Mtendaji Mkuu wa Mahkama Zanzibar Kai Bashir Mbaruk kulia akitiliana saini na Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Advent Construction ltd Mkataba wa Ujenzi wa Mahkama Kuu Tunguu Mkoa Kusini Ungja. .hafla iliofanyika katika ukumbi wa Mahkama Kuu Vuga Zanzibar
Mtendaji Mkuu wa Mahkama Zanzibar Kai Bashir Mbaruk kulia wakibadilishana hati ya saini na Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Advent Construction ltd Mkataba wa Ujenzi wa Mahkama Kuu Tunguu Mkoa Kusini Ungja.hafla iliofanyika katika ukumbi wa Mahkama Kuu Vuga Zanzibar.
Waziri wa Katiba na Sheria Khamis Juma Maalim akitoa hotuba katika hafla ya utiliaji saini Mkataba wa Ujenzi wa Mahkama Kuu Tunguu Mkoa Kusini Unguja.ambayo itakayojengwa na Kampuni ya Advent Construction ltd hafla iliofanyika katika ukumbi wa Mahkama Kuu Vuga Zanzibar.
Rahma Khamis na Mwashungi Tahir Maelezo.
Mtendaji Mkuu wa Mahkama Zanzibar Kai Bashir Mbaruk kulia wakibadilishana hati ya saini na Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Advent Construction ltd Mkataba wa Ujenzi wa Mahkama Kuu Tunguu Mkoa Kusini Ungja.hafla iliofanyika katika ukumbi wa Mahkama Kuu Vuga Zanzibar.
Waziri wa Katiba na Sheria Khamis Juma Maalim akitoa hotuba katika hafla ya utiliaji saini Mkataba wa Ujenzi wa Mahkama Kuu Tunguu Mkoa Kusini Unguja.ambayo itakayojengwa na Kampuni ya Advent Construction ltd hafla iliofanyika katika ukumbi wa Mahkama Kuu Vuga Zanzibar.
Jaji Mkuu wa Zanzibar Omar Othman Makungu akitoa hotuba katika hafla ya utiliaji saini Mkataba wa Ujenzi wa Mahkama Kuu Tunguu Mkoa Kusini Unguja.ambayo itakayojengwa na Kampuni ya Advent Construction ltd hafla iliofanyika katika ukumbi wa Mahkama Kuu Vuga Zanzibar.
PICHA NA YUSSUF SIMAI/MAELEZO ZANZIBAR.
Rahma Khamis na Mwashungi Tahir Maelezo.
Ameyasema hayo huko Mahakama Kuu Vuga wakati alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya ghafla ya kutiliana saini na Kampuni ya Advent Construction ambayo inayotarajia kujenga Mahakama mpya Tunguu Mkoa wa Kusini Unguja .
Amesema kitendo cha kusaini mkataba huo ni muhimu sana ikiwa ni Utekelezaji wa Ilani ya Chama Cha Mapinduzi ikiwemo kusimamia na kuimarisha haki ili wananchi wapate haki za kusimamia kesi zao.
Amewataka kujenga jengo lenye ubora na kukamilisha kwa muda uliopangwa ili wawe na jengo la kisasa na waweze kufanya kazi zao kwa ufanisi na kupata Mahkama iliyo nzuri Zanzibar ambapo inatarajiwa kumalizika hapo mwakani kabla ya Dkt Shein kumaliza uongozi wake ikiwa ni miongoni mwa ahadi zake.
Pia amesema sheria ya msaada ishatungwa kwa lengo la kuandaa mazingira yaliyo mazuri kwa wananchi kupata haki zao kwa urahisi.
Hivyo amewaomba wakandarasi hao kujenga jengo lenye ubora na kiwango madhubuti ili liweze kudumu kwa muda mrefu na kutarajia likimaliza litasaidia Serikali katika utendaji wake.
“Tunaomba jengo hili lijengwe kwa kiwango kilicho bora ili kuweza kudumu kwa muda mrefu na kuepuka kujenga jengo bila ya kiwango” alisema Waziri huyo.
Nae Jaji Mkuu Omar Othman Makungu amewataka wakandarasi hao kuhakikisha wanajenga Mahkama iliyo ya kupendeza ili na sie tuwe na Mahkama iliyo nzuri yenye sifa kwa Zanzibar na kufanya wafanyakazi kila kitendo kinapata sehemu ya kufanyia kazi kwa nafasi.
Tunaishukuru Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kwa kujiandaa kutujengea jengo la Mahkama mpya kwa lengo la kutuimarishia miundo mizuri ya utendaji wa kazi kwa kila sekta .
“Tunashukuru Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kwa kuweza kutaka kutujengea jengo hili kwani jengo hili sasa lishakuwa dogo halikidhi haja kwa wafanyakazi hivyo likimalizika huko tutaweza kufanya kazi zetu katika mazingira mazuri”, alisema Jaji huyo.
No comments:
Post a Comment