STATE
HOUSE ZANZIBAR
OFFICE OF
THE PRESS SECRETARY
PRESS RELEASE
Zanzibar 12.01.2020

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.
Ali Mohamed Shein amepongeza Mtawala wa Ras-Al-Khaimah Sheikh Saud Bin Saqr Al Qasimi kwa kutuma
mjumbe aliyemwakilisha katika sherehe za miaka 56 ya Mapinduzi ya Zanzibar.
Rais Dk. Shein alipongeza ujio wa Bwana Mohamed Ali Musabeh Al Nuaimi
ambaye alifanya nae mazungumzo Ikulu ndogo Migombani na kusisitiza kuwa
Zanzibar inathamni uhusiano na ushirikiano uliopo kati yake na Ras Al Khaimah
na kusema kuwa ujumbe huo unathibitisha ukweli huo.
Katika mazungumzo hayo Rais Dk. Shein alimueleza kiongozi huyo kuwa
sherehe za Mapinduzi ya Zanzibar zimefana kwa kiasi kikubwa ambapo kabla ya
kilele hulitanguliwa na shamrashamra za uzinduzi wa miradi mbali mbali ya
maendeleo Unguja na Pemba.
Alieleza kuwa katika miaka 56 ya Mapinduzi ya Zanzibar maendeleo makubwa
yamefikiwa Unguja na Pemba huku akitumia fursa hiyo kuwaponegza wananchi wa
Zanzibar kwa kushiriki wka wingi katika kilele cha sherehe hizo zilizofanyika
huko katika uwanja wa Amaan jijini Zanzibar.
Nae Bwana Mohamed Ali Masabel Al Nuaimi alimpongeza Rais Dk. Shein pamoja
na wananchi wote wa Zanzibar kwa kusherehekea miaka 56 ya Mapinduzi matukufu ya
Zanzibar kwa aina yake na kutoa shukurani kwa mwaliko huo.
Kiongozi huyo alipongeza mapokezi makubwa aliyoyapata yeye na ujumbe wake
huku akitumia fursa hiyo kupongeza maendeleo makubwa yaliopatikana hapa
Zanzibar na kusisitiza kuwa Ras Al Khaimah itaendelea kuunga mkono juhudi hizo.
Katika mazungumzo hayo kiongozi huyo alimueleza Rais Dk. Shein kuwa
Mtawala wa Ras-Al-Khaimah Sheikh Saud Bin Saqr Al Qasimi anaungana na wananchi wote
wa Zanzibar katika kusherehekea miaka 56 ya Mapinduzi ya Zanzibar.
Kiongozi huyo alifuatana na Balozi wa Umoja wa Nchi za Falme za Kiarabu
(UAE) nchini Tanzania Khalifa
Abdulrahman Almarzooqi pamoja na Mkurugenzi Mtendaji wa RAK Gas Nishant Dighe.
Rajab
Mkasaba, Ikulu Zanzibar
Postal Address: 2422 Tel.:0777427449. Fax:
024 2231822
E-mail: rajabmkasaba@yahoo.co.uk
No comments:
Post a Comment