Habari za Punde

Milioni 70 zachangwa na Taasisi tofauti kukabiliana na janga la Corona

Meneja wa Benki ya NMB Tawi la Zanzibar Nd. Abdulla Duchi Kushoto akimkabidhi Mkamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi mfano wa Hundi ya Shilingi Milioni 30,000,000/- zilizoingizwa kwenye Akaunti ya Corona kusaidia mapambano dhidi ya Virusi vya Corona.
Afisa Biashara Mkuu wa Benki ya CRDB Tanzania Dr. Joseph Vicent akimkabidhi Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi Hundi ya Shilingi Milioni 30,000,000/- kusaidia mapambano dhidi ya Virusi vya Corona.
Makamu Mwenyekiti wa Bodi ya Uhaulishaji wa Ardhi Zanzibar Bwana Enzi Talib Aboud akimkabidhi Balozi Seif Ali Iddi Mchango wa Uongozi wa Bodi hiyo wa Shilingi Milioni 10,000,000/- kusaidia mapambano dhidi ya virusi vya Corona
 Meneja Abdullah Duchi akisisitiza azma ya Benki yake kuendelea kusaidia Jamii pale inapotokea wajibu wa kufanya hivyo hasa kwenye matukio ya Maafa.
Meneja Abdullah Duchi akisisitiza azma ya Benki yake kuendelea kusaidia Jamii pale inapotokea wajibu wa kufanya hivyo hasa kwenye matukio ya Maafa.
Makamu Mwenyekiti wa Bodi ya Uhaulishaji wa Ardhi Zanzibar Bwana Enzi Talib Aboud akimpa taarifa Balozi Seif Ali Iddi namna Bodi hiyo ilivyoguswa na wimbi la kuenea kwa virusi vya Corona Nchini.
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi akiyapongeza Mashirika na Taasisi mbali mbali Nchini kutokana na kuguswa kwao kusaidia mapambano dhidi ya kuenea kwa maambukizo ya Virusi vya Corona.

Pichana – OMPR – ZNZ.

Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar imeendelea kupokea Michango mbali mbali ya Fedha Taslim jumla ya Shilingi Milioni Arubaini {70,000,000/-} zilizotolewa na Taasisi tofauti Nchini kwa ajili ya kusaidia nguvu za Serikali katika Mapambano yake dhidi ya kupiga vita kuenea kwa Virusi vya Corona Nchini.

Michango hiyo imetolewa na Uongozi wa Benki ya NMB iliyokabidhi Shilingi Milioni 30,000,000/-, Benki ya Maendeleo Vijijini {CRDB} Shilingi Milioni 30,000,000/- pamoja na Uongozi wa Bodi ya Uhaulishaji wa Ardhi Zanzibar Shilingi Milioni 10,000,000/-.

Akipokea Michango hiyo hapo Afisini kwake Vuga Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi alisema Mashirika na Taasisi zinazotoa huduma kwa Jamii zikiwemo zile za Kifedha zinapaswa kuendelea kuwahamasisha Wananchi katika kuzingatia njia zinazopaswa kutumiwa katika mapambano dhidi ya Virusi vya Corona.
Alisema Serikali Kuu kwa upande wake inajitahidi kutumia nguvu zake kubwa katika juhudi za kutoa elimu ili kuona ufahamu wa kutambua hatari ya kuyaepuka maradhi yanayosababishwa na Vizuri hivyo unamfikia kila Mwananchi mahali popote alipo Mijini na Vijijini.

Alisema Mashirika na Taasisi hizo kwa vile zimekuwa zikitoa huduma kila siku kwa kundi kubwa la Jamii. Hivyo  ni vyema wakaitumia fursa hiyo kuendelea kutioa elimu hata kwa kutumia vipeperushi vitakavyosaidia utoaji wa Elimu ya kujiepusha na Maradhi hayo.

Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar aliupongeza Uongozi wa Taasisi na Mashirika hayo kwa michango inayoendelea kutoa na kuwahakikishia kwamba itatumiwa kwa utafutaji wa Vifaa na zana zitakazosaidia mapambano dhidi ya kudhitibi kuenea kwa Virusi vya Corona.

Alisema Mashirika na Taasisi hizo zimeamua kutoa michango yao ya hali na mali zikielewa vyema kadhia iliyoipata Jamii na Dunia ya kuvamiwa na Janga hilo baya la  Kirusi cha Corona.

Balozi Seif  aliutanabahisha Umma kwamba ni vizuri kwa baadhi ya Watu kuacha mzaha kwa vile haustahiki kipindi hichi kizito kutokana na kidonda kikubwa cha kupotea kwa Maisha ya Watu Zaidi ya Milioni Tatu kwenye Mataifa mbali mbali Ulimwenguni.

Alikumbusha ni vyema Zanzibar ikarejea katika Historia yake ya kuwa mfano wa matukio mengi Duniani inayotoa fursa kwa baadhi ya Mataifa Duniani kufika kujifunza akitolea mfano ufanisi ulipatikana katika mapambano dhidi ya kuondoa Malaria, Kipindupindu, Ugonjwa wa Ndui na hatimae hivi sasa juhudi ziongezwe katika kupiga vita kuenea kwa Virusi vya Corona.

Mapema Meneja wa Benki ya NMB Tawi la Zanzibar Nd. Abdullah Duchi alisema mchango wa Taasisi yao ya Kifedha tayari umeshaingizwa kwenye Akaunti Maalum iliyoanzishwa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kwa ajili ya kusaidia mapambano dhidi ya Virusi vya Corona Nchini.

Alisema Uongozi wa Benki ya NMB umeguswa na tukio hilo lililoikumba Tanzania na Dunia kwa ujumla ambapo wanapaswa kuingiza nguvu zake katika kuona mapambano hayo yanafanikiwa vyema.

Nd. Abdullah aliziomba Taasisi na Mashirika mengine kujitokeza kuchangia nguvu zao kwa kushirikiana na Serikali Kuu ili kuondosha kabisa janga hilo linalomgusa kila Mwananchi hapa Nchini.

Naye Afisa Biashara Mkuu wa Benki ya CRDB Tanzania Dr. Joseph Vicent Taasisi hiyo ya kifedha Nchini imejitolea kushiriki kwenye Mapambano dhidi ya Virusi hivyo tokea kuibuka kwake kwa mara ya kwanza Nchini Tanzania huko Mkoani Kilimanjaro.
Dr. Joseph alimueleza Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar kwamba Uongozi wa Taasisi hiyo umedhamiria kusaidiana na Serikali zote mbili katika kuona ustawi wa Wananchi wote ambao ndio Mtaji mkubwa wa kazi zao kwa kuongeza Mapato unaendelea kuimarika vyema.

Kwa upande wake Makamo Mwenyekiti wa Bodi ua Uhaulishaji  wa Ardhi Zanzibar Bwana Enzi Talib Aboud alisema Uongozi wa Bodi hiyo umeguswa na janga hilo pamoja na kufanya vyema katika majukumu yake ya kila siku ya ushughulikiaji na ufuatiliaji wa masuala ya Ardhi lakini umelazimika kushirikiana na Taasisi nyengine Nchini katika kuungana na Serikali kwenye mapambano hayo.

Bwana Enzi alisema mapambano dhidi ya Virusi vya Corona {COVIC – 19} yanapaswa kushirikisha kila Taasisi, Mashirika ya Umma, yale ya Kimataifa na hata Jamii ili kuiona Zanzibar na Tanzania kwa ujumla inabakia salama.

Alisema Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania ikijumuisha Bara na Zanzibar bado inaendelea kuwa na unafuu wa kukumbwa na janga hilo la Virusi vya Corona ikilinganishwa na Mataifa mengine Duniani yakiwemo pia hata yake jirani ya Afrika Mashariki.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.