Habari za Punde

Mapinduzi Matukufu ya Januri 12, 1964 Ili Kuleta Usawa na Umoja Sambamba na Kuwafanya Waafrika Waishi Maisha Bora. -Dk.Shein.


Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk. Ali Mohamed Shein akiondia kipazia kuashiria kuweka Jiwe la Msingi la Jengo la Michezani Mall Jijini Zanzibar (kushoto kwa Rais) Waziri wa Fedha na Mipango Zanzibar Mhe.Balozi Mohammed Ramia Abdiwawa, hafla hiyo imefanyika katika eneo hilo michezani, ikiwa ni shamrashamra za kusherehekea Miaka 56 ya Mapinduzi ya Zanzibar. 


RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein amesema kuwa kulikuwa kuna kila sababu ya kufanyika Mapinduzi matukufu ya Januri 12, 1964 ili kuleta usawa na umoja sambamba na kuwafanya Waafrika waishi maisha bora.

Rais Dk. Shein aliyasema hayo leo katika hotuba yake aliyoitoa katika hafla ya uwekaji wa mawe ya msingi ya Michenzani Mall na jengo la Sheikh Thabit Kombo, hafla iliyofanyika katika viwanja vya Mapinduzi Square, Michezani Mjini Zanzibar ikiwa ni shamrashamra za sherehe za miaka 56 ya Mapinduzi ya Januari 12, 1964.

Alisema kuwa Mapinduzi yameleta usawa, umoja, udugu na maelewano na kubwa zaidi ni kuondosha ubaguzi wa aina zote na kuwafanya watu wawe wamoja sambamba na kutandika mipango mipya ya maendeleo.

Rais Dk. Shein alisema kuwa Zanzibar inayoonekana leo na ile ya miaka 60 iliyopita ni tofauti na hivi sasa kuna Zanzibar mpya iliyozaliwa Januari 12, 1964.

Akieleza historia ya Zanzibar, Rais Dk. Shein alisema kuwa wazee walipata madhila na hawakuwa na maisha mazuri kama ilivyo hivi sasa na kuwataka Wazanzibari kutosahau historia yao ikiwa ni pamoja na kujua walikotoka, walipo na wanakokwenda.

Rais Dk. Shein alitumia fursa hiyo kueleza historia ya mji wa Zanzibar na mipaka yake kabla ya Mapinduzi matukufu ya Januari 12, 1964 na jinsi Waafrika walivyokuwa wakiishi katika nyumba zisizostahiki kuishi binaadamu.

Katika historia hiyo, alisema kuwa lazima historia ielezwe kwa watoto, wajukuu, virembwe na vinyinginya hasa ikizingatiwa kuwa kabla ya Mapinduzi Mwafrika alikuwa hana haki ya kufanya jambo lolote la maendeleo hata kustarehe nchini mwake.

Alisema kuwa hatua hiyo ndio iliyopekekea mapambano ya miaka saba katika kupigania uhuru wa Mwafrika hapa Zanzibar na hatimae kufanywa kwa Mapinduzi matukufu ya Januari 12, 2964.

Alisema kuwa ni jambo la simanzi kwa wale wanaokebehi Mapinduzi kwani Mapinduzi yamefanyika nchi nyingi  duniani ikiwemo Ufaransa,  Marekani, Cuba, Misri, China na nyenginezo kwa lengo la kuondoa dhulma.

Aidha, Rais Dk. Shein alisema kuwa Mapinduzi yalikuwa ni lazima yafanyike hapa Zanzibar ili wananchi waishi katika mazingira mazuri na kuondokana na dhulma zilizokuwepo wakati huo kabla ya Mapinduzi ili kuleta usawa na umoja.

Rais Dk. Shein alitumia fursa hiyo kuieleza Sheria ya mwanzo Sheria namba 6, ambayo ilisisitiza umoja, amani, maridhiano sambamba na kuishi pamoja kwani hayo ndio malengo ya Mapinduzi.

