Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu
wa Rais Mhandisi Joseph Malongo ameongoza watumishi wa Ofisi yake katika
mazishi ya Alazaro Sokoine ambaye ni mtoto Mkubwa wa Hayati Edward Moringe
Sokoine. Mazishi hayo yamefanyika jana Monduli Juu Mkoani Arusha na kuhudhuriwa
na viongozi mbalimbali wa Serikali, ndugu, jamaa na Marafiki.
Mkurugenzi wa Utawala na
usimamizi wa Rasilimali watu Bi. Emma Lyimo akitoa heshima za mwisho katika
ibaada ya kuaga mwili wa Alazaro Sokoine ambae ni mtoto mkubwa wa Hayati Edward
Moringe Sokoine. Mazishi yamefanyika jana Monduli Mkoani Arusha.
Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya
Makamu wa Rais Balozi Joseph Sokoine
(kushoto) akiweka shada la maua pamoja wanafamilia katika kaburi la kaka yake
mkubwa Alazaro Sokoine. Mazishi yamefanyika jana Monduli Mkoani Arusha.
Wakuu wa Mikoa ya Njombe
Mhe. Christopher Ole Sendeka, Morogogo - Mhe. Loata Sanare, Tanga - Mhe. Martine
Shigela na Arusha Mhe. Mrisho Gambo wakiweka shada la maua katika kaburi la
Alazaro Sokoine, Monduli Mkoani Arusha.
No comments:
Post a Comment