Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dk. Ali Mohamed Shein, Mkuu wa Mkoa wa Mjini Magharibi Unguja Mhe. Ayoub Mohammed Mahmoud, wakimsikiliza Daktari Dhamana wa Manispa ya Wilaya ya Magharib i BM, Unguja Dk.Rahma Abdallah Maisara, akitowa maelezo ya picha za Kituo cha Afya cha Magirisi baada ya kuweka Jiwe la Msingi Wilaya ya Magharibi Unguja.wakati wa ziara yake leo.
Na.Abdi Shamnah.Ikulu Zanzibar.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk
Shein aliendelea na ziara yake kwa uwekaji wa Jiwe la msingi wa Kituo cha Afya
Magirisi, Wilaya ya Magharibi ‘B’ Unguja.
Akizungumza
na wananchi Dk. Shein alisema ujenzi wa kituo hicho cha Afya ni jambo la faraja
kwa wananachi wa Jimbo la Kijitoupele, akiwashukuru viongozi wa jimbo hilo kwa
uamuzi wao wa busara.
Alisema
Ilani za Uchaguzi za Chama cya ASP za mwaka 1961 na 1965 ziliweka bayana azma
ya Serikali kutowa huduma za Afya bila malipo, jambo ambalo Serikali ya
Mapinduzi inaliendeleza.
Alisema
Mapinduzi ya 1964 yameleta mabadiliko makubwa katika sekta ya Afya na elimu, mbali na kuwepo kwa changamoto ya
ongezeko la watu hapa nchini.
Akinasibishana kauli hilo, Dk. Shein alisema kituo hicho kina
uwezo wa kutoa huduma kwa wastani wa watu 15,000 pekee hivyo hakitoshelezi mahitaji
kwa kuzingatia wananchi 93,119
wanaotarajiwa kukitumia.
Aliishukuru
taasisi ya Direct AID kutoka Kuwait kwa kuunga mkono juhudi za viongozi wa jimbo
hilo baada ya kukubali kukamilisha hatua iliypobaki ya ujenzi.
Alisema
kituo hicho kitakapokamilika kitaweza kutoa elimu ya kinga ya maradhi mbali
mbali na kubainisha wazi upatikanaji wa uhakika wa dawa, kutokana na juhudi za
Serikali za kuimarisha bajeti ya Wizara ya Afya katika mwaka wa fedha
unaoendelea.
Alisema
katika mwaka wa fedha wa 2018/19 Serikali imetenga kiasi cha shilingi Bilioni
12.7 kwa ajili ya kuimarisha huduma za
Afya, hususan katika suala zima la upatikanaji wa dawa, akibainisha huduma zote
muhimu ikiwemo uchunguzi wa magonjwa mbali mbali kupatikana bure.
Dk.
Shein aliiagiza Wizara ya Afya kujiandaa vyema, ili pale kituo hicho
kitakapofunguliwa kiwe na waataalamu na wafanyakazi wanaotosheleza ili kutoa
huduma bora kwa wananchi.
Nae,
Mkuu wa Wilaya ya Maghribi “B” Kepteni Silima Haji Haji alisema ujenzi wa kituo
hicho kwa kiasi kikubwa kutavipungumzia mzigo vituo vyengine , ikiwemo kituo
cha Afya Mwera katika kutoa huduma za Afya.
Mapema,
Waziri wa Nchi (OR)Tawala za Mikoa, Serikali za Mitaaa, Idara maalum na Vikosi
vya SMZ, Haji Omar Kheir alisema Wizara hiyo kwa kushirikiana na Wizara Afya
itajenga uzio pamoja na kukipatia wataalamu an wafanyakazi kituo hicho.
Aliipongeza
taasisi ya Direct Aid kwa kuendelea kutoa misaada ya kijamii kwa wananchi wa Jimbo la Kijitoupele baada ya
kufanikisha ujenzi wa kisima.
Nae,
Mkurugenzi wa Baraza la Manispaa Magharibi “B” Ali Abdalla Said alisema ujenzi
wa kituio hicho umegharimu zaidi ya shilingi Milioni 90 ambapo miongoni mwa
fedha hizo zinatoka Halmashauri na mfuko
wa Jimbo kupitia Mbunge na Mwakilishi wa Jimbo la Kijitoupele.
Alisema
ni matarajio ya kituo hicho pale kitakapokamilika kuweza kutoa huduma bora za
afya kwa wananchi wapatao 93,119.
No comments:
Post a Comment