Mapinduzi yamejenga umoja na maelewano kwa wananchi wa Zanzibar wakiwemo wa Unaguja na Pemba.

Alileza kuwa Michenzani ni kitovu na historia ya Mapinduzi na mambo yote wakati huo yalikuwa yakipatikana Michenzani hivyo, ni vyema historia hiyo ikaimarishwa.

Rais Dk. Shein alisema kuwa yeye hajazoea kuwadanganya wananchi kwani aliahidi kuwa atajenga Michezani Mall na ndivyo alivyofanya licha ya baadhi ya watu wachache kuibeza ahadi yake hiyo.

Alisema kuwa jengo la Thabit Kombo linatokana na historia ya muasisi huyo ambaye ameitumikia nchi na anahistoria kubwa ya Zanzibar sambamba na historia ya biashara na historia ya ASP na baadae CCM.

Alisema kuwa Awamu ya Saba imeamua kuendeleza historia yake kwa kujenga mji mpya wa Kwahani ambapo ujenzi umeanza tayari na Shirika la ZSSF limekuwa likiekeza kwa maelekezo ya Serikali.

Alisema kuwa wafanyabiashara waliohamishwa wawe ndio wa mwazo kwani wameipisha Serikali ikajenga hivyo ni lazima watekelezewe ahadi waliyoahidiwa  ili kuepuka kuja  kuwaudhi na kupelekea kuinunia Serikali yao.

Rais Dk. Shein alieleza mipamgo ya Serikali ya kujenga majengo zaidi sambamba na kujenga miji mengine midogo ukiwemo Chumbuni, Chwaka, Mkokotoni, Tunguu na mengineyo.

Alisema kuwa Serikali ina mpango wa kuanzisha Kampuni yake ya Ujenzi ili kuepusha gharama za ujenzi na kujenga majengo makubwa sambamba na kuweza kushindana na Kampuni nyengine.

Aliipongeza ZSSF na kueleza kuwa anaimani kwamba uongozi uliopo utafanya mambo mazuri zaidi ambapo pia, alitumia fursa hiyo kuipongeza Maskani Kaka ya MwembeKisonge kwa kukubali kiwanja chao kiwekezwe na ZSSF kwa lengo la kupata mafanikio.

Ameeleza kufurahishwa na mashirikiano mazuri yaliopo kati ya Maskani ya CCM ya Mwembekisonge na Shirika la ZSSF na kuwataka Wanamaskani wa maskani hiyo kuekeza vizuri na kuzitumia rasilimali hizo ili kuweza kupata tija.

Alisisitiza kuwa Zanzibar itaendelea kunawiri kwani Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar si Serikali ya wababaishaji kwani inatekeleza yale yote iliyowaahidi wananchi.

Alieleza kuwa ni jukumu la wananchi wote kuyalinda na kuyadumisha Mapinduzi matukufu ya Januari 12, 1964 kwani Mapinduzi ni mabadiliko ambayo yameondosha yake yote yaleyaliokuwa hayako sawa.

Alisemakuwa jukumu la wananchi mnikuyalinda na kuyaendeleza Mapinduzi kwani bado safari ya kuendelea kufanya vizuriinahitajika hsa kukiwa na lengo lakuwa kila Wizaya na Mkoa kuwa na Mall zake.

Rais Dk. Shein aliwaeleza wananchi kuwa ni matarajio iwapo mradi wa mafuta na gesi utakwenda vizuri Zanzibar itazidi kupata mafanikio zaidi ambapo mambo mengi yatafanikishwa.

Mapema Rais Dk. Shein aliweka mawe ya msingi katika jengo la Michenzani Mall na jengo la Sheikh Thabit Kombo liloopo Mwembekisonge na kuweza kupata maelezo juu ya ujenzi wa majengo hayo kutoka kwa Abdulazizi Ibrahim Idd Meneja Mipango, Uwekezaji na Utafiti wa ZSSF.

