Habari za Punde

Kutokuandika Wasia Chanzo cha Migogoro Katika Jamii na Familia.- TAWLA

Mratibu wa Chama cha Wanasheria Wanawake Mkoani Tanga (TAWLA) Wakili Latifa Ayoub akisisitiza jambo wakati wa mafunzo kwa wasaidizi wa Kisheria wa wilaya za Tanga ,Muheza na Pangani yaliyofanyika Jijini Tanga.
Mwanasheria wa Chama cha cha Wanasheria Wanawake Mkoani Tanga (TAWLA) Mwanaidi Kombo akisisitiza jambo wakati wa mafunzo hayo 
Sehemu ya washiriki wakifuatilia mada mbalimbali kwenye mafunzo hayo 
Sehemu ya washiriki wakifuatilia mada mbalimbali kwenye mafunzo hayo 
Mmoja wa washiriki wa Mafunzo hayo Michael Guni akiuliza swali wakati wa mafunzo kwa wasaidizi wa Kisheria wa wilaya za Tanga ,Muheza na Pangani yaliyofanyika Jijini Tanga.


KUTOKUANDIKWA wosia kwa baadhi ya jamii mkoani Tanga kumetajwa kuwa ndio chanzo kikubwa cha migogoro mingi ambayo imepelekea mipasuko ambayo inachangia familia nyingi kutengana kutokana na kugombania mali imeelezwa

Hayo yalisemwa na Mratibu wa Chama cha Wanasheria Wanawake Mkoani Tanga (TAWLA) Wakili Latifa Ayoub wakati wa mafunzo kwa wasaidizi wa Kisheria wa wilaya za Tanga ,Muheza na Pangani .

Mafunzo hayo yalilenga juu ya upatikanaji wa haki kwa wanawake katika kumiliki kupata na kutumia ardhi na uelewa juu ya sheria ya utoaji wa msaada wa kisheria kwa wasaidizi hao jana yaliyoratibiwa na chama hicho.

Kwa mujibu wa mratibu huyo alisema uandikaji wa wosia ni mzuri kutokana na kwamba umekuwa ukipunguza migogoro ndani ya familia wakati aliyekuwa akimilika mali husika anapofariki dunia iwapo utaandikwa kihalali.

“Kutokana na kuonekana kuwepo kwa changamoto hii ya uandikaji wosia jamii sisi kama Tawla tulianza kuandika wosia tokea mwaka 2007 lengo kubwa likiwa ni kupunguza migogoro mikubwa pindi mtu anapokuwa akiondoka duniani”Alisema.

Aidha alisema tokea walipoanza kufanya hivyo mpaka sasa wamekwisha kuandika wosia kwa watu 10 lakini bado wanaendelea na suala hilo hivyo jamii inaweza kuchangamkia fursa hiyo iwapo itaaona kuna umuhimu wa kuandika

“Lakini hapa cha muhimu kuandika ni kuwapatia elimu jamii waweze kujua kuandika changamoto ni wanaotaka kufanya hivyo ni wazee wakati mwengine hawafiki ofisini na hivyo kuhitaji kufuatwa”Alisema

Pia alisema bado mwamko ni mdogo sana kwa watu kuandikia wosia jambo ambalo wakati mwengine linachangiwa na imani za dini kwa baadhi ya watu huku wengine kutokuwa na uelewa.

Alieleza wanashindwa kuelewa mali mbalimbali wanazomilika ikiwemo baiskeli ,shamba na nyumbazote hizo ni mali ambazo mtu anaweza kuandika wosia ikiwa anafariki dunia ili wahusika wanaobakia kuepukana na migogoro.

“Kutokana na kuwepo kwa mwamko huo mdogo sasa tutalazimika kuendelea kutoa elimu kueleza namna ya waweze kuandika wosia kwa lengo la kuepusha mipasuko na mifarakano kwenye jamii hususani mwenye mali anapofariki dunia “Alisema Mratibu huyo Wakili Latifa.

Awali akizungumza wakati wa Mafunzo hayo mmoja wa washiriki Michael Guni alisema mafunzo hayo yamewapa mwanga kuweza kutekeleza wajibu wao wa kila siku katika utoaji wa haki hususani kwa wanawake katika kupata na kumiliki Ardhi.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.