Waziri wa Viwanda na
Biashara, Mhe. Innocent Bashungwa akifafanua jambo kwa Waandishi wa
Habari(hawapo pichani), kuhusu bidhaa za kujinga na Covid-19, ambapo baadhi ya
wafanyabiashara wamekuwa wakipandisha bei, Waziri amewataka waache hiyo tabia
kabla ya kuchukuliwa hatua kali, kushoto ni Mkurugenzi Mkuu wa TBS. Dkt.
Ngenya, na kulia ni Mkurugenzi wa Tume ya Ushindani (FCC), John Mduma katika
mkutano na Waanshi wa Habari Jijini Dar es Salaam.
Na.
Mwandishi Wetu-MAELEZO
Serikali kupitia
Wizara ya Viwanda na Biashara, Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia Wazee
na Watoto na Taasisi mbalimbali za Serikali imejipanga vyema kukabiliana na
changamoto zinazohusiana na mapambano dhidi ya mlipuko wa ugonjwa wa Corona (Covid-19).
Katika kuhakikisha changamoto
hizo zinatatuliwa mapema hii leo Waziri Innocent Bashungwa ametembelea viwanda
vinavyozalisha sabuni na Vitakasa mikono vilivyoko Jijini Dar es Salaam
kuangalia bei ya bidhaa hiyo na kuwaagiza wafanyabiashara kuuza kuendana na bei
iliyoko sokoni.
Katika mazungumzo na
Waandishi wa Habari yaliyofanyika Jijini Dar es Salaam, Waziri Bashungwa
alisema kuwa maelekezo yaliyotolewa na Serikali yanalenga kuwasaidia wananchi
kujua hatua stahiki zinazopaswa kuchukuliwa ili kujinga na Covid-19.
“Watanzania wote
tunawiwa kuwa na mchango katika kupambana dhidi ya kuenea Covid-19, watalaam
kutoka tume ya Ushindani (FCC), katika maeneo ya kuuzia barakoa (face masks),
vikinga mkono (gloves), vitakasa mikono na kemikali za usafi wa mazingira (Hand
sanitizer and surface disinfectant) katika eneo la Dar es Salaam watalaam
wamebaini kuwepo kwa uhaba na changamoto ya kupanda bei kwa bidhaa hizo”,
Alisema Waziri Innocent Bashungwa.
Waziri Bashungwa
Amewataka wafanyabiashara kuacha njama za makusudi za kuficha bidhaa hizo kwa
kigezo cha kuadimika hali ambayo inasababisha kupungua kwa uwezo wa kujikinga
na kudhibiti ugonjwa huo wa Covid-19 kwa kuzuia maambukizi mapya.
Aidha Waziri
Bashungwa alisema kuwa Shirika la Viwango Tanzania (TBS), limebainisha kuwepo
na umuhimu wa wazalishaji wa bidhaa za kujikinga na maambukizi mapya ya
Covid-19, hususani kwa wazalishaji wa Vitakasa mikono (Hand Sanitizer) kuzingatia viwango vilivyoweka na Shirika
hilo.
“Kiwango kilichowekwa
kwa uzalishaji wa vitakasa mikono ni Na. TZS 1650: 2014, kiwango hiki
kinahusisha pia uwepo wa kileo (alcohol) ya walau asilimia 60 kuwezesha
vitakasa mikono kuweza kufanya kazi iliyokusudiwa, kwa hiyo nawaelekeza TBS
kushirikiana na wazalishaji waliopo na wapya ili kukidhi matumizi ya bidhaa
hizo ili kuwawezesha wananchi kupata bidhaa yenye kiwango bora ili kudhibiti
janga hili,” Alisema Waziri Bashungwa.
Alibainisha kuwa
Wizara ya Viwanda na Biashara kwa kushirikiana na taasisi zake imeendelea
kufanya ukaguzi na uchunguzi sokoni ili kubaini endapo kuna vitendo vyovyote
vya udanganyifu au vinavyokiuka sheria zinazosimamiwa na taasisi hizo ikiwemo
TBS katika kuzalisha, kuingiza, kusambaza na kuuza bidhaa hizo.
Aliongeza kuwa
kumekuwepo na udanganyifu wa bei za bidhaa hizo za kujinga dhidi ya Maambukizi
ya Covid-19, hususani vitakasa mikono, kwa mujibu wa Bohari Kuu ya Dawa (MSD),
mil.250 inauzwa Tsh. 5,500, lakini baadhi ya wafanyabiashara wamekuwa wakiuza
kwa Tsh. 20,000, huku mil. 60 ikiuzwa Tsh. 2,500 lakini kwenye baadhi ya
maduka wanauza kwaTsh.8,000, na amewataka wafanyabiashara kuuza
kulingana na bei iliyoko sokoni.
“Nawaelekeza TBS na
FCC kuendeleo kuchunguza bei,
uzalishwaji, uingizwaji wa bidhaa unaozingatia viwango vya ubora na
ushindani wa soko ili bidhaa hizi
zipatikane kwa urahisi , zikidhi matarajio ya matumizi na zipatikane kwa bei ya
soko, kwahiyo kwa wafanyabiashara wanaouza bidhaa hizo kwa bei ya juu
wakibainika wafutiwe leseni ili tuone wataenda kuuza wapi”, Alisema Bashungwa
Kwa Upande wake
Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Viwango nchini TBS, Dkt. Yusuph Athuman Ngenya
amewataka wananchi kuepuka habari za utengenezaji wa Vitakasa mikono, ikihusisha
uwepo wa kiwango cha Alcohol kwa asilimia 60 ambacho ndiyo kiwango cha chini
cha kutengeneza bidhaa hiyo ili iweze kupambana na Covid-19.
“Kuhusu ubora na
kiwango cha chini cha Alcohol kwenye vitakasa mikono ni asilimia 60 ambacho
kimebainishwa kwenye kiwango cha 1650: 2014 cha TBS, lakini pia tunahusika kwa
kiasi kikubwa kudhibiti bidhaa zinazoingia nchini kwahiyo tumejipanga kulinda
ubora wa vitakasa mikono hasa vinavyotoka nje ya nchi ili kupata bidhaa bora kwa
matumizi ya wananchi kujikinga na Covid-19,” Alisema Dkt.Athuman.
No comments:
Post a Comment