Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk. Ali Mohamed Shein, akizungumza na Uongozi wa Shirika la Utangazaji Zanzibar.(ZBC TV) mkutano uliofanyika ukumbi wa Kituo cha ZBC TV mnazi mmoja Zanzibar, kulia Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Utangazaji Zanzibar (ZBC) Ndg. Chande Omar na Katibu Mkuu Kiongozi na Katibu wa Baraza la Mapinduzi.Dkt. Abdulhamid Yahya Mzee.
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa
Baraza la Mapinduzi, Dk. Ali Mohamed Shein, ameeleze azma ya Serikali ya
kuliimarisha Shirika la Utangazaji Zanzibar (ZBC), pamoja na kuzingatia maslahi
mazuri ya wafanyakazi wake.
Dk. Shein amesema hayo wakati alipokutana na Uongozi na
wafanyakazi wa Shirika hilo, mkutano uliofanyika katika ukumbi wa Shirika hilo
uliopo Mnazimmoja mjini hapa.
Alisema ZBC ni shirika jipya lililoundwa miaka sita iliyopita,
hivyo aliwataka wafanyakazi kufahamu ulazima wa kuwepo kwa changamoto mbali
mbali katika kipindi hiki kuelekea hatua
ya mafanikio.
Alisema Serikali imelazimika kutumia fedha nyingi katika
uundaji wa Shirika hilo na kulipatia mitambo mipya ili liweze kuondokana na
matumizi ya mfumo wa Analojia kuelekea ule wa Digitali.
“Kuunda Shirika sio jambo dogo ni jambo linalohitaji fedha
nyingi sana ilikuwa lazima tuunde na kufanyakazi, miaka sita haitoshi kupata
chombo madhubuti”, alisema.
Aidha, alisema kuna umuhimu kwa shirika hilo kujiendesha
wenyewe, jambo alilobainisha kuwa bado halijafanikiwa kwa kuwa linategemea
ruzuku kutoka Serikalini.
Alieleza kuwa Wizara ya Habari, Utalii na mambo ya Kale ina dhima ya kuongoza
kuelekea mabadiliko ya shirika hilo, akibainisha umuhimu wa kuwepo mipango ya
jumla kwa ajili ya ZBC ya kesho, huku akisitiza kuwa jambo hilo sio la mkato.
Dk. Shein alilitaka Shirika hilo kupitia Wizara kuainisha vipaumbele
katika bajeti yake, kulingana na mahitaji yaliopo na kusisistiza azma ya
serikali ya kuliendeleza shirika hilo kwa kulipatia vifaa vyote
vinavyohitajika,
“Kupanga na kuchaguwa ni lazima muainishe mambo gani ya msingi
mnataka kununuwa”, alisema.
Alieleza kuwa Serikali ina nia njema ya kuliendeleza shirika
hilo ili lifanane na mashirika mbali mbali duniani, na ndio maana juhudi mbali
mbali zimekuwa zikichukuliwa kuliimarisha.
Alisema muundo wa Shirika hilo unapaswa kuwiana na ule wa Wizara
ili kuwepo mustakbali mwema katika uendeshaji wake,chini ya usimamizi wa Bodi
ya Shirika.
Aidha, alisistiza
mashirikiano, mapenzi na mshikamano katika utendaji wa kazi, huku akiwaaahidi
wafanayakazi hao kuimarishwa maslahi na
stahiki zao mbali mbali kupitia Bodi ya Shirika hilo.
Alisema ZBC ni sawa an televisheni nyengine Duniani
zinazomilikiwa na Seriklai na kubainisha tofauti iliyopo kati yake ni uwezo,
huku akielezea mwelekeo wa shirika hilo kwua wa mafanikio.
“Naithamini sana ZBC, nawathamini wafanyakazi, natamani
Serikali iwe na uwezo mkubwa tufanye yote, lakini nataka mtuamini tunataka
kuleta mabadiliko”, alisema.
