Tunapenda kuwafahamisha waombaji mikopo ya elimu ya
juu kwa mwaka wa masomo 2019/2020 kuwa dirisha la
kuomba mkopo kwa njia ya mtandao litafunguliwa
rasmi Jumatatu, Julai 1, 2019 na kufungwa Alhamisi,
Agosti 15, 2019. Maombi yote yatafanywa kupitia mtandao
utakaopatikana kupitia www.heslb.go.tz.
Kati ya leo (Jumanne, Juni 25) na Julai 1, 2019 wakati
dirisha litakapofunguliwa, wanafunzi wanashauriwa
kuhakikisha wanakamilisha nyaraka muhimu zinazotajwa
katika‘Mwongozo wa Utoaji Mikopo na Ruzuku kwa
2019/2020’ unaopatikana katika tovuti ya HESLB
Nyaraka hizo na maelezo mengine ya ufafanuzi pia
yanapatikana katika kitabu kidogo cha ‘Maswali na
Majibu 26’ kuhusu uombaji mkopo kinachopatikana katika tovuti hiyohiyo.
Kwa ajili ya kumbukumbu, nyaraka muhimu ni pamoja na:
i. Nakala ya cheti cha kuzaliwa cha mwombaji wa
mkopo iliyothibitishwa na Wakala wa Usajili, Ufilisi
na Udhamini (RITA) au Wakala wa Usajili wa
Matukio ya Kijamii Zanzibar (ZCSRA);
ii. Nakala ya cheti cha kifo cha mzazi wa mwombaji mkopo iliyothibitishwa na Wakala wa Usajili, Ufilisi
na Udhamini (RITA) au Wakala wa Usajili wa
Matukio ya Kijamii Zanzibar (ZCSRA);
iii. Barua ya Mganga Mkuu wa Mkoa (RMO), Mganga Mkuu wa Wilaya (DMO) au Mganga wa
Hospitali ya Halmashauri ya Mji, Wilaya, Manispaa
au Jiji inayothibitisha ulemavu wa mwombaji
mkopo au mzazi wake; na
iv. Barua kutoka kwa taasisi iliyofadhili masomo ya sekondari au stashahada ya mwombaji mkopo.
Ufafanuzi kwa wanafunzi waliomaliza
kidato cha sita na stashahada mwaka huu
Baada ya wanafunzi waliomaliza kidato cha sita au
stashahada (diploma) wamekuwa wakiuliza maswali kadhaa
kuhusu utaratibu wa ujazaji wa fomu za uombaji mkopo
wakiwa katika kambi za Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) na
iwapo wanaweza kujaza fomu kabla matokeo ya mitihani
hayajatoka.
Ufafanuzi ni kuwa HESLB inawasiliana na Makao Makuu ya
JKT ili kuweka utaratibu bora kuwawezesha wanafunzi
wahitaji waliopo katika kambi za JKT kuwasilisha maombi
kwa njia ya mtandao.
Aidha, mfumo wa uombaji mikopo kwa njia ya mtandao
utakaofunguliwa Julai 1 mwaka huu haumlazimishi
mwombaji kuwa na matokeo ya kidato cha sita. Mwombaji
atapaswa kuwa na namba ya mtihani wake wa kidato cha nne
tu.
Wito
Waombaji wa mikopo watarajiwa wanashauriwa kusoma
mwongozo uliotolewa na kuandaa nyaraka zote muhimu
zinazohitajika kuthibitisha uhitaji wao kabla ya kuingia
katika mfumo wa uombaji. Uzoefu unaonesha kuwa
mwombaji mkopo anaweza kutumia dakika 30 kukamilisha
maombi yake katika mfumo ikiwa ana nyaraka zote muhimu.
Imetolewa na:
Mkurugenzi Mtendaji,
Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu,
Dar es salaam
Jumanne, Juni 25, 2019
No comments:
Post a Comment