Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dk. Ali Mohamed Shein, akiwa amesimama wakati ukipigwa Wimbo wa Taifa baada ya kuwasili katika Uwanja wa Kufurahishia Watoto Tibirinzi Chakechake Pemba, kulia Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mhe. Balozi Seif Ali Iddi na kushoto Waziri wa Vijana Michezo Sanaa na Utamaduni Balozi Ali Karume, Katibu Mkuu Kiongozi Dkt. Abdulhamid Yahya Mzee.
KATIBU Mkuu
wa Wizara ya Vijana,Utamaduni,Sanaa na Michezo Omar Hassan ‘King’
amesema
tayari Wizara hiyo imekipatia Kikundi
cha Taarabu cha Taifa ofisi za kuendeshea shughuli zake pamoja na kuwa na
bajeti ili kukidhi mahitaji ya msingi.
Amesema
pamoja na mambo mengine, Wizara imetekeleza kikamilifu maagizo ya Serikali ili
kukiwezesha kikundi huicho kufanya shughuli zake kwa ufanisi pamoja na kuleta
ustawi bora wa wasanii wanaokitumikia.
King,
amesema hayo jana katika Uwanja wa kufurahishia watoto Tibirinzi Chake-chake
Pemba, katika taarabu maalum iliyoandaliwa, ikiwa ni miongoni mwa shamra shamra
za miaka 55 ya Mapinduzi ya Zanzibar.
Rais wa
Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Ali Mohamed Shein alikuwa
mgeni rasmi katika taarabu hiyo, ambapo mamia ya wananchi kutoka mikoa yote ya
Zanzibar walijumuika na kukonga nyonyo zao vilivyo.
Akitoa
taarifa za utekelezaji wa maagizo hayo, alisema tayari wasanii wa kikundi hicho
wameanza kupokea mirahaba kutokana na nyimbo 12 walizozisajili pamoja na kujiingizia
mapato kutokana na ushirikiano uliopo kati ya kikundi hicho na baadhi ya taasisi, kama vile ZSTC.
Katika hafla
hiyo, kikundi hicho kilicho chini ya Uenyekiti wa Msanii nguli Idd Suweid,
kiliibuka na nyimbo kadhaa, zikiwemo zile zenye mnasaba na Mapinduzi, ambapo
magwiji wa sanaa hiyo walighani na kukonga vilivyo nyonyo za watazamaji/wasikilizaji.
Miongoni mwa
nyimbo zilizounogesha usiku huo ni
pamoja na ‘’miaka 55 ya Mapinduzi” iliyoimbwa na Pro. Gogo, “anaetowa ni Mola’’
iliyoghaniwa na al-anisa Sada Mohamed, ‘tarehe 11 (Idd Siweid), ‘‘Ni yeye’’
pamoja na ‘’umewashuka” iliyoimbwa an
al-anisa Amina Ramadhan.
Nyengine ni “Wahoi’’,
“Njoo kwa mtu mkweli’’ (al-anisa Rukia Ramadhan), “maisha ya Vijijini’’
iliyoghaniwa na chiriku Hilda Mohamed, “mpewa hapokonyeki” , “kama kupenda ni
dhara’’ iliyoimbwa na ‘sauti ya Zege’ Makame Faki pamoja na ‘’ninae’’
iliyoghaniwa vyema na mpendwa na wengi Idd Suweid.
Kikundi cha
Taarabu cha Taifa kina jumla ya wasanii 35 wanaotoka katika vikundi saba vya
taarabu hapa Zanzibar.
Abdi Shamnah,
Ikulu Zanzibar
Postal Address: 2422 Tel.:0777476982. Fax:
024 2231822
E-mail: abdya062@gmail.com
No comments:
Post a Comment