanana na  watu wa  nchi hizo wamekuwa wakishirikiana katika  shughuli mbali mbali za kiuchumi  na kijamii.

Katika mazungumo hayo, Dk Shein alihimiza haja ya kuimarisha uhusiano wa kidugu na kihistoria uliopo baina ya nchi mbili hizo
Katika kikao hicho  Dk. Shein alikumbushia mambo mbali mbali waliozungumza na Rais wa Zamani wa  Seychelles Mheshiwa  James Michel  walipokutana wakati wa  Mkutano wa Nchi za Visiwa wa Samoa mwezi Septemba mwaka 2014.

Alisema viongozi hao walipokutana walizungumza haja ya kuimarisha mashirikiano katika masuala mbali mbali ya uchumi wa bahari, ikiwemo sekta ya utalii, uvuvi , usafiri wa anga na masuala, kwa kuzingatia kwamba hayo ni maeneo muhimu ya kiuchumi kwa nchi wanachama wa Jumuiya ya Nchi zinazopakana na Bahari ya Hindi (IORA).

Dk. Shein alisema kwamba itakuwa ni vyema Serikali iliyopo madarakani hivi sasa na Rais Danny Faure ni vyema ikaendeza ushirikiano katika maeneo hayo na mengine mapya kwa kuzingatia mahitaji ya wananchi  na mwenendo wa kiuchumi wa hivi sasa.

Aidha, Dk Shein alileleza   kwamba Serikali ya Mapinduzi  ya Zanzibar na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania zitaendeleza kushirikiana na Serikali ya Seychelles katika   masuala ya ulinzi na salama.

Vile vile, alihimiza haja ya  viongozi wa pande hizo mbili  kuwa na utaratibu wa kutembeleana mara kwa mara,na kusisitiza haja ya viongozi pia  kukutana pamoja kwa ajili ya kubainisha na hatimae kutiliana saini maeneo  ya ushirikiano baina ya Seychelles na Zanzibar .

Kwa upande wake  Mheshimiwa Danny Faure  alitoa shukurani kwa Dk .  Shein kwa kutenga muda maalumu wa kukutana kwa ajili ya kujadili masuala muhimu ya kiuchumi na kijamii kwa ajili ya kuimarisha ustawi wa wananchi wa pande mbili hizo.

Alieleza kwamba ushirikiano  biana ya  Seychelles na Zanzibar una historia ndegu na umezidi kuimairika baada ya kuundwa kwa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Alitoa historia ya ushirikiano baina ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Seychelles kabla ya nchi hiyo kupata uhuru mwaka 1976 na baada ya kupata huru.

Alieleza kwama wananchi wa Seychelles  wanakumbuka na kuthamini mchango wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika masuala mbali mbali ya kiuchumi, kiulinzi na kiusalama, na watahakisha wanaendeleza uhusiano huo.

Alieleza kwamba amefurahi  kupata taarifa ya mazungumzo   aliyofanya Dk. Shein na   Seychelles na Rais aliyeondoka madaakani,   James Michel  walipokutana wakati wa  Mkutano wa Nchi za Visiwa wa Samoa mwezi Septemba mwaka 2014.

Alisema kwamba maeneo ya ushiriakiano waliyoyadili nchini Samoa ni muhimu na  Serikali yake iko tayari kuyaendeleza na kuongeza  maeneo mapya ambayo yataonekana muhimu kwa pande mbili hizo.

Alieleza kwamba nchi yake iko tayari kushirikiana na Zanzibar katika kuimarisha sekta ya utalii, biashara, uhifadhi wa mazingira, ulinzi na usalama na maeneo yote muhimu katika kuendeleza uchumi endelevu wa bahari kama  kwa kuzingatia malengo ya mkutano wa uchumi  endelevu wa bahari uliowakutanisha viongoi hao mjini Nairobi

Mheshimiwa Danny Faure  nae alisititiza juu ya haja ya viongozi  wakuu wa sekta mbali mbali wa Zanzibar na Seychelles  kukutana  kwa ajili ya kujadili na hatimae kusaini makubalino ya maeneo ya ushirikiano kwa faida ya pande zote  mbili.

Viongozi hao waliagana  kwa kila mmoja kumtakia  mwenzake safari njema ya kurudi nyumbani.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.