Habari za Punde

Wizara ya Vijana Utamaduni Sanaa na Michezo Yawasilisha Utekelezaji Mpango Kazi Kwa Mwezi wa Julai hadi Disemba 2019 /2020.

Waziri wa Vijana,Utamaduni,Sanaa  na Michezo Balozi Ali Abeid Karume (katikati) alipokuwa  akiwasilisha Taarifa ya Utekelezaji wa Mapango kazi kwa kipindi cha robo mbili Julai-Disemba 2019 kwa mwaka wa Fedha 2019/2020 katika mkutano wa Wizara hiyo uliofanyika leo katika ukumbi wa Ikulu Mjini Zanzibar,(kushoto) Naibu Waziri Lulu Msham Abdalla na Katibu Mkuu Baraza la Mapinduzi pia Katibu Mkuu Kiongozi Dkt.Abduhamid Yahya Mzee (kulia).

 Dk. Shein alikutana na uongozi wa Wizara ya Vijana, Utamaduni, Sanaa na Michezo chini ya  Waziri wake Balozi Ali Abeid Karume ambapo Waziri huyo alieleza kuwa  Wizara hiyo imefanikiwa kutekeleza Ilani ya Uchaguzi ya CCM ya mwaka 2015-2020 kwa kiasi kikubwa hasa katika sekta ya michezo.

Alieleza kuwa vijana wamewezeshwa katika shughuli za kiuchumi kwa kupatiwa vifaa mbali mbali vya kujiendeleza pamoja na kupatiwa nafasi za mafunzo kazi ili kuweza kujiajiri wenyewe kwa lengo la  kuinua pato lao na la Taifa.

Kwa upande wa utamaduni, Balozi Karume alisema kuwa Wizara imeendelea kuazimisha matamasha mbali mbali likiwemo tamasha la utamaduni wa Mzanzibari, kukiendeleza kikundi cha Taifa cha taarab kwa kukipatia vifaa na ofisi.

Akieleza kuhusu lugha ya Kiswahili alisema kuwa kongamano la Kimataifa la lugha hiyo limekuwa likifanyika kwa kushirikisha wataalamu na magwiji wa lugha hiyo kutoka ndani na nje ya nchi na kueleza jinsi Wizara hiyo inavyokuza michezo ya asili.

Aidha, Wizara hiyo ilimpongeza Rais Dk. Shein kwa azma yake ya kuanzisha Studio ya Filamu na Muziki  iliyopo Rahaleo ambapo wasanii, Taasisi za Serikali pamoja na watu binafsi wamekuwa wakiitumia kwa shughuli mbali mbali za Sanaa na kijamii.

Aliongeza kuwa  Wizara hiyo imefanikiwa kuzindua program ya Ajira kwa Vijana kwa awamu ya kwanza ambapo jumla ya vijana 3,300 (Unguja 2,102 na Pemba 1,198) wamenufaika na programu hiyo.

Rajab Mkasaba, Ikulu Zanzibar
Postal Address: 2422 Tel.:0777427449. Fax: 024 2231822 
 E-mail: rajabmkasaba@yahoo.co.uk


No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.