Habari za Punde

RC MAKONDA AWAAPISHA WAJUMBE WA BARAZA LA ARDHI NA NYUMBA WILAYA YA KINONDONI NA TEMEKE

Na.K-VIS BLOG

MKUU wa Mkoa wa Dar es Salaam, Mhe. Paul Makonda, leo Novemba 23, 2019 amewaapisha Wajumbe wa Baraza la Ardhi na Nyumba wa Wilaya ya Kinondoni na Temeke.
Kwa upande wa Wilaya ya Kionondoni, walioapishwa ni pamoja na Bw. Derek Murusuri, Balozi Celestine Christopher Liundi na Mama Merina Mlunde.
Aidha Mheshimiwa Makonda pia aliwaapisha wajumbe wengine wane wa Wilaya ya Temeke.
 Akitoa nasaha zake baada ya zoezi hilo, Mkuu wa Mkoa Mhe.  Makonda aliwataka Wajumbe hao kuwa sehemu ya utatuzi wa migogoro na sio kuichochea.
Aliwataka Wajumbe hao kutumia mbinu zote kutatua migogoro ya ardhi ili mashauri yasiwe yanachukua muda mrefu.
"Muwe msaada kwa watu wote na hasa wanyonge, wajane na yatima ili wapate haki yap," alisisitiza.
 Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Mhe. Paul Makonda (kulia), akimuapisha Bw. Derek Murusuri kuwa Mjumbe wa Baraza la Ardhi na Nyumba wa Wilaya ya Kinondoni. 


Na.K-VIS BLOG
MKUU wa Mkoa wa Dar es Salaam, Mhe. Paul Makonda, leo Novemba 23, 2019 amewaapisha Wajumbe wa Baraza la Ardhi na Nyumba wa Wilaya ya Kinondoni na Temeke.
Kwa upande wa Wilaya ya Kionondoni, walioapishwa ni pamoja na Bw. Derek Murusuri, Balozi Celestine Christopher Liundi na Mama Merina Mlunde.
Aidha Mheshimiwa Makonda pia aliwaapisha wajumbe wengine wane wa Wilaya ya Temeke.
 Akitoa nasaha zake baada ya zoezi hilo, Mkuu wa Mkoa Mhe.  Makonda aliwataka Wajumbe hao kuwa sehemu ya utatuzi wa migogoro na sio kuichochea.
Aliwataka Wajumbe hao kutumia mbinu zote kutatua migogoro ya ardhi ili mashauri yasiwe yanachukua muda mrefu.

"Muwe msaada kwa watu wote na hasa wanyonge, wajane na yatima ili wapate haki yap," alisisitiza.
 Mhe. Makonda akimkabidhi kitendea kazi Bw. Murusuri mara baada ya kumuapisha.
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Mhe. Paul makonda (katikati) na Katibu Tawala wa Mkoa wa Dar es Salaam Bw.Abubakar Kunenge (wapili kushoto), wakiwa kwenye picha ya pamoja na wajumbe hao baada ya kuwaapisha.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.