Katika hatua nyengine Dk. Shein slisema ni umuhimu kuhakikisha
wafanyakazi wanaojitolea katika shirika hilo kwa kipindi kirefu kupatiwa ajira
kwa kuzingatia kuwa wametumia miaka mingi kulitumikia kwa ufanisi.
Ameutaka uongozi wa ZBC,
kuwasilisha Serikalini taarifa za wafanyakazi 16 ambao wamekuwepo katika
shirika hilo kwa kipindi cha kujitoleya , ili hatua za kuwapatia ajira ziweze
kuchukuliwa.
Alisema suala la ajira kwa wafanyakazi wanaojitolea ni la
kiutawala, ambapo tayari Serikali ililitoleya
muongozo muda mrefu uliiopita.
Dk. Shein alipongeza utaratibu ulioanzishwa na uongozi wa ZBC
kuwakutanisha pamoja Viongozi na wafanyakazi kila mwezi ili waweze kuwasilisha
matatizo yao kwa lengo la kuyapatia ufumbuzi.
Aliwataka wafanyaakzi kufanya juhudi kuvutia sekta ya Utalii
kwa kuutangaza katika vyombo vya habari (Tv na Redio), sambamba na kutaka
kuwepo mashirikano ya karibu na Uongozi wa Wizara husika.
Aidha, aliutaka Uongozi wa Shirika hilo kuweka mazingira bora
ya kuvutia wafanyakazi wao ili waweze
kuipenda kazi yao na kufanyakazi kwa bidii, huku akitowa pongezi kwa kazi
nzuri inayofanywa na wafanayakazi wa shirika hilo, kiasi cha kuvutia watazamaji
wengi.
Katika hatua nyengine, Dk. Shein alisema serikali itazingatia
kwa makini usalama wa wafanyakazi wa shriika hilo katika matukio makubwa,
ikiwemo wakati wa Uchaguzi mkuu.
Aliwataka wafanyakazi hao kufanyakazi zao kwa kuzingatia
maadili ya kazi za uandishi wa habari na kuondokana na utartibu wa kuegemea
upande mmoja pale inapoibuka hoja inayoyoihusus Serikali, ili kuepuka kuigawa.
Aidha, alisistiza
mashirikiano, mapenzi na mshikamano katika utendaji wa kazi, huku akiwaaahidi wafanayakazi hao kuimarishwa maslahi na stahiki zao mbali
mbali kupitia Bodi ya Shirika hilo.
“Naithamini sana ZBC, nawathamini wafanyakazi, natamani
Serikali iwe na uwezo mkubwa tufanye yote, lakini nataka mtuamini tunataka
kuleta mabadiliko”, alisema.
Mapema, Katibu wa Baraza la Mapinduzi na Katibu Mkuu Kiongozi,
Dk. Abdulhamid Yahya Mzee, alisema suala la ajira kwa wafanyakazi waliojitolea
siku nyingi, lina uwezekano mkubwa wa kupatikana ufumbuzi wake pale uongozi wa
shirika hilo utakapowasilisha serikalini taarifa na jinsi litakavyoweza
kuwalipa mishahara wafanyakazi hao.
“Kama kuna wafanyakazi wanajitolea na kama fedha zipo,
niandikieni mimi nitatowa kibali cha kuajiriwa”, alisema.
Aliutaka uongozi wa shirika hilo kujiendesha kwa kuzingatia
vipaumbele vinavyohitajika kwa ukufuata taratibu wa kuzishirikisha maeneo yote
ya kazi ya Shirika hilo.
Alisistiza umuhimu wa kuwepo mpango maalum wa mafunzo kwa
watumishi wa shirika hilo kwa mwaka, kuambatana na mahitaji halisi ya taasisi.
Akizungumzia maslahi ya wafanyakazi, Abdulhamid alisema serikali
imetowa muongozo kwa kila Shirika kuwa na daraja lake, akibainisha kuwa
mashrika yote yanayojitregemea tayari yameanza kutumia miongozo ya kimaslahi
yaliowekwa na serikali.
