Habari za Punde

Balozi Sief awasili Lindi kuhudhuria kilele cha sherehe za Mwenge wa Uhuru

 Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi akipokewa na Mkuu wa Mkoa Lindi Mh. Godfrey Zambi aliposhuka katika Uwanja wa Ndege wa Mkoa huo kuhudhuria Sherehe za kilele cha mbio za Mwenge wa Uhuru.
Kati kati yao ni Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Kazi,Ajira, na Watu wenye Ulemavu Mh. Jenista Joaquim Mhagama.
  Balozi Seif akisalimiana na Makamanda wa Vikosi vya Ulinzi na Usalama waliowasili kumpokea Uwanja wa Ndege wa Mkoa wa Lindi kuhudhuria Sherehe za kilele cha mbio za Mwenge wa Uhuru zilizofanyika katika Uwanja wa Ilulu.
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi akisalimiana na Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi Dr. Bashiru Ali alipofika Uwanja wa Ilulu Mkoani Lindi kuhudhuria Sherehe za kilele cha mbio za Mwenge wa Uhuru.
Kati kati yao ni Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Tanzania Dr. Harrison Mwakyembe.
Picha na – OMPR – ZNZ.


No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.