Nae Waziri wa Fedha na Mipango Balozi Mohammed Ramia Abdiwawa alisema kuwa eneo hilo lina historia yake katika vuguvugu la Mapinduzi ya Januari 12, 1964.

Aliongeza kuwa miradi hiyo miwili iliyowekewa mawe ya Msingi hivi le ni mimgoni mwa utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya CCM sambamba na utekelezaji wa  Dira ya 2020 ambapo matumaini yake kuwa kazi ya kukamilisha majengo hayo itakwenda vizuri na matarajio ni kuzinduliwa na Rais Dk. Shein.

Alisema kuwa ujenzi wa jengo la Sheikh Thabit Kombo limeonesha mashirikiano mazuri na jina la Sheikh Thabit Kombo limesibu huku akitumia fursa hiyo kusisitiza haja ya kuwaezi wazee na waasisi wa Mapinduzi matukufu ya Zanzibar.

Aliwataka wananchi wasiwe na wasiwasi juu ya miradi ya uwekezaji ya ZSSF kwani miradi yote inafanyiwa upembuzi wa kutosha kusisitiza kuwa Serikali itaendelea kuwawekeza mazingira mazuri wananchi wake.  

Nae Naibu Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar Abdalla Juma Sadalla Mabodi alitumia fursa hiyo kutoa salamu za pongezi kwa Rais Dk. Shein kwa uongozi wake mahiri na wenye mfano akiwa ni Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi pia, ni Makamo wa CCM Zanzibar.

Alisema kuwa umahiri wake wa kuiongoza Serikali unaonekana mpaka katika kukiongoza Chama hatua ambayo imepelekea maendeleo makubwa na uongozi uliotukuka sambamba na mashirikiano anayoyaonesha kati ya Serikali na CCM.

Alisema kuwa umuhimu wa maskani ya Mwembekisonge na Kachorora kwani ni maskani hizo zinahistoria yake hapa nchini.

Naibu Katibu Mkuu huyo alipongeza hatua zilizochukuliwa katika ushirikiano wa Chama na Serikali katika kuhakikisha maendeleo ya wananchi yanapatikana na kueleza kuwa wameanza kuonesha mfano kwani maskani hiyo imejengwa na ZSSF.

Alisema kuwa hivi sasa kuna mazungumzo juu ya uendeshaji wa eneo la chini na ghorofa ya kwanza kwa ajili ya CCM kwa lengo la kupata kipato hasa ikizingatiwa kuwa chama hicho kina mwelekeo katika ushindi wa chama hicho sambamba na kujiimarisha kiuchumi ili  chama kiweze kujiendesha wenyewe.

Nae Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mipango Khamis Mussa katika risala yake alisema kuwa ujenzi wa maduka hayo katika eneo la Michenzani ni miongoni mwa utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) ya mwaka 2015/2020 ambayo kwa Zanzibar, Rais Dk. Shein amekuwa akiitekeleza kwa vitendo.

Alieleza kuwa usanifu wa jengo la Michenzani Mall umefanywa na Kampuni ya ARQES AFRICA kutoka Dar –es Salaam na ujenzi wake unafanywa na Kampuni ya CRJE- East Africa pia ya Dar-es Salaam yenye asili ya China ambapo mkataba wa ujenzi huo ulisaniwa Oktoba 4, 2018 kwa gharama ya Bilioni 27.9 ikiwa ni pamoja na VAT.

Alieleza kuwa ujenzi wa maduka hayo utakuwa na urefu wa mita 35 na ghorofa 9 ambapo ghorofa ya hini ya ardhi atatumika kama ni ghala kwa ajili ya kuhifadhi bidhaa za wafanyabiashara wa jengo hilo na ghorofa ya chini itakayotumika kwa ajili ya huduma za benki na sehemu za maduka ya kufanya biashara.

Aidha, alisema kuanzia ghorofa ya tatu litagawika katika sehemu tau ambazo zinaanzia ghorofa ya tatu hadi saba ambapokutokana na mahitaji ya afisi yanayojitokeza kilasiku, sehemu mbili za duka hilo itakuwanisehemu za afisi.

