Habari za Punde

Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Dkt. John Magufuli Afungua Jengo la Mahkama ya Wilaya ya Chato Pamoja na Kuzindua Ujenzi wa Kituo Cha Jeshi la Zimamoto na Uokozi Cha Wilaya ya Chato Mkoani Geita

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akivuta utepe pamoja na Jaji Mkuu wa Tanzania Profesa Ibrahim Juma, Spika wa Bunge Job Ndugai pamoja na Waziri wa Katiba na Sheria Balozi Agustine Mahiga kuashiria ufunguzi wa Jengo la Mahakama ya Wilaya ya Chato mkoani Geita. 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akimpongeza Jaji Mkuu wa Tanzania Profesa Ibrahim Juma mara baada ya kufungua jengo la Mahakama ya Wilaya ya Chato lililopo Mlimani Chato mkoani Geita.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiwapungia mkono wananchi wa Chato (hawaonekani pichani) wakati akiwasili katika viwanja vya Mahakama ya Wilaya ya Chato mkoani Geita. Kulia ni Jaji Mkuu wa Tanzania Profesa Ibrahim Juma.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akikagua eneo la Mapokezi katika jengo jipya la Mahakama ya Wilaya ya Chato lililopo eneo la Mlimani Chato mkoani Geita mara baada ya kulifungua.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiwapungia mkono wananchi wa Chato mara ya kufungua jengo la Mahakama la Wilaya ya Chato. 
Moja ya Vyumba vya Mahakama hiyo ya Wilaya ya Chato kama inavyoonekana pichani.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akivuta utepe kuashiria uwekaji wa Jiwe la Msingi mradi wa ujenzi wa Kituo cha Jeshi  la Zimamoto la Wilaya ya Chato mkoani Geita.

Sehemu ya Jengo la Kituo cha Jeshi la Zimamoto na Uokoaji cha Wilaya ya Chato kilichowekewa Jiwe la Msingi leo na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli. 
Picha na Ikulu.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.