Kuhusiana na uendaji wa likizo ya kila mwaka kwa wafanyakazi,
alisema likizo ni haki ya mfanyakazi na kufafanua kuwa Posho la mazingira
magumu halina uhusiano na posho la malipo ya ziada ya kazi (over time), huku
akiwataka viongozi wa taasisi kuratibu vyema upatikanaji w ‘overtime’ili
kuepuka ujanja unaofanywa na baadhi ya wafanyaakazi wa kutega kazi ili kupata
posho hilo
Aliwataka wafanyakazi kuwa watundu katika kutafuta fursa za
masomo katika taasisi na vyuo mbali
mbali ndani na nje ya nchi.
Aidha, aliutaka uongozi wa Shirika hilo kuibuwa mahitaji ya
kitaalamu kupitia kada tofauti na kuyawasilisha Serikali ili yaweze
kuwasilishwa katika Idara ya Elimu ya juu kwa utekelezaji.
Dk. Abdulhamid aliitaka Menejment ya ZBC kulipatia ufumbuzi
suala la usafiri wa wafanyakazi ili waweze kuondokana na kadhia ya kukosa
usafiri wa kuwafikisha na kuwarudisha kazini , hatua aliyosema itawajengea
heshima na kuwahakikishia usalama wao.
Aliikumbusha Idara ya Habari na Maelezo wajibu wa kuwataka
Mawaziri kutekeleza muongozo wa kutoa taarifa za utekelezaji wa Wizara zao kila
baada ya miezi mitatu, sambamba na kusisitiza umuhimu wa waandishi wa habari
kutafuta habari na kuondokana na urasimu wakati huu wa ushindani.
Aidha, alieleza umuhimu wa wafanyakazi wa Shirika hilo
kufanyakazi kwa mashirkiano na kuweka utaifa mbele kwa kufuata sera na miongozo
ya Serikali na sheria za Utumishi wa umma pamoja na kuondokana na makundi.
Nae, Waziri wa Habari, Utalii na Mmabo ya Kale, Mahamoud
Thabiti Kombo alisema atasimamia kikamilifu kuhakikisha wafanyaakzi wanaojitolea
kipindi kirefu wanaajiriwa awamu kwa awamu pamoja na wale wenye ulemavu.
Aidha, alisema kuna mashirikiano ya kutosha kati ya Uongozi wa
Wizara hiyo na wafanyakazi wa ZBC, sambamba na kuuutaka uongozi wa Shirika hilo
kufanya juhudi kuendeleza ushirikiano uliopo kati yake na Kampuni ya Azam
TV kwa maslahi ya wafanyakazi,Shirika na
Taifa kwa ujumla.
Aidha, Mkurugenzi Mkuu wa ZBC Chande Omar, aliahidi kufanya
juhudi kuzipatia ufumbuzi changamoto mbali mbali zinazolikabili Shirika hilo,
ikiwemo suala la ajira , mafunzo na usafiri.
Alisema suala la mafunzo linakwenda kwa kasi kubwa,
akibainisha hatua mbali mbali zinazochukuliwa kulingana na Bajeti iliyopo.
Alisema kuna mwamko mkubwa kwa wafanyakazi kupenda kusoma,
hivyo Uongozi wa ZBC unafanya juhudi ya kuwapatia fursa za mafunzo katika taasisi
mbali mbali nchini pamoja na kupokea wataalamu kutoka nje ya nchi kuendesha
mafunzo mbalimbali, ikiwemo uzalishaji wa vipindi.
Katika mkutano huo,
ambapo pia uliwashirikia viongozi mbali mbali wa serikali, ikiwemo Washauri wa
Rais, wafanyakazi
walipata fursa ya kutoa maoni, mapendekezo na ushauri kwa Rais wa Zanzibar na
Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein katika maeneo mbali
mbali, ikiwemo ajira, mafunzo, usafiri, usalama na usafiri.
Abdi Shamna, Ikulu Zanzibar
Postal Address: 2422 Tel.:0777476982. Fax: 024 2231822
E-mail:
abdya062@gmail.com
No comments:
Post a Comment