Aliongeza kuwa sehemu ya katikati ambayo ina jumla ya ghorofa saba itakuwa na ukumbi wa mikutano, sherehe za harusi na sherehe nyenginezo wenye uwezo wwa kubeba hadi watu 500, sinema ya kisasa pamoja na sehemu ya kufanyia mazoezi (GYM).

Katibu Mkuu huyo alisema kuwa ujenzi huo umezingatia walemavu kwa kuwekwa “ramp” katika sehemu za kuingia katika jengo,vyoo maalum kwa ajili ya watu wenye mahitaji maalum pamoja na lift saba ambazo zinaweza kuwafikisha katika maeneo tofauti ya jengo.

Alisema kuwa kupitia jengo hilo la Michenzani Mall kwa upande wa ZSSF itakuwa wameitekeleza dhana ya Rais Dk. Shein kwa vitendo kwani kiasi cha sehemu 100 za biashara tofauti zitakuwepo kwani aliwahi kusema kwamba

“Sasa basi tena kufanya biashara mitaani, nataka biashara zishamiri katika maeneo maalum ya biashara, na hivi ndivyo katika nchi za wenzetu wanavyofanya”.

Alisema kuwa Mkandarasi aliahidi na kukubali kujenga kwa muda wa miezi 21 baada ya kukabidhiwa eneo na tayari ameshatumia muda wa miezi 15 tokea kuanza ujenzi.

Alisisitiza kuwa ASSF kwa kushirikiana na mshauri wa ujenzi watasimamia muda huo na kwa ujenzi wa kiwango kinachotakiwa ambapo Kampuni ya CRJE inajenga mradi huo kwa thamani ya TZS Bilioni 27.900 pamoja na VAT.

Kwa upande wa jengo la Sheikh Thabit Kombo alisema kuwa huo ni ubia kati ya Mfuko wa Hifadhi ya Jamii Zanzibar (ZSSF) na Chama Cha Mapinduzi (CCM) katika eneo la maskani ya MwembeKisonge kwa ajili ya mradi wa jengo la biashara lenye maduka, ofisi na kumbi za mikutano.

Alisema kuwa baada ya tathmini kufanyika Kampuni ya Group Six International Ltd YA Dar –es-Salaam ambayo ina asili ya China ilichaguliwa kwa kuwa ndio kampuni iliyowashinda wenzake kivigezo lakini ilichaguliwa kwa kuwa ndio yenye gharama ndogo za ujenzi kwa mradi huo kwa gharama ya TZS Bilioni 9.71.
alisema kuwa mradi huo utahusisha ujenzi wa ghorofa tano ikiwemo ghorofa ya chini ya ardhi itakayotumika kwa ajili ya maegesho ya gari, ghorofa ya chini na ya kwanza zitakazokuwa na maduka 40 ya biashara.

Aliongeza kuwa ghorofa ya pili na ya tatu ya jengo hilo la Sheikh Thabit Kombo zitakwua ni ofisi zitakazokodishwa kwa wananchi.

Alisema kuwa ujenzi huo hauhamishi maskani ya Mwembekisonge, maskani Kaka bali maskani itaendelea na shughuli zake kama kawaida ndani ya jengo katika ghorofa ya chini ilizopo mbele ya jengo upande wa barabarani.

Sambamba na hayo, katibu Mkuu huyoa lisema kuwa ZSSF hivi sasa imo katika hatua za kujenga jengo jengine la kuegesha gari kwa juu ambalo kwa Zanzibar litakuwa la kwanza ambalo linatarajiwa kujengwa pembezoni ya Michezani Mall na linaplenga kuondosha tatizo la maegesho  ya gari kwa watakaokuwa wakifika maeneo hayo.

Rajab Mkasaba, Ikulu Zanzibar
Postal Address: 2422 Tel.:0777427449. Fax: 024 2231822 

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.