Habari za Punde

Tawi la Simba Cream Tanga Watoa Msaada Kituo Cha Watoto Yatima Raskazone Cha Casafamilia Rossete.

KATIBU Msaidizi wa Tawi la Simba Cream la Jijini Tanga Edgar Mdime ambaye pia ni Mweka Hazina kulia akimkabidhi biskuti mtoto Huchirachi Ally leo anayelelewa kwenye kituo cha Kulea watoto yatima cha Casafamilia Rosetta Centre kilichopo Raskazone Jijini Tanga wakati wapenzi na wanachama wa Simba Jijini Tanga walipokwenda kutoa misaada kwenye kituo hicho ikiwa ni maadhimisho ya wiki ya simba
KATIBU Msaidizi wa Tawi la Simba Cream la Jijini Tanga Edgar Mdime ambaye pia ni Mweka Hazina kulia akimkabidhi biskuti mtoto Huchirachi Ally leo anayelelewa kwenye kituo cha Kulea watoto yatima cha Casafamilia Rosetta Centre kilichopo Raskazone Jijini Tanga wakati wapenzi na wanachama wa Simba Jijini Tanga walipokwenda kutoa misaada kwenye kituo hicho ikiwa ni maadhimisho ya wiki ya simba
KATIBU Msaidizi wa Tawi la Simba Cream la Jijini Tanga Edgar Mdime ambaye pia ni Mweka Hazina kulia akimkabidhi msaada wa vitu mbalimbali Mkurugenzi wa MKURUGENZI wa Kituo hicho Irine Kaoneka

 Sehemu ya wana Simba
 Sehemu ya wana Simba wakiwa wamebabe vitu mbalimbali baada ya kufika kwenye kituo hicho
 KATIBU Msaidizi wa Tawi la Simba Cream la Jijini Tanga Edgar Mdime kushoto akiwa na Mwanachama mwenzie Bertha Mwambela wakiingia kwenye kituo hicho wakiwa na vitu mbalimbali
Sehemu ya vitu ambavyo vimekabidhiwa leo vikiwa vimetolewa


TAWI la Simba Cream la Jijini Tanga leo wamekabidhi misaada ya viti mbalimbali kwenye kituo cha Kulea watoto yatima cha Casafamilia Rosseta ikiwa ni kuelekea kilele cha siku ya Simba maarufu kama Simba Day.

Hafla ya makabidhiano ya msaada wa vitu ulifanywa na katibu Msaidizi wa tawi la Simba Cream Edgar Mdime kwa Mkurugenzi wa Kituo hicho Irine Kaoneka

Akizungumza mara baada ya kupokea msaada huo MKURUGENZI wa Kituo hicho Irine Kaoneka amesema kwamba wamekuwa wakiiombea kila mara klabu ya Simba iweze kufanya makubwa kwenye soka hapa nchini na nje ya mipaka ya Tanzania.

Alisema kwamba wamefurahishwa na ugeni huo kutoka Simba Tanga kwani wamefanya jambo jema bibilia inasema ibada njema ni iliyosafi kusaidia jamii inayokuwa ikihitaji mahitaji mbalimbali

“Hivyo kwa hili Simba Cream hapa mmefanya ibada njema na sisi tutaendelea kuiombea Simba kila wakati ili iweze kupata mafanikio makubwa pamoja na kuendelea kuiwakilisha nchi kwenye mashindano makubwa “Alisema

Awali akizungumza wakati wa makabidhiano hayo Katibu Msaidizi wa Tawi la Simba Cream la Jijini Tanga alisema kwamba wameamua kukabidhi msaada huo ili kurejesha shukrani kwa jamii

“Leo hii tumekabidhi msaada huu tunaamini kwamba utakuwa chachu kwenye kituo hiki lakini pia niwatumie salamu watani wetu wa Jadi Yanga wajipange kwani msimu ujao hawatasalimika na kipigo kutoka kwa Mnyama “Alisema

Mdime ambaye pia ni Mweka Hazina alisema pia utaratibu huu wa Simba Day umekuwa ukifanyika kwa kipindi cha miaka 10 sasa kwa kutoa misaada mbalimbali kwa watoto yatima na kuwafariji wagonjwa .

Alisema wameandaa Coaster na wanachama 33 wataondoka kuelekea dar kwa ajili ya kushuhudia Simba day wamejipanga wapo vizuri na hawana presha.

Hata hivyo alisema kutokana na uwepo kwa kikosi kipana ndani ya timu hiyo hakuna mtu ambaye wanaweza kumuogopa wala kushindana nao isipokuwa TP Mazembe.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.